< Matthew 15 >

1 Then Pharisees and scribes came to Jesus from Jerusalem, saying,
Ndipo Mafarisayo na waadishi walikuja kwa Yesu kutoka Yerusalemu. Na kusema,
2 “Why do your disciples disobey the tradition of the elders? For they do not wash their hands when they eat bread.”
“Kwa nini wanafunzi wanayahalifu mapokeo ya wazee? Kwa kuwa hawanawi mikono yao wanapokuwa wanakula chakula.''
3 He answered them, “Why do you also disobey the commandment of God because of your tradition?
Yesu akawajibu na kuwaambia, “Nanyi kwa nini mnaihalifu sheria ya Bwana kwa ajili ya mapokeo yenu?
4 For God commanded, ‘Honor your father and your mother,’ and, ‘He who speaks evil of father or mother, let him be put to death.’
Kwa kuwa Mungu alisema, 'Mheshimu baba yako na mama yako; na 'Asemaye uovu kwa baba yake na mama yake, hakika atakufa.'
5 But you say, ‘Whoever may tell his father or his mother, “Whatever help you might otherwise have gotten from me is a gift devoted to God,”
Lakini ninyi husema, 'Kila amwambiaye baba yake na mama yake, '“Kila msaada ambao angepata kutoka kwangu sasa ni zawadi kutoka kwa Mungu,'''
6 he shall not honor his father or mother.’ You have made the commandment of God void because of your tradition.
“Mtu huyo hana haja ya kumuheshimu baba yake. Katika namna hii mmelitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.
7 You hypocrites! Well did Isaiah prophesy of you, saying,
Enyi wanafiki, ni vema kama Isaya alivyo tabiri juu yenu aliposema,
8 ‘These people draw near to me with their mouth, and honor me with their lips; but their heart is far from me.
'Watu hawa wananiheshimu mimi kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
9 And they worship me in vain, teaching as doctrine rules made by men.’”
Wananiabudu bure, kwa sababu wanafundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”'
10 He summoned the multitude, and said to them, “Hear, and understand.
Ndipo akawaita makutano na kuwaambia,” Sikilizeni na mfahamu
11 That which enters into the mouth does not defile the man; but that which proceeds out of the mouth, this defiles the man.”
Hakuna kitu kiingiacho mdomoni mwa mtu na kumfanya najisi. Bali, kile kitokacho kinywani, hiki ndicho kimfanyacho mtu kuwa najisi.''
12 Then the disciples came and said to him, “Do you know that the Pharisees were offended when they heard this saying?”
Ndipo wanafunzi wakamwendea na kusema na Yesu, “Je!, Unafahamu Mafarisayo walipolisikia lile neno walikwazika?”
13 But he answered, “Every plant which my heavenly Father did not plant will be uprooted.
Yesu aliwajibu na kusema, “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hajaupanda utang'olewa.
14 Leave them alone. They are blind guides of the blind. If the blind guide the blind, both will fall into a pit.”
Waacheni pekee, wao ni viongozi vipofu. Kama mtu kipofu atamuongoza kipofu mwenzake, wote wawili wataanguka shimoni.”
15 Peter answered him, “Explain the parable to us.”
Petro akajibu na kumwambia Yesu,” Tuelezee mfano huu kwetu,
16 So Jesus said, “Do you also still not understand?
Yesu akajibu, ''Nanyi pia bado hamuelewi?
17 Do not you understand that whatever goes into the mouth passes into the belly and then out of the body?
Ninyi hamuoni kuwa kila kiendacho mdomoni hupitia tumboni na kwenda chooni?
18 But the things which proceed out of the mouth come out of the heart, and they defile the man.
Lakini vitu vyote vitokavyo mdomoni hutoka ndani ya moyo. Ndivyo vitu vimtiavyo mtu unajisi.
19 For out of the heart come evil thoughts, murders, adulteries, sexual sins, thefts, false testimony, and blasphemies.
Kwa kuwa katika moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo, na matusi.
20 These are the things which defile the man; but to eat with unwashed hands does not defile the man.”
Haya ndiyo mambo yamtiayo mtu unajisi. Lakini kula bila kunawa mikono hakumfanyi mtu kuwa najisi.”
21 Jesus went out from there and withdrew into the region of Tyre and Sidon.
Ndipo Yesu akatoka mahali pale na akajitenga kuelekea pande za miji ya Tiro na Sidoni.
