< Numbers 28 >

1 The LORD spoke to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Command the children of Israel, and tell them, ‘See that you present my offering, my food for my offerings made by fire, as a pleasant aroma to me, in their due season.’
“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
3 You shall tell them, ‘This is the offering made by fire which you shall offer to the LORD: male lambs a year old without defect, two day by day, for a continual burnt offering.
Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
4 You shall offer the one lamb in the morning, and you shall offer the other lamb at evening,
Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
5 with one tenth of an ephah of fine flour for a meal offering, mixed with the fourth part of a hin of beaten oil.
kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
6 It is a continual burnt offering which was ordained in Mount Sinai for a pleasant aroma, an offering made by fire to the LORD.
Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
7 Its drink offering shall be the fourth part of a hin for each lamb. You shall pour out a drink offering of strong drink to the LORD in the holy place.
Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
8 The other lamb you shall offer at evening. As the meal offering of the morning, and as its drink offering, you shall offer it, an offering made by fire, for a pleasant aroma to the LORD.
Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
9 “‘On the Sabbath day, you shall offer two male lambs a year old without defect, and two tenths of an ephah of fine flour for a meal offering mixed with oil, and its drink offering:
“‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
10 this is the burnt offering of every Sabbath, in addition to the continual burnt offering and its drink offering.
Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
11 “‘In the beginnings of your months, you shall offer a burnt offering to the LORD: two young bulls, one ram, seven male lambs a year old without defect,
“‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
12 and three tenths of an ephah of fine flour for a meal offering mixed with oil, for each bull; and two tenth parts of fine flour for a meal offering mixed with oil, for the one ram;
Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
13 and one tenth part of fine flour mixed with oil for a meal offering to every lamb, as a burnt offering of a pleasant aroma, an offering made by fire to the LORD.
pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
14 Their drink offerings shall be half a hin of wine for a bull, the third part of a hin for the ram, and the fourth part of a hin for a lamb. This is the burnt offering of every month throughout the months of the year.
Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
15 Also, one male goat for a sin offering to the LORD shall be offered in addition to the continual burnt offering and its drink offering.
Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
16 “‘In the first month, on the fourteenth day of the month, is the LORD’s Passover.
“‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
17 On the fifteenth day of this month shall be a feast. Unleavened bread shall be eaten for seven days.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
18 In the first day shall be a holy convocation. You shall do no regular work,
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
19 but you shall offer an offering made by fire, a burnt offering to the LORD: two young bulls, one ram, and seven male lambs a year old. They shall be without defect,
Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
20 with their meal offering, fine flour mixed with oil. You shall offer three tenths for a bull, and two tenths for the ram.
Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
21 You shall offer one tenth for every lamb of the seven lambs;
pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
22 and one male goat for a sin offering, to make atonement for you.
Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 You shall offer these in addition to the burnt offering of the morning, which is for a continual burnt offering.
Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
24 In this way you shall offer daily, for seven days, the food of the offering made by fire, of a pleasant aroma to the LORD. It shall be offered in addition to the continual burnt offering and its drink offering.
Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
25 On the seventh day you shall have a holy convocation. You shall do no regular work.
Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
26 “‘Also in the day of the first fruits, when you offer a new meal offering to the LORD in your feast of weeks, you shall have a holy convocation. You shall do no regular work;
“‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
27 but you shall offer a burnt offering for a pleasant aroma to the LORD: two young bulls, one ram, seven male lambs a year old;
Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
28 and their meal offering, fine flour mixed with oil, three tenths for each bull, two tenths for the one ram,
Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
29 one tenth for every lamb of the seven lambs;
na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
30 and one male goat, to make atonement for you.
Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 Besides the continual burnt offering and its meal offering, you shall offer them and their drink offerings. See that they are without defect.
Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

< Numbers 28 >