< Proverbs 10 >

1 The proverbs of Solomon. A wise son makes a glad father; but a foolish son brings grief to his mother.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Treasures of wickedness profit nothing, but righteousness delivers from death.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 The LORD will not allow the soul of the righteous to go hungry, but he thrusts away the desire of the wicked.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 He becomes poor who works with a lazy hand, but the hand of the diligent brings wealth.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 He who gathers in summer is a wise son, but he who sleeps during the harvest is a son who causes shame.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Blessings are on the head of the righteous, but violence covers the mouth of the wicked.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 The memory of the righteous is blessed, but the name of the wicked will rot.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 The wise in heart accept commandments, but a chattering fool will fall.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 He who walks blamelessly walks surely, but he who perverts his ways will be found out.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 One who winks with the eye causes sorrow, but a chattering fool will fall.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 The mouth of the righteous is a spring of life, but violence covers the mouth of the wicked.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 Hatred stirs up strife, but love covers all wrongs.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 Wisdom is found on the lips of him who has discernment, but a rod is for the back of him who is void of understanding.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Wise men lay up knowledge, but the mouth of the foolish is near ruin.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 The rich man’s wealth is his strong city. The destruction of the poor is their poverty.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 The labor of the righteous leads to life. The increase of the wicked leads to sin.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 He is in the way of life who heeds correction, but he who forsakes reproof leads others astray.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 He who hides hatred has lying lips. He who utters a slander is a fool.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 In the multitude of words there is no lack of disobedience, but he who restrains his lips does wisely.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 The tongue of the righteous is like choice silver. The heart of the wicked is of little worth.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 The lips of the righteous feed many, but the foolish die for lack of understanding.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 The LORD’s blessing brings wealth, and he adds no trouble to it.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 It is a fool’s pleasure to do wickedness, but wisdom is a man of understanding’s pleasure.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 What the wicked fear will overtake them, but the desire of the righteous will be granted.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 When the whirlwind passes, the wicked is no more; but the righteous stand firm forever.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 As vinegar to the teeth, and as smoke to the eyes, so is the sluggard to those who send him.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 The fear of the LORD prolongs days, but the years of the wicked shall be shortened.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 The prospect of the righteous is joy, but the hope of the wicked will perish.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 The way of the LORD is a stronghold to the upright, but it is a destruction to the workers of iniquity.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 The righteous will never be removed, but the wicked will not dwell in the land.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 The mouth of the righteous produces wisdom, but the perverse tongue will be cut off.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 The lips of the righteous know what is acceptable, but the mouth of the wicked is perverse.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.

< Proverbs 10 >