< Proverbs 14 >

1 Every wise woman builds her house, but the foolish one tears it down with her own hands.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 He who walks in his uprightness fears the LORD, but he who is perverse in his ways despises him.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 The fool’s talk brings a rod to his back, but the lips of the wise protect them.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Where no oxen are, the crib is clean, but much increase is by the strength of the ox.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 A truthful witness will not lie, but a false witness pours out lies.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 A scoffer seeks wisdom, and does not find it, but knowledge comes easily to a discerning person.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Stay away from a foolish man, for you will not find knowledge on his lips.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 The wisdom of the prudent is to think about his way, but the folly of fools is deceit.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Fools mock at making atonement for sins, but among the upright there is good will.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 The heart knows its own bitterness and joy; he will not share these with a stranger.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 The house of the wicked will be overthrown, but the tent of the upright will flourish.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 There is a way which seems right to a man, but in the end it leads to death.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Even in laughter the heart may be sorrowful, and mirth may end in heaviness.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 The unfaithful will be repaid for his own ways; likewise a good man will be rewarded for his ways.
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 A simple man believes everything, but the prudent man carefully considers his ways.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 A wise man fears and shuns evil, but the fool is hot headed and reckless.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 He who is quick to become angry will commit folly, and a crafty man is hated.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 The simple inherit folly, but the prudent are crowned with knowledge.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 The evil bow down before the good, and the wicked at the gates of the righteous.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 The poor person is shunned even by his own neighbor, but the rich person has many friends.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 He who despises his neighbor sins, but he who has pity on the poor is blessed.
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 Do not they go astray who plot evil? But love and faithfulness belong to those who plan good.
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 In all hard work there is profit, but the talk of the lips leads only to poverty.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 The crown of the wise is their riches, but the folly of fools crowns them with folly.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 A truthful witness saves souls, but a false witness is deceitful.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 In the fear of the LORD is a secure fortress, and he will be a refuge for his children.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 The fear of the LORD is a fountain of life, turning people from the snares of death.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 In the multitude of people is the king’s glory, but in the lack of people is the destruction of the prince.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 He who is slow to anger has great understanding, but he who has a quick temper displays folly.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 The life of the body is a heart at peace, but envy rots the bones.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 He who oppresses the poor shows contempt for his Maker, but he who is kind to the needy honors him.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 The wicked is brought down in his calamity, but in death, the righteous has a refuge.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 Wisdom rests in the heart of one who has understanding, and is even made known in the inward part of fools.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 Righteousness exalts a nation, but sin is a disgrace to any people.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 The king’s favor is toward a servant who deals wisely, but his wrath is toward one who causes shame.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< Proverbs 14 >