< Job 10 >

1 “My soul is weary of my life. I will give free course to my complaint. I will speak in the bitterness of my soul.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 I will tell God, ‘Do not condemn me. Show me why you contend with me.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 Is it good to you that you should oppress, that you should despise the work of your hands, and smile on the counsel of the wicked?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 Do you have eyes of flesh? Or do you see as man sees?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 Are your days as the days of mortals, or your years as man’s years,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 that you inquire after my iniquity, and search after my sin?
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 Although you know that I am not wicked, there is no one who can deliver out of your hand.
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 “‘Your hands have framed me and fashioned me altogether, yet you destroy me.
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Remember, I beg you, that you have fashioned me as clay. Will you bring me into dust again?
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 Have not you poured me out like milk, and curdled me like cheese?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 You have clothed me with skin and flesh, and knit me together with bones and sinews.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 You have granted me life and loving kindness. Your visitation has preserved my spirit.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 Yet you hid these things in your heart. I know that this is with you:
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 if I sin, then you mark me. You will not acquit me from my iniquity.
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 If I am wicked, woe to me. If I am righteous, I still will not lift up my head, being filled with disgrace, and conscious of my affliction.
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 If my head is held high, you hunt me like a lion. Again you show yourself powerful to me.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 You renew your witnesses against me, and increase your indignation on me. Changes and warfare are with me.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 “‘Why, then, have you brought me out of the womb? I wish I had given up the spirit, and no eye had seen me.
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 I should have been as though I had not been. I should have been carried from the womb to the grave.
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 Are not my days few? Stop! Leave me alone, that I may find a little comfort,
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 before I go where I will not return from, to the land of darkness and of the shadow of death;
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 the land dark as midnight, of the shadow of death, without any order, where the light is as midnight.’”
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”

< Job 10 >