< 1 Chronicles 27 >

1 Now the children of Israel after their number, the heads of fathers’ households and the captains of thousands and of hundreds, and their officers who served the king in any matter of the divisions which came in and went out month by month throughout all the months of the year—of every division were twenty-four thousand.
Hii ndiyo orodha ya Waisraeli: viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu, majemadari wa mamia na maafisa wao, waliomtumikia mfalme kwa lolote lililohusu vikosi vya jeshi vilivyokuwa zamu mwezi baada ya mwezi katika mwaka mzima. Kila kikosi kimoja kilikuwa na watu 24,000.
2 Over the first division for the first month was Jashobeam the son of Zabdiel. In his division were twenty-four thousand.
Msimamizi wa kikosi cha kwanza kwa mwezi wa kwanza alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Kulikuwa na watu 24,000 katika kikosi chake.
3 He was of the children of Perez, the chief of all the captains of the army for the first month.
Yeye alikuwa mzao wa Peresi, na mkuu wa maafisa wote wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
4 Over the division of the second month was Dodai the Ahohite and his division, and Mikloth the ruler; and in his division were twenty-four thousand.
Msimamizi wa kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai Mwahohi. Miklothi ndiye alikuwa kiongozi wa kikosi chake. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
5 The third captain of the army for the third month was Benaiah, the son of Jehoiada the chief priest. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa kikosi cha tatu kwa mwezi wa tatu alikuwa Benaya mwana wa kuhani Yehoyada. Ndiye alikuwa mkuu wa kikosi chake kilichokuwa na watu 24,000.
6 This is that Benaiah who was the mighty man of the thirty and over the thirty. Of his division was Ammizabad his son.
Huyu ndiye yule Benaya aliyekuwa shujaa miongoni mwa wale Thelathini na ndiye alikuwa juu yao hao Thelathini. Mwanawe Amizabadi ndiye alikuwa mkuu katika kikosi chake.
7 The fourth captain for the fourth month was Asahel the brother of Joab, and Zebadiah his son after him. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa nne kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli nduguye Yoabu, mwanawe Zebadia ndiye aliingia mahali pake kwenye uongozi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
8 The fifth captain for the fifth month was Shamhuth the Izrahite. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa kikosi cha tano kwa mwezi wa tano alikuwa Shamhuthi Mwizrahi. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
9 The sixth captain for the sixth month was Ira the son of Ikkesh the Tekoite. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa kikosi cha sita kwa mwezi wa sita alikuwa Ira, mwana wa Ikeshi Mtekoa. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
10 The seventh captain for the seventh month was Helez the Pelonite, of the children of Ephraim. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa kikosi cha saba kwa mwezi wa saba alikuwa Helesi Mpeloni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
11 The eighth captain for the eighth month was Sibbecai the Hushathite, of the Zerahites. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa nane kwa mwezi wa nane, alikuwa Sibekai Mhushathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
12 The ninth captain for the ninth month was Abiezer the Anathothite, of the Benjamites. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa tisa kwa mwezi wa tisa alikuwa Abiezeri Mwanathothi wa Wabenyamini. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
13 The tenth captain for the tenth month was Maharai the Netophathite, of the Zerahites. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa kumi kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai Mnetofathi wa Wazera. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
14 The eleventh captain for the eleventh month was Benaiah the Pirathonite, of the children of Ephraim. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa kumi na moja kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaya Mpirathoni wa Waefraimu. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
15 The twelfth captain for the twelfth month was Heldai the Netophathite, of Othniel. In his division were twenty-four thousand.
Jemadari wa kumi na mbili kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Heldai Mnetofathi kutoka jamaa ya Othnieli. Kikosi chake kilikuwa na watu 24,000.
16 Furthermore over the tribes of Israel: of the Reubenites, Eliezer the son of Zichri was the ruler; of the Simeonites, Shephatiah the son of Maacah;
Maafisa waliokuwa wanaoongoza makabila ya Israeli walikuwa: Kwa Wareubeni: Eliezeri mwana wa Zikri; kwa Wasimeoni: Shefatia mwana wa Maaka;
17 of Levi, Hashabiah the son of Kemuel; of Aaron, Zadok;
kwa Walawi: Hashabia mwana wa Kemueli; kwa Aroni: Sadoki;
18 of Judah, Elihu, one of the brothers of David; of Issachar, Omri the son of Michael;
kwa Yuda: Elihu, nduguye Daudi; kwa Waisakari: Omri mwana wa Mikaeli;
19 of Zebulun, Ishmaiah the son of Obadiah; of Naphtali, Jeremoth the son of Azriel;
kwa Wazabuloni: Ishmaya mwana wa Obadia; kwa Wanaftali: Yeremothi mwana wa Azrieli;
20 of the children of Ephraim, Hoshea the son of Azaziah; of the half-tribe of Manasseh, Joel the son of Pedaiah;
kwa Waefraimu: Hoshea mwana wa Azazia; kwa nusu ya kabila la Manase: Yoeli mwana wa Pedaya;
21 of the half-tribe of Manasseh in Gilead, Iddo the son of Zechariah; of Benjamin, Jaasiel the son of Abner;
kwa nusu nyingine ya kabila la Manase huko Gileadi: Ido mwana wa Zekaria; kwa Wabenyamini: Yaasieli mwana wa Abneri;
22 of Dan, Azarel the son of Jeroham. These were the captains of the tribes of Israel.
