< Matthew 7 >

1 “Do not judge, so that you will not be judged.
Usihukumu, nawe usije ukahukumiwa.
2 For with whatever judgment you judge, you will be judged; and with whatever measure you measure, it will be measured to you.
Kwa hukumu unayohukumu, nawe utahukumiwa. Na kwa kipimo unachopima na wewe pia utapimiwa hicho hicho.
3 Why do you see the speck that is in your brother’s eye, but do not consider the beam that is in your own eye?
Na kwa nini unatazama kipande cha mti kilichoko kwenye jicho la ndugu yako, lakini hutambuwi kipande cha gogo ambalo limo katika jicho lako?
4 Or how will you tell your brother, ‘Let me remove the speck from your eye,’ and behold, the beam is in your own eye?
Unawezaje kusema kwa ndugu yako, ngoja nikutolee kipande kilichomo kwenye jicho lako, wakati kipande cha gogo kimo ndani ya jicho lako?
5 You hypocrite! First remove the beam out of your own eye, and then you can see clearly to remove the speck out of your brother’s eye.
Mnafiki wewe; kwanza toa gogo lililomo kwenye jicho lako, na ndipo utakapoweza kuona vizuri na kukitoa kipande cha mti kilichomo kwenye jicho la ndugu yako.
6 “Do not give that which is holy to the dogs, neither throw your pearls before the pigs, lest perhaps they trample them under their feet, and turn and tear you to pieces.
Usiwape mbwa kilicho kitakatifu, na usiwarushie nguruwe lulu mbele yao. Vinginevyo wataviharibu na kuvikanyaga kwa miguu, na tena watakugeukia wewe na kukurarua vipande vipande.
7 “Ask, and it will be given you. Seek, and you will find. Knock, and it will be opened for you.
Omba, nawe utapewa. Tafuta, nawe utapata. Bisha hodi, na wewe utafunguliwa.
8 For everyone who asks receives. He who seeks finds. To him who knocks it will be opened.
Kwa yeyote anayeomba, hupokea. Na kwa yeyote anayetafuta, hupata. Na kwa mtu ambaye anayebisha hodi, atafunguliwa.
9 Or who is there among you who, if his son asks him for bread, will give him a stone?
Au kuna mtu miongoni mwenu ambaye, ikiwa mtoto wake amemwomba kipande cha mkate atampa jiwe?
10 Or if he asks for a fish, who will give him a serpent?
Au ikiwa atamwomba samaki, na yeye atampa nyoka?
11 If you then, being evil, know how to give good gifts to your children, how much more will your Father who is in heaven give good things to those who ask him!
Kwa hiyo, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, Je! Ni kiasi gani zaidi Baba aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wanao muomba yeye?
12 Therefore, whatever you desire for men to do to you, you shall also do to them; for this is the law and the prophets.
Kwa sababu hiyo, unapotaka kufanyiwa kitu chochote na watu wengine, nawe pia itakupasa kuwafanyia hivyo hivyo wao. Kwa kuwa hiyo ni sheria na manabii.
13 “Enter in by the narrow gate; for the gate is wide and the way is broad that leads to destruction, and there are many who enter in by it.
Ingieni kwa kupitia geti jembamba. Kwa kuwa geti ni pana na njia ni pana inayoongoza kwenye uharibifu, na kuna watu wengi wanaopitia njia hiyo.
14 How narrow is the gate and the way is restricted that leads to life! There are few who find it.
Geti ni jembamba, Geti jembamba ni njia inayongooza katika uzima na ni wachache wanaoweza kuiona.
15 “Beware of false prophets, who come to you in sheep’s clothing, but inwardly are ravening wolves.
Jihadhari na manabii wa uongo, wanaokuja wamevaa ngozi ya kondoo, lakini kweli ni mbweha wakali.
16 By their fruits you will know them. Do you gather grapes from thorns or figs from thistles?
Kwa matunda yao mtawatambua. Je watu wanaweza kuvuna matunda kwenye miba, au mtini kwenye mbengu ya mbaruti?
17 Even so, every good tree produces good fruit, but the corrupt tree produces evil fruit.
Kwa jinsi hiyo, kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini mti mbaya huzaa matunda mabaya.
18 A good tree cannot produce evil fruit, neither can a corrupt tree produce good fruit.
Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
19 Every tree that does not grow good fruit is cut down and thrown into the fire.
Kila mti ambao hauzai matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.
20 Therefore by their fruits you will know them.
Hivyo basi, utawatambua kutokana na matunda yao.
21 “Not everyone who says to me, ‘Lord, Lord,’ will enter into the Kingdom of Heaven, but he who does the will of my Father who is in heaven.
Si kila mtu aniambiaye mimi, 'Bwana, Bwana,' ataingia katika ufalme wa mbinguni, bali ni yule pekee atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Many will tell me in that day, ‘Lord, Lord, did not we prophesy in your name, in your name cast out demons, and in your name do many mighty works?’
Watu wengi wataniambia siku hiyo, 'Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, hatukutoa mapepo kwa jina lako, na kwa jina lako tulifanya matendo mengi makuu?'
23 Then I will tell them, ‘I never knew you. Depart from me, you who work iniquity.’
Ndipo nitawaambia wazi, 'sikuwatambua ninyi! Ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu!'
24 “Everyone therefore who hears these words of mine and does them, I will liken him to a wise man who built his house on a rock.
Kwa hiyo, kila mmoja asikiaye maneno yangu na kutii atafanana na mtu mwenye hekima aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
25 The rain came down, the floods came, and the winds blew and beat on that house; and it did not fall, for it was founded on the rock.
Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na ukaipiga nyumba hiyo, lakini haikuweza kuanguka chini, kwa kuwa ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.
26 Everyone who hears these words of mine and does not do them will be like a foolish man who built his house on the sand.
Lakini kila mtu anayesikia neno langu na asilitii, atafananishwa na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
27 The rain came down, the floods came, and the winds blew and beat on that house; and it fell—and its fall was great.”
Mvua ikaja, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na kuipiga nyumba hiyo. Na ikaanguka, na uharibifu wake ukakamilika.”
28 When Jesus had finished saying these things, the multitudes were astonished at his teaching,
Ulifika wakati ambao Yesu alipomaliza kuongea maneno haya, makutano walishangazwa na mafundisho yake,
29 for he taught them with authority, and not like the scribes.
kwa kuwa alifundisha kama mtu mwenye mamlaka, na si kama waandishi wao.

< Matthew 7 >