< Job 30 >

1 “But now those who are younger than I have me in derision, whose fathers I considered unworthy to put with my sheep dogs.
Sasa vijana wananidhihaki - vijana ambao baba zao wasingeweza hata kuwahudumia mbwa wa kundi langu.
2 Of what use is the strength of their hands to me, men in whom ripe age has perished?
Kwa kweli, nguvu za mikono ya baba zao, zingenisaidia nini - watu ambao hawakuwa na nguvu wakati wa kukua kwao?
3 They are gaunt from lack and famine. They gnaw the dry ground, in the gloom of waste and desolation.
Walidhoofishwa na umasikini na njaa; walisaga nchi kavu mafichoni.
4 They pluck salt herbs by the bushes. The roots of the broom tree are their food.
Walichuma mche chumvi na majani ya vichaka; mizizi ya mti wa ufagio ilikuwa ndiyo chakula chao.
5 They are driven out from among men. They cry after them as after a thief,
Waliondolewa miongoni mwa watu waliopiga kelele nyuma yao kama ambavyo mtu angempigia kelele mwizi.
6 so that they live in frightful valleys, and in holes of the earth and of the rocks.
Hivyo walipaswa kuishi katika mabonde ya mto, katika mashimo ya ardhi na miamba.
7 They bray among the bushes. They are gathered together under the nettles.
Walilia kwa uchungu porini kama punda; chini ya vichaka walikutana.
8 They are children of fools, yes, children of wicked men. They were flogged out of the land.
Walikuwa uzao wa wapumbavu, hakika, wa watu wasiofaa; waliondolewa duniani kama waarifu.
9 “Now I have become their song. Yes, I am a byword to them.
Lakini sasa, nimekua sababu ya wimbo wa dhihaka kwa wana wao; hakika, nimekuwa mzaa kwao.
10 They abhor me, they stand aloof from me, and do not hesitate to spit in my face.
Wananichukia na kusimama mbali nami; hawaachi kunitemea usoni.
11 For he has untied his cord, and afflicted me; and they have thrown off restraint before me.
Kwa maana Mungu ameondoa kamba katika upinde wangu na amenipiga, na hivyo watu hawa wanashindwa kujizuia mbele yangu.
12 On my right hand rise the rabble. They thrust aside my feet. They cast their ways of destruction up against me.
Kundi la vijana wabaya wanashambulia nguvu zangu; wananiondolea mbali na kukusanya kinyume changu rundo la kuhusuru.
13 They mar my path. They promote my destruction without anyone’s help.
Wanaharibu maisha yangu; wanapeleka mbele maangamizi yangu, watu wasio na wakuwazuia.
14 As through a wide breach they come. They roll themselves in amid the ruin.
Wanakuja kinyume changu kama jeshi katika tundu pana katika ukuta wa mji; katikati ya maangamizi wanajizungusha juu yangu.
15 Terrors have turned on me. They chase my honor as the wind. My welfare has passed away as a cloud.
Hofu zimeniandama; heshima yangu imeondolewa mbali nami kama kwa upepo; mafanikio yangu yameondolewa kama wingu.
16 “Now my soul is poured out within me. Days of affliction have taken hold of me.
Sasa uhai wangu umeondolewa ndani yangu; siku nyingi za maumivu zimenipita.
17 In the night season my bones are pierced in me, and the pains that gnaw me take no rest.
Mifupa inauma ndani yangu wakati wa usiku; maumivu yanayonisaga hayaishi.
18 My garment is disfigured by great force. It binds me about as the collar of my tunic.
Nguvu kuu ya Mungu imeshika mavazi yangu; yananizunguka kama kala ya vazi langu.
19 He has cast me into the mire. I have become like dust and ashes.
Amenitupa matopeni; nimekuwa kama vumbi na majivu.
20 I cry to you, and you do not answer me. I stand up, and you gaze at me.
Nakulilia wewe, Mungu, lakini haunijibu; ninasimama, nawe unaniangalia tu.
21 You have turned to be cruel to me. With the might of your hand you persecute me.
Umegeuka na kuwa mkali kwangu; kwa nguvu za mkono wako umenitesa.
22 You lift me up to the wind, and drive me with it. You dissolve me in the storm.
Unaniinua katika upepo na kuufanya unikokote; unanirusha huku na kule katika dhoruba.
23 For I know that you will bring me to death, to the house appointed for all living.
Kwa maana najua ya kwamba utanipeleka mautini, nyumba ya hatima kwa viumbe vyote.
24 “However does not one stretch out a hand in his fall? Or in his calamity therefore cry for help?
Lakini, je hakuna ainuaye mkono wake kuomba msaada aangukapo? Je hakuna aombaye msaada akiwa tabuni?
25 Did not I weep for him who was in trouble? Was not my soul grieved for the needy?
Je sikulia kwa ajili yake aliyekuwa tabuni? Je sijahuzunika kwa ajili ya mwitaji?
26 When I looked for good, then evil came. When I waited for light, darkness came.
Nilipotazamia mema, ndipo yalipokuja mabaya; niliposubiri nuru, giza lilikuja badala yake.
27 My heart is troubled, and does not rest. Days of affliction have come on me.
Moyo wangu umetaabika na hautulii; siku za mateso zimenipata.
28 I go mourning without the sun. I stand up in the assembly, and cry for help.
Nimekuwa na ngozi nyeusi lakini si kwa sababu ya jua; nasimama katika kusanyiko na kulilia msaada.
29 I am a brother to jackals, and a companion to ostriches.
Nimekuwa ndugu kwa mbwea, mshirika wa mbuni.
30 My skin grows black and peels from me. My bones are burned with heat.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi na inapukutika; mifupa yangu imeunguzwa na joto.
31 Therefore my harp has turned to mourning, and my pipe into the voice of those who weep.
Kwa hiyo kinubi changu kimefunguliwa kwa nyimbo za maombolezo, zomari yangu kwa kuimba kwao waombolezao.

< Job 30 >