< Joshua 15 >

1 The lot for the tribe of the children of Judah according to their families was to the border of Edom, even to the wilderness of Zin southward, at the uttermost part of the south.
Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
2 Their south border was from the uttermost part of the Salt Sea, from the bay that looks southward;
Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
3 and it went out southward of the ascent of Akrabbim, and passed along to Zin, and went up by the south of Kadesh Barnea, and passed along by Hezron, went up to Addar, and turned toward Karka;
Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
4 and it passed along to Azmon, went out at the brook of Egypt; and the border ended at the sea. This shall be your south border.
Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
5 The east border was the Salt Sea, even to the end of the Jordan. The border of the north quarter was from the bay of the sea at the end of the Jordan.
Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
6 The border went up to Beth Hoglah, and passed along by the north of Beth Arabah; and the border went up to the stone of Bohan the son of Reuben.
Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
7 The border went up to Debir from the valley of Achor, and so northward, looking toward Gilgal, that faces the ascent of Adummim, which is on the south side of the river. The border passed along to the waters of En Shemesh, and ended at En Rogel.
Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
8 The border went up by the valley of the son of Hinnom to the side of the Jebusite (also called Jerusalem) southward; and the border went up to the top of the mountain that lies before the valley of Hinnom westward, which is at the farthest part of the valley of Rephaim northward.
kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
9 The border extended from the top of the mountain to the spring of the waters of Nephtoah, and went out to the cities of Mount Ephron; and the border extended to Baalah (also called Kiriath Jearim);
Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
10 and the border turned about from Baalah westward to Mount Seir, and passed along to the side of Mount Jearim (also called Chesalon) on the north, and went down to Beth Shemesh, and passed along by Timnah;
Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
11 and the border went out to the side of Ekron northward; and the border extended to Shikkeron, and passed along to Mount Baalah, and went out at Jabneel; and the goings out of the border were at the sea.
Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
12 The west border was to the shore of the great sea. This is the border of the children of Judah according to their families.
Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
13 He gave to Caleb the son of Jephunneh a portion among the children of Judah, according to the commandment of the LORD to Joshua, even Kiriath Arba, named after the father of Anak (also called Hebron).
Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
14 Caleb drove out the three sons of Anak: Sheshai, and Ahiman, and Talmai, the children of Anak.
Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
15 He went up against the inhabitants of Debir: now the name of Debir before was Kiriath Sepher.
Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
16 Caleb said, “He who strikes Kiriath Sepher, and takes it, to him I will give Achsah my daughter as wife.”
Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
17 Othniel the son of Kenaz, the brother of Caleb, took it: and he gave him Achsah his daughter as wife.
Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
18 When she came, she had him ask her father for a field. She got off her donkey, and Caleb said, “What do you want?”
Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
19 She said, “Give me a blessing. Because you have set me in the land of the South, give me also springs of water.” So he gave her the upper springs and the lower springs.
Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
20 This is the inheritance of the tribe of the children of Judah according to their families.
Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
21 The farthest cities of the tribe of the children of Judah toward the border of Edom in the South were Kabzeel, Eder, Jagur,
Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
22 Kinah, Dimonah, Adadah,
Kina, Dimona, Adada,
23 Kedesh, Hazor, Ithnan,
Kadeshi, Hazor, Ithinani,
24 Ziph, Telem, Bealoth,
Zifu, Telemu, Bealothi.
25 Hazor Hadattah, Kerioth Hezron (also called Hazor),
Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
26 Amam, Shema, Moladah,
Amamu, shema, Molada,
27 Hazar Gaddah, Heshmon, Beth Pelet,
Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
28 Hazar Shual, Beersheba, Biziothiah,
Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
29 Baalah, Iim, Ezem,
Baala, Limu, Ezemu,
30 Eltolad, Chesil, Hormah,
Eltoladi, Kesili, Horma,
31 Ziklag, Madmannah, Sansannah,
Ziklagi, Madimana, Sansana,
32 Lebaoth, Shilhim, Ain, and Rimmon. All the cities are twenty-nine, with their villages.
Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
33 In the lowland, Eshtaol, Zorah, Ashnah,
Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
34 Zanoah, En Gannim, Tappuah, Enam,
Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
35 Jarmuth, Adullam, Socoh, Azekah,
Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
36 Shaaraim, Adithaim and Gederah (or Gederothaim); fourteen cities with their villages.
Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
37 Zenan, Hadashah, Migdal Gad,
Zena, Hadasha, Migidagadi,
38 Dilean, Mizpah, Joktheel,
Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
39 Lachish, Bozkath, Eglon,
Lakishi, Bozikathi, Egloni.
40 Cabbon, Lahmam, Chitlish,
Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
41 Gederoth, Beth Dagon, Naamah, and Makkedah; sixteen cities with their villages.
Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
42 Libnah, Ether, Ashan,
Libna, Etheri, Ashani,
43 Iphtah, Ashnah, Nezib,
Ifuta, Ashina, Nezibu,
44 Keilah, Achzib, and Mareshah; nine cities with their villages.
Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
45 Ekron, with its towns and its villages;
Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
46 from Ekron even to the sea, all that were by the side of Ashdod, with their villages.
kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
47 Ashdod, its towns and its villages; Gaza, its towns and its villages; to the brook of Egypt, and the great sea with its coastline.
Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
48 In the hill country, Shamir, Jattir, Socoh,
Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
49 Dannah, Kiriath Sannah (which is Debir),
Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
50 Anab, Eshtemoh, Anim,
Anabu, Eshitemo, Animu,
51 Goshen, Holon, and Giloh; eleven cities with their villages.
Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
52 Arab, Dumah, Eshan,
Arabu, Duma, Ehani,
53 Janim, Beth Tappuah, Aphekah,
Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
54 Humtah, Kiriath Arba (also called Hebron), and Zior; nine cities with their villages.
Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
55 Maon, Carmel, Ziph, Jutah,
Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
56 Jezreel, Jokdeam, Zanoah,
Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
57 Kain, Gibeah, and Timnah; ten cities with their villages.
Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
58 Halhul, Beth Zur, Gedor,
Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
59 Maarath, Beth Anoth, and Eltekon; six cities with their villages.
Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
60 Kiriath Baal (also called Kiriath Jearim), and Rabbah; two cities with their villages.
Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
61 In the wilderness, Beth Arabah, Middin, Secacah,
Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
62 Nibshan, the City of Salt, and En Gedi; six cities with their villages.
Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
63 As for the Jebusites, the inhabitants of Jerusalem, the children of Judah could not drive them out; but the Jebusites live with the children of Judah at Jerusalem to this day.
Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.

< Joshua 15 >