< Job 5 >

1 “Call now; is there any who will answer you? To which of the holy ones will you turn?
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 For resentment kills the foolish man, and jealousy kills the simple.
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 I have seen the foolish taking root, but suddenly I cursed his habitation.
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 His children are far from safety. They are crushed in the gate. Neither is there any to deliver them,
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 whose harvest the hungry eat up, and take it even out of the thorns. The snare gapes for their substance.
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 For affliction does not come out of the dust, neither does trouble spring out of the ground;
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 but man is born to trouble, as the sparks fly upward.
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 “But as for me, I would seek God. I would commit my cause to God,
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 who does great things that cannot be fathomed, marvelous things without number;
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 who gives rain on the earth, and sends waters on the fields;
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 so that he sets up on high those who are low, those who mourn are exalted to safety.
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 He frustrates the plans of the crafty, so that their hands cannot perform their enterprise.
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 He takes the wise in their own craftiness; the counsel of the cunning is carried headlong.
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 They meet with darkness in the day time, and grope at noonday as in the night.
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 But he saves from the sword of their mouth, even the needy from the hand of the mighty.
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 So the poor has hope, and injustice shuts her mouth.
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 “Behold, happy is the man whom God corrects. Therefore do not despise the chastening of the Almighty.
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 For he wounds and binds up. He injures and his hands make whole.
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 He will deliver you in six troubles; yes, in seven no evil will touch you.
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 In famine he will redeem you from death; in war, from the power of the sword.
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 You will be hidden from the scourge of the tongue, neither will you be afraid of destruction when it comes.
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 You will laugh at destruction and famine, neither will you be afraid of the animals of the earth.
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 For you will be allied with the stones of the field. The animals of the field will be at peace with you.
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 You will know that your tent is in peace. You will visit your fold, and will miss nothing.
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 You will know also that your offspring will be great, your offspring as the grass of the earth.
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 You will come to your grave in a full age, like a shock of grain comes in its season.
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 Behold, we have researched it. It is so. Hear it, and know it for your good.”
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< Job 5 >