< Psalms 146 >

1 Praise the LORD! Praise the LORD, my soul.
Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
2 While I live, I will praise the LORD. I will sing praises to my God as long as I exist.
Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
3 Do not put your trust in princes, in a son of man in whom there is no help.
Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
4 His spirit departs, and he returns to the earth. In that very day, his thoughts perish.
Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
5 Happy is he who has the God of Jacob for his help, whose hope is in the LORD, his God,
Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
6 who made heaven and earth, the sea, and all that is in them; who keeps truth forever;
Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
7 who executes justice for the oppressed; who gives food to the hungry. The LORD frees the prisoners.
Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
8 The LORD opens the eyes of the blind. The LORD raises up those who are bowed down. The LORD loves the righteous.
Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
9 The LORD preserves the foreigners. He upholds the fatherless and widow, but he turns the way of the wicked upside down.
Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
10 The LORD will reign forever; your God, O Zion, to all generations. Praise the LORD!
Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.

< Psalms 146 >