< Psalms 135 >

1 Praise the LORD! Praise the LORD’s name! Praise him, you servants of the LORD,
Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
2 you who stand in the LORD’s house, in the courts of our God’s house.
ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Praise the LORD, for the LORD is good. Sing praises to his name, for that is pleasant.
Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4 For the LORD has chosen Jacob for himself, Israel for his own possession.
Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5 For I know that the LORD is great, that our Lord is above all gods.
Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6 Whatever the LORD pleased, that he has done, in heaven and in earth, in the seas and in all deeps.
Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7 He causes the clouds to rise from the ends of the earth. He makes lightnings with the rain. He brings the wind out of his treasuries.
Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8 He struck the firstborn of Egypt, both of man and animal.
Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9 He sent signs and wonders into the middle of you, Egypt, on Pharaoh, and on all his servants.
Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 He struck many nations, and killed mighty kings—
Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11 Sihon king of the Amorites, Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan—
Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12 and gave their land for a heritage, a heritage to Israel, his people.
Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
13 Your name, LORD, endures forever; your renown, LORD, throughout all generations.
Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
14 For the LORD will judge his people and have compassion on his servants.
Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
15 The idols of the nations are silver and gold, the work of men’s hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16 They have mouths, but they cannot speak. They have eyes, but they cannot see.
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17 They have ears, but they cannot hear, neither is there any breath in their mouths.
zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18 Those who make them will be like them, yes, everyone who trusts in them.
Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19 House of Israel, praise the LORD! House of Aaron, praise the LORD!
Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20 House of Levi, praise the LORD! You who fear the LORD, praise the LORD!
Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
21 Blessed be the LORD from Zion, who dwells in Jerusalem. Praise the LORD!
Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.

< Psalms 135 >