< Psalms 3 >

1 A Psalm by David, when he fled from Absalom his son. LORD, how my adversaries have increased! Many are those who rise up against me.
Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
2 Many there are who say of my soul, “There is no help for him in God.” (Selah)
Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
3 But you, LORD, are a shield around me, my glory, and the one who lifts up my head.
Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
4 I cry to the LORD with my voice, and he answers me out of his holy hill. (Selah)
Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
5 I laid myself down and slept. I awakened, for the LORD sustains me.
Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
6 I will not be afraid of tens of thousands of people who have set themselves against me on every side.
Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
7 Arise, LORD! Save me, my God! For you have struck all of my enemies on the cheek bone. You have broken the teeth of the wicked.
Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
8 Salvation belongs to the LORD. May your blessing be on your people. (Selah)
Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.

< Psalms 3 >