< Job 6 >

1 Then Job answered,
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 “Oh that my anguish were weighed, and all my calamity laid in the balances!
“Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
3 For now it would be heavier than the sand of the seas, therefore my words have been rash.
Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For the arrows of the Almighty are within me. My spirit drinks up their poison. The terrors of God set themselves in array against me.
Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
5 Does the wild donkey bray when he has grass? Or does the ox low over his fodder?
Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
6 Can that which has no flavor be eaten without salt? Or is there any taste in the white of an egg?
Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
7 My soul refuses to touch them. They are as loathsome food to me.
Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
8 “Oh that I might have my request, that God would grant the thing that I long for,
Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
9 even that it would please God to crush me; that he would let loose his hand, and cut me off!
kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
10 Let it still be my consolation, yes, let me exult in pain that does not spare, that I have not denied the words of the Holy One.
Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
11 What is my strength, that I should wait? What is my end, that I should be patient?
Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
12 Is my strength the strength of stones? Or is my flesh of bronze?
Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
13 Is not it that I have no help in me, that wisdom is driven away from me?
Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
14 “To him who is ready to faint, kindness should be shown from his friend; even to him who forsakes the fear of the Almighty.
Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
15 My brothers have dealt deceitfully as a brook, as the channel of brooks that pass away;
Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
16 which are black by reason of the ice, in which the snow hides itself.
ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
17 In the dry season, they vanish. When it is hot, they are consumed out of their place.
Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
18 The caravans that travel beside them turn away. They go up into the waste, and perish.
Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
19 The caravans of Tema looked. The companies of Sheba waited for them.
Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
20 They were distressed because they were confident. They came there, and were confounded.
Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
21 For now you are nothing. You see a terror, and are afraid.
Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
22 Did I ever say, ‘Give to me’? or, ‘Offer a present for me from your substance’?
Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
23 or, ‘Deliver me from the adversary’s hand’? or, ‘Redeem me from the hand of the oppressors’?
Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
24 “Teach me, and I will hold my peace. Cause me to understand my error.
Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
25 How forcible are words of uprightness! But your reproof, what does it reprove?
Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
26 Do you intend to reprove words, since the speeches of one who is desperate are as wind?
Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
27 Yes, you would even cast lots for the fatherless, and make merchandise of your friend.
Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
28 Now therefore be pleased to look at me, for surely I will not lie to your face.
Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
29 Please return. Let there be no injustice. Yes, return again. My cause is righteous.
Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
30 Is there injustice on my tongue? Cannot my taste discern mischievous things?
Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?

< Job 6 >