< Job 26 >

1 Then Job answered,
Kisha Ayubu akajibu:
2 “How have you helped him who is without power! How have you saved the arm that has no strength!
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 How have you counseled him who has no wisdom, and plentifully declared sound knowledge!
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 To whom have you uttered words? Whose spirit came out of you?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 “The departed spirits tremble, those beneath the waters and all that live in them.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 Sheol (Sheol h7585) is naked before God, and Abaddon has no covering.
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 He stretches out the north over empty space, and hangs the earth on nothing.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 He binds up the waters in his thick clouds, and the cloud is not burst under them.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 He encloses the face of his throne, and spreads his cloud on it.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 He has described a boundary on the surface of the waters, and to the confines of light and darkness.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 The pillars of heaven tremble and are astonished at his rebuke.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 He stirs up the sea with his power, and by his understanding he strikes through Rahab.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 By his Spirit the heavens are garnished. His hand has pierced the swift serpent.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 Behold, these are but the outskirts of his ways. How small a whisper do we hear of him! But the thunder of his power who can understand?”
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Job 26 >