kwa Wadani: Azareli mwana wa Yerohamu. Hao ndio waliokuwa maafisa wa makabila ya Israeli.
23 But David did not take the number of them from twenty years old and under, because the LORD had said he would increase Israel like the stars of the sky.
Daudi hakuwahesabu watu waliokuwa chini ya miaka ishirini, kwa sababu Bwana alikuwa ameahidi kuwafanya Israeli kuwa wengi kama nyota za angani.
24 Joab the son of Zeruiah began to take a census, but did not finish; and wrath came on Israel for this. The number was not put into the account in the chronicles of King David.
Yoabu mwana wa Seruya alianza kuwahesabu watu lakini hakumaliza. Kwa sababu ya kuwahesabu watu, hasira ya Mungu iliwaka juu ya Israeli, nayo hiyo hesabu yao haikuingizwa katika kitabu cha kumbukumbu za Mfalme Daudi.
25 Over the king’s treasures was Azmaveth the son of Adiel. Over the treasures in the fields, in the cities, in the villages, and in the towers was Jonathan the son of Uzziah;
Azmawethi mwana wa Adieli ndiye alikuwa msimamizi wa hazina za mfalme. Msimamizi wa hazina katika mashamba, miji, vijiji na kwenye ngome alikuwa Yonathani mwana wa Uzia.
26 Over those who did the work of the field for tillage of the ground was Ezri the son of Chelub.
Ezri mwana wa Kelubu alikuwa msimamizi wa wafanyakazi waliolima katika mashamba.
27 Over the vineyards was Shimei the Ramathite. Over the increase of the vineyards for the wine cellars was Zabdi the Shiphmite.
Shimei Mramathi alikuwa msimamizi wa mashamba ya mizabibu. Zabdi Mshifmi alikuwa msimamizi wa zabibu, utengenezaji na uhifadhi wa divai katika mapipa makubwa.
28 Over the olive trees and the sycamore trees that were in the lowland was Baal Hanan the Gederite. Over the cellars of oil was Joash.
Baal-Hanani Mgederi ndiye alikuwa mwangalizi wa mashamba ya mfalme ya mizeituni na mikuyu katika tambarare za vilima vya magharibi. Yoashi alikuwa msimamizi wa ghala za mafuta ya zeituni.
29 Over the herds that fed in Sharon was Shitrai the Sharonite. Over the herds that were in the valleys was Shaphat the son of Adlai.
Shitrai Msharoni alikuwa msimamizi wa makundi ya ngʼombe waliojilisha huko Sharoni. Shafati mwana wa Adlai alikuwa msimamizi wa yale makundi ya ngʼombe yaliyokuwa makondeni.
30 Over the camels was Obil the Ishmaelite. Over the donkeys was Jehdeiah the Meronothite. Over the flocks was Jaziz the Hagrite.
Obili Mwishmaeli alikuwa msimamizi wa ngamia. Yedeya Mmeronothi alikuwa msimamizi wa punda.
31 All these were the rulers of the property which was King David’s.
Yazizi Mhagri alikuwa msimamizi wa makundi ya kondoo na mbuzi. Hawa wote ndio waliokuwa maafisa wasimamizi wa mali alizokuwa nazo Mfalme Daudi.
32 Also Jonathan, David’s uncle, was a counselor, a man of understanding, and a scribe. Jehiel the son of Hachmoni was with the king’s sons.
Yonathani mjomba wa Daudi alikuwa mshauri, mtu mwenye ufahamu mkubwa na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakmoni alikuwa akiwahudumia wana wa mfalme.
33 Ahithophel was the king’s counselor. Hushai the Archite was the king’s friend.
Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme. Hushai Mwariki alikuwa rafiki wa mfalme.
34 After Ahithophel was Jehoiada the son of Benaiah, and Abiathar. Joab was the captain of the king’s army.
Baada ya Ahithofeli, Yehoyada mwana wa Benaya aliingia mahali pake kama mshauri wa mfalme pamoja na Abiathari. Yoabu alikuwa ndiye jemadari wa majeshi ya mfalme.

< 1 Chronicles 27 >