22 Behold, a Canaanite woman came out from those borders and cried, saying, “Have mercy on me, Lord, you son of David! My daughter is severely possessed by a demon!”
Tazama akaja mwanamke Mkanani kutoka pande hizo. Akapaza sauti akisema, ''Nihurumie, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu anateswa sana na pepo.''
23 But he answered her not a word. His disciples came and begged him, saying, “Send her away; for she cries after us.”
Lakini Yesu hakumjibu neno. Wanafunzi wake wakaja wakimsihi, wakisema, ''Muondoe aende zake, maana anatupigia kelele.''
24 But he answered, “I was not sent to anyone but the lost sheep of the house of Israel.”
Yesu aliwajibu na kusema, Sikutumwa kwa mtu yeyoye isipokuwa kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.''
25 But she came and worshiped him, saying, “Lord, help me.”
Lakini alikuja na kuinama mbele yake, akisema, ''Bwana nisaidie.''
26 But he answered, “It is not appropriate to take the children’s bread and throw it to the dogs.”
Alimjibu na kusema, “Siyo vema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa,”
27 But she said, “Yes, Lord, but even the dogs eat the crumbs which fall from their masters’ table.”
Akasema, “Ndiyo, Bwana, hata hivyo mbwa wadogo hula chakula kiagukacho mezani mwa Bwana wao.”
28 Then Jesus answered her, “Woman, great is your faith! Be it done to you even as you desire.” And her daughter was healed from that hour.
Ndipo Yesu akajibu na akisema “Mwanamke, imani yako ni kubwa. Na ifanyike kwako kama utakavyo.” Na binti yake alikuwa ameponywa katika wakati huo.
29 Jesus departed from there and came near to the sea of Galilee; and he went up on the mountain and sat there.
Yesu aliondoka mahali pale na kwenda karibu na bahari ya Galilaya. Kisha alienda juu ya mlima na kuketi huko.
30 Great multitudes came to him, having with them the lame, blind, mute, maimed, and many others, and they put them down at his feet. He healed them,
Kundi kubwa likaja kwake. Na kumletea viwete, vipofu, bubu, vilema na wengine wengi, waliokuwa wagonjwa. Waliwaweka katika miguu ya Yesu na akawaponya.
31 so that the multitude wondered when they saw the mute speaking, the injured healed, the lame walking, and the blind seeing—and they glorified the God of Israel.
Nao umati wakashangaa walipoona mabubu wakiongea, na vilema wakifanywa wazima, viwete wakitembea, na vipofu wakiona. Walimsifu Mungu wa Israeli.
32 Jesus summoned his disciples and said, “I have compassion on the multitude, because they have continued with me now three days and have nothing to eat. I do not want to send them away fasting, or they might faint on the way.”
Yesu akawaita wanafunzi wake na kusema, “Nimewaonea huruma umati, kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu bila kula kitu chochote. Sitawaaga waende kwao bila kula, wasije wakazimia njiani.”
33 The disciples said to him, “Where could we get so many loaves in a deserted place as to satisfy so great a multitude?”
Wanafunzi wake wakamwambia, “Ni wapi tunaweza kupata mikate ya kutosha hapa nyikani kushibisha umati mkuwbwa hivi?”
34 Jesus said to them, “How many loaves do you have?” They said, “Seven, and a few small fish.”
Yesu akawaambia, “Mna mikate mingapi?” Wakasema, “Saba, na samaki wadogo wachache.”
35 He commanded the multitude to sit down on the ground;
Yesu akawaamuru umati uketi chini.
36 and he took the seven loaves and the fish. He gave thanks and broke them, and gave to the disciples, and the disciples to the multitudes.
Aliitwaa ile mikate saba na samaki, na baada ya kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi. Wanafunzi wakawapa umati.
37 They all ate and were filled. They took up seven baskets full of the broken pieces that were left over.
Watu wote wakala na kutosheka. Na wakakusanya mabaki ya vipande vya chakula vilivyosalia vipande vipande, vilijaa vikapu saba.
38 Those who ate were four thousand men, in addition to women and children.
Wote waliokula walikuwa wanaume elfu nne bila wanawake na watoto.
39 Then he sent away the multitudes, got into the boat, and came into the borders of Magdala.
Kisha Yesu akauaga umati waende zao na akaingia ndani ya mashua na kwenda sehemu za Magadani.

< Matthew 15 >