< Psalms 129 >

1 A Song of Ascents. Many times they have afflicted me from my youth up. Let Israel now say:
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia,” Israeli na iseme.
2 many times they have afflicted me from my youth up, yet they have not prevailed against me.
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia, lakini hawajanishinda.
3 The plowers plowed on my back. They made their furrows long.
Wakulima wamekuwa wakilima mgonngoni kwangu; wametengeneza matuta yao marefu.
4 The LORD is righteous. He has cut apart the cords of the wicked.
Yahwe ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.”
5 Let them be disappointed and turned backward, all those who hate Zion.
Wote waaibishwe na kurudishwa nyuma, wale wachukiao Sayuni.
6 Let them be as the grass on the housetops, which withers before it grows up,
Na wawe kama nyasi juu ya paa ambayo hunyauka kabla hayajakua,
7 with which the reaper does not fill his hand, nor he who binds sheaves, his bosom.
ambayo hayawezi kujaza mkono wa mvunaji wala kifua cha mfunga miganda.
8 Neither do those who go by say, “The blessing of the LORD be on you. We bless you in the LORD’s name.”
Wale wapitao karibu wasiseme, “Baraka za Mungu na ziwe juu yako; Tunakubariki katika jina la Yahwe.”

< Psalms 129 >