< Job 31 >

1 “I made a covenant with my eyes; how then should I look lustfully at a young woman?
Nimefanya patano na macho yangu; ni kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?
2 For what is the portion from God above, and the heritage from the Almighty on high?
Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?
3 Is it not calamity to the unrighteous, and disaster to the workers of iniquity?
Nilikuwa nafikiri kwamba majanga ni kwa watu wasio na haki, na misiba ni kwa ajili ya watu watendao mabaya.
4 Does not he see my ways, and count all my steps?
Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?
5 “If I have walked with falsehood, and my foot has hurried to deceit
Kama nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo,
6 (let me be weighed in an even balance, that God may know my integrity);
na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa ili kwamba Mungu aujue uadilifu wangu.
7 if my step has turned out of the way, if my heart walked after my eyes, if any defilement has stuck to my hands,
Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi, kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu, na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu,
8 then let me sow, and let another eat. Yes, let the produce of my field be rooted out.
na kisha mimi nipande na mtu mwingine na ale; mavuno na yang'olewe katika shamba langu.
9 “If my heart has been enticed to a woman, and I have laid wait at my neighbor’s door,
Na kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine, ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake,
10 then let my wife grind for another, and let others sleep with her.
na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine, na wanaume wengine na walale naye.
11 For that would be a heinous crime. Yes, it would be an iniquity to be punished by the judges,
Na kwa hilo litakuwa ni kosa kubwa; kwa kweli, utakuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi.
12 for it is a fire that consumes to destruction, and would root out all my increase.
Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote.
13 “If I have despised the cause of my male servant or of my female servant, when they contended with me,
Ikiwa nilikataa ombi la haki kutoka kwa watumishi wangu wa kiume na wa kike wakati walipohojiana nami,
14 what then will I do when God rises up? When he visits, what will I answer him?
kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?
15 Did not he who made me in the womb make him? Did not one fashion us in the womb?
Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?
16 “If I have withheld the poor from their desire, or have caused the eyes of the widow to fail,
kama nimewanyima watu masikini matakwa yao, au kama nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,
17 or have eaten my morsel alone, and the fatherless has not eaten of it
au ikiwa kama nimekula kipande changu na sijawaruhusu wale wasio na baba kukila pia -
18 (no, from my youth he grew up with me as with a father, I have guided her from my mother’s womb);
kwasababu tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.
19 if I have seen any perish for want of clothing, or that the needy had no covering;
ikiwa nimemwona yeyote akiangamia kwa kwa kukosa mavazi, au kama nimemwona mtu mhitaji akiwa hana nguo;
20 if his heart has not blessed me, if he has not been warmed with my sheep’s fleece;
ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,
21 if I have lifted up my hand against the fatherless, because I saw my help in the gate;
ikiwa nimeinua juu mkono wangu kinyume na watu wasio na baba kwa kuwa niliona msaada wangu katika lango la mji, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu.
22 then let my shoulder fall from the shoulder blade, and my arm be broken from the bone.
Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake.
23 For calamity from God is a terror to me. Because of his majesty, I can do nothing.
Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu; kwasababu ya mawazo ya ukuu wake, nisingeweza kufanya mambo hayo.
24 “If I have made gold my hope, and have said to the fine gold, ‘You are my confidence;’
Kama ningeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, na kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';
25 If I have rejoiced because my wealth was great, and because my hand had gotten much;
na kama nimefurahi kwasababu ya utajiri wangu ulikuwa mkubwa, kwa kuwa mkono wangu umepata mali nyingi, na kisha kuleta mashitaka dhidi yangu!
26 if I have seen the sun when it shined, or the moon moving in splendor,
Ikiwa nimeliona jua lilipowaka, au mwezi ukitembea katika mng'ao wake,
27 and my heart has been secretly enticed, and my hand threw a kiss from my mouth;
na kama moyo wangu umevutwa kwa siri, ili kwamba mdomo wangu umeubusu mkono wangu katika ibada yao -
28 this also would be an iniquity to be punished by the judges, for I would have denied the God who is above.
hili nalo pia lingekuwa ni ubaya wa kuadhibiwa na waamuzi, kwa kuwa ningekuwa nimemkana Mungu aliyejuu.
29 “If I have rejoiced at the destruction of him who hated me, or lifted up myself when evil found him
Ikiwa nimefurahia uharibifu wa yeyote ambaye ananichukia mimi, au kuwapa hongera wakati majanga yanapowapata, ndipo ulete mashitaka dhidi yangu!
30 (I have certainly not allowed my mouth to sin by asking his life with a curse);
Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.
31 if the men of my tent have not said, ‘Who can find one who has not been filled with his meat?’
Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?
32 (the foreigner has not camped in the street, but I have opened my doors to the traveler);
(hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri), na kama haiko hivyo, ndipo mlete mashitaka kinyume nami!
33 if like Adam I have covered my transgressions, by hiding my iniquity in my heart,
Ikiwa, kama binadamu nimezificha dhambi zangu kwa kuficha hatia ndani ya kanzu yangu -
34 because I feared the great multitude, and the contempt of families terrified me, so that I kept silence, and did not go out of the door—
kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha, hivyo basi nilinyamaza kimya na sikuweza kwenda nje, basi nileteni mashitaka dhidi yangu!
35 oh that I had one to hear me! Behold, here is my signature! Let the Almighty answer me! Let the accuser write my indictment!
Ee, kama nilikuwa na mtu wa kunisikiliza! Ona, hii ni saini yangu; na Mwenye nguvu na anijibu! Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!
36 Surely I would carry it on my shoulder, and I would bind it to me as a crown.
Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji.
37 I would declare to him the number of my steps. I would go near to him like a prince.
Ningemweleza hesabu ya hatua zangu; na kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini ningepanda kwenda kwake.
38 If my land cries out against me, and its furrows weep together;
Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja,
39 if I have eaten its fruits without money, or have caused its owners to lose their life,
ikiwa nimekula mavuno yake bila kulipia au kama nimesababisha wamiliki wake kupoteza maisha yao,
40 let briers grow instead of wheat, and stinkweed instead of barley.” The words of Job are ended.
ndipo miiba na iote badala ya ngano na magugu badala ya shayiri.” Maneno ya Ayubu yamemalizika.

< Job 31 >