< Genesis 5 >

1 This is the book of the generations of Adam. In the day that God created man, he made him in God’s likeness.
Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
2 He created them male and female, and blessed them. On the day they were created, he named them Adam.
Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
3 Adam lived one hundred thirty years, and became the father of a son in his own likeness, after his image, and named him Seth.
Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
4 The days of Adam after he became the father of Seth were eight hundred years, and he became the father of other sons and daughters.
Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
5 All the days that Adam lived were nine hundred thirty years, then he died.
Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
6 Seth lived one hundred five years, then became the father of Enosh.
Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
7 Seth lived after he became the father of Enosh eight hundred seven years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
8 All of the days of Seth were nine hundred twelve years, then he died.
Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
9 Enosh lived ninety years, and became the father of Kenan.
Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
10 Enosh lived after he became the father of Kenan eight hundred fifteen years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
11 All of the days of Enosh were nine hundred five years, then he died.
Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
12 Kenan lived seventy years, then became the father of Mahalalel.
Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
13 Kenan lived after he became the father of Mahalalel eight hundred forty years, and became the father of other sons and daughters
Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
14 and all of the days of Kenan were nine hundred ten years, then he died.
Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
15 Mahalalel lived sixty-five years, then became the father of Jared.
Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
16 Mahalalel lived after he became the father of Jared eight hundred thirty years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
17 All of the days of Mahalalel were eight hundred ninety-five years, then he died.
Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
18 Jared lived one hundred sixty-two years, then became the father of Enoch.
Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
19 Jared lived after he became the father of Enoch eight hundred years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
20 All of the days of Jared were nine hundred sixty-two years, then he died.
Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
21 Enoch lived sixty-five years, then became the father of Methuselah.
Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
22 After Methuselah’s birth, Enoch walked with God for three hundred years, and became the father of more sons and daughters.
Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
23 All the days of Enoch were three hundred sixty-five years.
Henoko aliishi miaka 365.
24 Enoch walked with God, and he was not found, for God took him.
Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
25 Methuselah lived one hundred eighty-seven years, then became the father of Lamech.
Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
26 Methuselah lived after he became the father of Lamech seven hundred eighty-two years, and became the father of other sons and daughters.
Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
27 All the days of Methuselah were nine hundred sixty-nine years, then he died.
Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
28 Lamech lived one hundred eighty-two years, then became the father of a son.
Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
29 He named him Noah, saying, “This one will comfort us in our work and in the toil of our hands, caused by the ground which the LORD has cursed.”
Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
30 Lamech lived after he became the father of Noah five hundred ninety-five years, and became the father of other sons and daughters.
Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
31 All the days of Lamech were seven hundred seventy-seven years, then he died.
Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
32 Noah was five hundred years old, then Noah became the father of Shem, Ham, and Japheth.
Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.

< Genesis 5 >