< Job 11 >

1 Then Zophar, the Naamathite, answered,
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 “Should not the multitude of words be answered? Should a man full of talk be justified?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Should your boastings make men hold their peace? When you mock, will no man make you ashamed?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 For you say, ‘My doctrine is pure. I am clean in your eyes.’
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 But oh that God would speak, and open his lips against you,
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 that he would show you the secrets of wisdom! For true wisdom has two sides. Know therefore that God exacts of you less than your iniquity deserves.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 “Can you fathom the mystery of God? Or can you probe the limits of the Almighty?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 They are high as heaven. What can you do? They are deeper than Sheol (Sheol h7585). What can you know?
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol h7585)
9 Its measure is longer than the earth, and broader than the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If he passes by, or confines, or convenes a court, then who can oppose him?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For he knows false men. He sees iniquity also, even though he does not consider it.
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 An empty-headed man becomes wise when a man is born as a wild donkey’s colt.
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 “If you set your heart aright, stretch out your hands toward him.
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 If iniquity is in your hand, put it far away. Do not let unrighteousness dwell in your tents.
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 Surely then you will lift up your face without spot. Yes, you will be steadfast, and will not fear,
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 for you will forget your misery. You will remember it like waters that have passed away.
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 Life will be clearer than the noonday. Though there is darkness, it will be as the morning.
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 You will be secure, because there is hope. Yes, you will search, and will take your rest in safety.
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 Also you will lie down, and no one will make you afraid. Yes, many will court your favor.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 But the eyes of the wicked will fail. They will have no way to flee. Their hope will be the giving up of the spirit.”
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

< Job 11 >