< John 4 >

1 Therefore when the Lord knew that the Pharisees had heard that Jesus was making and baptizing more disciples than John
Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
2 (although Jesus himself did not baptize, but his disciples),
ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
3 he left Judea and departed into Galilee.
Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
4 He needed to pass through Samaria.
Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
5 So he came to a city of Samaria called Sychar, near the parcel of ground that Jacob gave to his son Joseph.
Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
6 Jacob’s well was there. Jesus therefore, being tired from his journey, sat down by the well. It was about the sixth hour.
Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 A woman of Samaria came to draw water. Jesus said to her, “Give me a drink.”
Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.”
8 For his disciples had gone away into the city to buy food.
(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 The Samaritan woman therefore said to him, “How is it that you, being a Jew, ask for a drink from me, a Samaritan woman?” (For Jews have no dealings with Samaritans.)
Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)
10 Jesus answered her, “If you knew the gift of God, and who it is who says to you, ‘Give me a drink,’ you would have asked him, and he would have given you living water.”
Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”
11 The woman said to him, “Sir, you have nothing to draw with, and the well is deep. So where do you get that living water?
Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi?
12 Are you greater than our father Jacob, who gave us the well and drank from it himself, as did his children and his livestock?”
Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”
13 Jesus answered her, “Everyone who drinks of this water will thirst again,
Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.
14 but whoever drinks of the water that I will give him by no means will thirst for the age (aiōn g165); but the water that I will give him will become in him a well of water springing up to consummate (aiōnios g166) life."
Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 The woman said to him, “Sir, give me this water, so that I do not get thirsty, neither come all the way here to draw.”
Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”
16 Jesus said to her, “Go, call your husband, and come here.”
Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
17 The woman answered, “I have no husband.” Jesus said to her, “You said well, ‘I have no husband,’
Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.
18 for you have had five husbands; and he whom you now have is not your husband. This you have said truly.”
Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”
19 The woman said to him, “Sir, I perceive that you are a prophet.
Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.
20 Our fathers worshiped in this mountain, and you Jews say that in Jerusalem is the place where people ought to worship.”
Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”
21 Jesus said to her, “Woman, believe me, the hour is coming when neither in this mountain nor in Jerusalem will you worship the Father.
Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.
22 You worship that which you do not know. We worship that which we know; for salvation is from the Jews.
Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23 But the hour comes, and now is, when the true worshipers will worship the Father in spirit and truth, for the Father seeks such to be his worshipers.
Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
24 God is spirit, and those who worship him must worship in spirit and truth.”
Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
25 The woman said to him, “I know that Messiah is coming, he who is called Christ. When he has come, he will declare to us all things.”
Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”
26 Jesus said to her, “I am he, the one who speaks to you.”
Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”
27 Just then, his disciples came. They marveled that he was speaking with a woman; yet no one said, “What are you looking for?” or, “Why do you speak with her?”
Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”
28 So the woman left her water pot, went away into the city, and said to the people,
Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,
29 “Come, see a man who told me everything that I have done. Can this be the Christ?”
“Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”
30 They went out of the city, and were coming to him.
Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.
31 In the meanwhile, the disciples urged him, saying, “Rabbi, eat.”
Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”
32 But he said to them, “I have food to eat that you do not know about.”
Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”
33 The disciples therefore said to one another, “Has anyone brought him something to eat?”
Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”
34 Jesus said to them, “My food is to do the will of him who sent me and to accomplish his work.
Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.
35 Do not you say, ‘There are yet four months until the harvest’? Behold, I tell you, lift up your eyes and look at the fields, that they are white for harvest already.
Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!
36 He who reaps receives wages and gathers fruit to consummate (aiōnios g166) life; that both he who sows and he who reaps may rejoice together.
Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
37 For in this the saying is true, ‘One sows, and another reaps.’
Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
38 I sent you to reap that for which you have not labored. Others have labored, and you have entered into their labor.”
Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
39 From that city many of the Samaritans believed in him because of the word of the woman, who testified, “He told me everything that I have done.”
Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
40 So when the Samaritans came to him, they begged him to stay with them. He stayed there two days.
Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
41 Many more believed because of his word.
Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
42 They said to the woman, “Now we believe, not because of your speaking; for we have heard for ourselves, and know that this is indeed the Christ, the Savior of the world.”
Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
43 After the two days he went out from there and went into Galilee.
Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
44 For Jesus himself testified that a prophet has no honor in his own country.
(Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
45 So when he came into Galilee, the Galileans received him, having seen all the things that he did in Jerusalem at the feast, for they also went to the feast.
Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.
46 Jesus came therefore again to Cana of Galilee, where he made the water into wine. There was a certain nobleman whose son was sick at Capernaum.
Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
47 When he heard that Jesus had come out of Judea into Galilee, he went to him and begged him that he would come down and heal his son, for he was at the point of death.
Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
48 Jesus therefore said to him, “Unless you see signs and wonders, you will in no way believe.”
Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
49 The nobleman said to him, “Sir, come down before my child dies.”
Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
50 Jesus said to him, “Go your way. Your son lives.” The man believed the word that Jesus spoke to him, and he went his way.
Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.” Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
51 As he was going down, his servants met him and reported, saying “Your child lives!”
Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
52 So he inquired of them the hour when he began to get better. They said therefore to him, “Yesterday at the seventh hour, the fever left him.”
Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
53 So the father knew that it was at that hour in which Jesus said to him, “Your son lives.” He believed, as did his whole house.
Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
54 This is again the second sign that Jesus did, having come out of Judea into Galilee.
Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.

< John 4 >