< Psalms 127 >

1 A Song of Ascents. By Solomon. Unless the LORD builds the house, they who build it labor in vain. Unless the LORD watches over the city, the watchman guards it in vain.
Yahwe asipoijenga nyumba, waijengao wafanya kazi bure. Yahwe asipoulinda mji, aulindaye afanya kazi bure.
2 It is vain for you to rise up early, to stay up late, eating the bread of toil, for he gives sleep to his loved ones.
Ni kazi bure kwa wewe unayeamka mapema, na kulala kwa kuchelewa, au kula mkate kwa kuufanyia kazi ngumu, maana Yahwe huwapa chakula awapendao hata wawapo usingizini.
3 Behold, children are a heritage of the LORD. The fruit of the womb is his reward.
Tazama, wana ni urithi kutoka kwa Yahwe, uzao wa tumbo ni thawabu kutoka kwake.
4 As arrows in the hand of a mighty man, so are the children of youth.
Kama mishale mkononi mwa shujaa, ndivyo walivyo wana wa ujanani.
5 Happy is the man who has his quiver full of them. They will not be disappointed when they speak with their enemies in the gate.
Ni namna gani alivyo barikiwa mtu ambaye amelijaza podo lake hivyo. Hata aibishwa pindi atakapo kabiliana na adui zake katika lango.

< Psalms 127 >