< Psalms 2 >

1 Why do the nations rage, and the peoples plot a vain thing?
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 The kings of the earth take a stand, and the rulers take counsel together, against the LORD, and against his Anointed, saying,
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 “Let’s break their bonds apart, and cast their cords from us.”
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 He who sits in the heavens will laugh. The Lord will have them in derision.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Then he will speak to them in his anger, and terrify them in his wrath:
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 “Yet I have set my King on my holy hill of Zion.”
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 I will tell of the decree: The LORD said to me, “You are my son. Today I have become your father.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Ask of me, and I will give the nations for your inheritance, the uttermost parts of the earth for your possession.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 You shall break them with a rod of iron. You shall dash them in pieces like a potter’s vessel.”
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Now therefore be wise, you kings. Be instructed, you judges of the earth.
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Serve the LORD with fear, and rejoice with trembling.
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Give sincere homage to the Son, lest he be angry, and you perish on the way, for his wrath will soon be kindled. Blessed are all those who take refuge in him.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

< Psalms 2 >