< Job 19 >

1 Then Job answered,
Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
2 “How long will you torment me, and crush me with words?
lini mtanifanya mimi kuteseka na kunivunja vunja mimi vipande vipnde kwa maneno?
3 You have reproached me ten times. You are not ashamed that you attack me.
Mara kumi hivi mmenishutumu mimi; ninyi hamuoni aibu kwamba mmenitendea mimi kwa ukatili.
4 If it is true that I have erred, my error remains with myself.
Kama ni dhahiri kweli mimi nimekosa, makosa yangu hubaki kuwa wajibu wangu.
5 If indeed you will magnify yourselves against me, and plead against me my reproach,
Kama ni dhahiri ninyi mtajiinua juu yangu mimi na kuutumia uvumilivu wangu kunipinga mimi,
6 know now that God has subverted me, and has surrounded me with his net.
kisha ninyi mnapaswa kutambua kwamba Mungu amefanya mabaya kwangu mimi na amenikamata mimi katika mtego wake yeye.
7 “Behold, I cry out of wrong, but I am not heard. I cry for help, but there is no justice.
Tazama, Mimi ninalia kwa sauti, “dhuluma!” lakini sipati jibu. Mimi ninaita kwa ajili ya msaada, lakini hakuna haki.
8 He has walled up my way so that I cannot pass, and has set darkness in my paths.
Yeye ameiwekea ukuta njia yangu, ili kwamba mimi nisiweze kupita, na yeye ameweka giza katika njia yangu.
9 He has stripped me of my glory, and taken the crown from my head.
Yeye ameniondoa Mimi kutoka katika utukufu wangu, na ameichukua taji kutoka kwenye kichwa changu mimi.
10 He has broken me down on every side, and I am gone. He has plucked my hope up like a tree.
Yeye amenivunjavunja mimi chini kwa kila upande, na Mimi nimetoweka; yeye amelikokota juu tumaini langu kama mti.
11 He has also kindled his wrath against me. He counts me among his adversaries.
Yeye pia ameiongeza ghadhabu yake dhidi yangu mimi; yeye ananihesabu mimi kama mmoja wa adui zake.
12 His troops come on together, build a siege ramp against me, and encamp around my tent.
Majeshi yake huja juu pamoja; wao wananikosesha tumaini kwa kuniteka nyara kwa kundi kubwa kupigana na mimi wakizunguka hema yangu.
13 “He has put my brothers far from me. My acquaintances are wholly estranged from me.
Yeye amewaweka ndugu zangu mbali kutoka kwangu mimi; watu wangu wa karibu wote wamejitenga kutoka kwangu mimi.
14 My relatives have gone away. My familiar friends have forgotten me.
Vizazi vyangu vimeniangusha mimi; rafiki zangu wa karibu wamenisahamu mimi.
15 Those who dwell in my house and my maids consider me a stranger. I am an alien in their sight.
Wale ambao mwanzoni walikaa kama wageni ndani ya nyumba yangu na watumishi wangu wa kike, hunihesabu mimi kama mgeni. Mimi nimekuwa mgeni katika macho yao.
16 I call to my servant, and he gives me no answer. I beg him with my mouth.
Mimi ninamwita mtumishi wangu, lakini yeye hanipi jibu japokuwa Mimi nimemsihi yeye kwa midomo yangu.
17 My breath is offensive to my wife. I am loathsome to the children of my own mother.
Pumzi yangu mimi ni chukizo kwa mke wangu; Hata mimi ninachukiwa na wale ambao walizaliwa kutoka katika tumbo la mama yangu mimi.
18 Even young children despise me. If I arise, they speak against me.
Hata watoto wachanga wananichukia mimi; ikiwa Mimi nitainuka kuzungumza, wao huzungumza dhidi yangu mimi.
19 All my familiar friends abhor me. They whom I loved have turned against me.
Rafiki zangu wote ninaowazoea wananichukia sana mimi; wale ambao Mimi ninawapenda wamegeuka kinyume na mimi.
20 My bones stick to my skin and to my flesh. I have escaped by the skin of my teeth.
Mifupa yangu inashikamana kwenye ngozi yangu na kwenye mwili wangu; Mimi ninaishi tu kwa ngozi ya meno yangu.
21 “Have pity on me. Have pity on me, you my friends, for the hand of God has touched me.
Iweni na huruma juu yangu mimi, muwe na huruma juu yangu mimi, rafiki zangu, kwa maana mkono wa Mungu umenigusa mimi.
22 Why do you persecute me as God, and are not satisfied with my flesh?
Kwa nini mnanitesa mimi kama ninyi mlikuwa Mungu? kwa nini hamjatosheka bado kwa kula mwili wangu?
23 “Oh that my words were now written! Oh that they were inscribed in a book!
Laiti, hayo maneno yangu yangekuwa yameandikwa chini! Laiti, hayo yangekuwa yameandikwa katika kitabu!
24 That with an iron pen and lead they were engraved in the rock forever!
Laiti, kwa kalamu ya chuma na risasi hayo yangekuwa yamechorwa katika mwamba siku zote!
25 But as for me, I know that my Redeemer lives. In the end, he will stand upon the earth.
Lakini kama ilivyo kwangu mimi, Mimi ninafahamu kwamba mkombozi wangu anaishi, na kwamba hata mwisho atasimama katika nchi;
26 After my skin is destroyed, then I will see God in my flesh,
baada ya ngozi yangu, hivyo ndivyo, mwili huu, unaharibiwa, ndipo katika mwili wangu mimi Nitamwona Mungu.
27 whom I, even I, will see on my side. My eyes will see, and not as a stranger. “My heart is consumed within me.
Mimi nitamwona yeye kwa macho yangu mwenyewe-Mimi, na siyo mtu mwingine. Moyo wangu hushindwa ndani yangu mimi.
28 If you say, ‘How we will persecute him!’ because the root of the matter is found in me,
Kama mnatasema, 'Kwa jinsi gani tutamtesa yeye? Mzizi wa mahangaiko yake unakaa katika yeye;
29 be afraid of the sword, for wrath brings the punishments of the sword, that you may know there is a judgment.”
ndipo uwe umeogopeshwa kwa ule upanga, kwa sababu ghadhabu huleta hukumu ya upanga, hivyo kwamba wewe uweze kutambua kuna hukumu.”

< Job 19 >