< Psalms 135 >

1 Praise the LORD! Praise the LORD’s name! Praise him, you servants of the LORD,
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 you who stand in the LORD’s house, in the courts of our God’s house.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Praise the LORD, for the LORD is good. Sing praises to his name, for that is pleasant.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 For the LORD has chosen Jacob for himself, Israel for his own possession.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 For I know that the LORD is great, that our Lord is above all gods.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Whatever the LORD pleased, that he has done, in heaven and in earth, in the seas and in all deeps.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 He causes the clouds to rise from the ends of the earth. He makes lightnings with the rain. He brings the wind out of his treasuries.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 He struck the firstborn of Egypt, both of man and animal.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 He sent signs and wonders into the middle of you, Egypt, on Pharaoh, and on all his servants.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 He struck many nations, and killed mighty kings—
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Sihon king of the Amorites, Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan—
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 and gave their land for a heritage, a heritage to Israel, his people.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Your name, LORD, endures forever; your renown, LORD, throughout all generations.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 For the LORD will judge his people and have compassion on his servants.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 The idols of the nations are silver and gold, the work of men’s hands.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 They have mouths, but they cannot speak. They have eyes, but they cannot see.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 They have ears, but they cannot hear, neither is there any breath in their mouths.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Those who make them will be like them, yes, everyone who trusts in them.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 House of Israel, praise the LORD! House of Aaron, praise the LORD!
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 House of Levi, praise the LORD! You who fear the LORD, praise the LORD!
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Blessed be the LORD from Zion, who dwells in Jerusalem. Praise the LORD!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalms 135 >