< Psalms 138 >

1 By David. I will give you thanks with my whole heart. Before the gods, I will sing praises to you.
Zaburi ya Daudi. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, kwa moyo wangu wote, mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.
2 I will bow down toward your holy temple, and give thanks to your Name for your loving kindness and for your truth; for you have exalted your Name and your Word above all.
Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu, nami nitalisifu jina lako kwa ajili ya upendo wako na uaminifu, kwa kuwa umelikuza jina lako na neno lako juu ya vitu vyote.
3 In the day that I called, you answered me. You encouraged me with strength in my soul.
Nilipoita, ulinijibu; ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.
4 All the kings of the earth will give you thanks, LORD, for they have heard the words of your mouth.
Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Bwana, wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.
5 Yes, they will sing of the ways of the LORD, for the LORD’s glory is great!
Wao na waimbe kuhusu njia za Bwana, kwa maana utukufu wa Bwana ni mkuu.
6 For though the LORD is high, yet he looks after the lowly; but he knows the proud from afar.
Ingawa Bwana yuko juu, humwangalia mnyonge, bali mwenye kiburi yeye anamjua kutokea mbali.
7 Though I walk in the middle of trouble, you will revive me. You will stretch out your hand against the wrath of my enemies. Your right hand will save me.
Nijapopita katikati ya shida, wewe unayahifadhi maisha yangu, unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.
8 The LORD will fulfill that which concerns me. Your loving kindness, LORD, endures forever. Do not forsake the works of your own hands.
Bwana atatimiza kusudi lake kwangu, Ee Bwana, upendo wako wadumu milele: usiziache kazi za mikono yako.

< Psalms 138 >