< Proverbs 9 >

1 Wisdom has built her house. She has carved out her seven pillars.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 She has prepared her meat. She has mixed her wine. She has also set her table.
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 She has sent out her maidens. She cries from the highest places of the city:
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 “Whoever is simple, let him turn in here!” As for him who is void of understanding, she says to him,
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 “Come, eat some of my bread, Drink some of the wine which I have mixed!
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 Leave your simple ways, and live. Walk in the way of understanding.”
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 One who corrects a mocker invites insult. One who reproves a wicked man invites abuse.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 Do not reprove a scoffer, lest he hate you. Reprove a wise person, and he will love you.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Instruct a wise person, and he will be still wiser. Teach a righteous person, and he will increase in learning.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 The fear of the LORD is the beginning of wisdom. The knowledge of the Holy One is understanding.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 For by me your days will be multiplied. The years of your life will be increased.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 If you are wise, you are wise for yourself. If you mock, you alone will bear it.
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 The foolish woman is loud, undisciplined, and knows nothing.
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 She sits at the door of her house, on a seat in the high places of the city,
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 to call to those who pass by, who go straight on their ways,
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 “Whoever is simple, let him turn in here.” As for him who is void of understanding, she says to him,
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 “Stolen water is sweet. Food eaten in secret is pleasant.”
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 But he does not know that the departed spirits are there, that her guests are in the depths of Sheol (Sheol h7585).
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)

< Proverbs 9 >