< 1 Chronicles 24 >

1 These were the divisions of the sons of Aaron. The sons of Aaron: Nadab, Abihu, Eleazar, and Ithamar.
Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 But Nadab and Abihu died before their father, and had no children; therefore Eleazar and Ithamar served as priests.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
3 David, with Zadok of the sons of Eleazar and Ahimelech of the sons of Ithamar, divided them according to their ordering in their service.
Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
4 There were more chief men found of the sons of Eleazar than of the sons of Ithamar; and they were divided like this: of the sons of Eleazar there were sixteen, heads of fathers’ houses; and of the sons of Ithamar, according to their fathers’ houses, eight.
Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
5 Thus they were divided impartially by drawing lots; for there were princes of the sanctuary and princes of God, both of the sons of Eleazar, and of the sons of Ithamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
6 Shemaiah the son of Nethanel the scribe, who was of the Levites, wrote them in the presence of the king, the princes, Zadok the priest, Ahimelech the son of Abiathar, and the heads of the fathers’ households of the priests and of the Levites; one fathers’ house being taken for Eleazar, and one taken for Ithamar.
Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
7 Now the first lot came out to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
8 the third to Harim, the fourth to Seorim,
ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
9 the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
10 the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
11 the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah,
ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
12 the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
13 the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab,
ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
14 the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
15 the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez,
ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
16 the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel,
ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
17 the twenty-first to Jachin, the twenty-second to Gamul,
ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
18 the twenty-third to Delaiah, and the twenty-fourth to Maaziah.
ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
19 This was their ordering in their service, to come into the LORD’s house according to the ordinance given to them by Aaron their father, as the LORD, the God of Israel, had commanded him.
Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
20 Of the rest of the sons of Levi: of the sons of Amram, Shubael; of the sons of Shubael, Jehdeiah.
Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
21 Of Rehabiah: of the sons of Rehabiah, Isshiah the chief.
Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
22 Of the Izharites, Shelomoth; of the sons of Shelomoth, Jahath.
Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
23 The sons of Hebron: Jeriah, Amariah the second, Jahaziel the third, and Jekameam the fourth.
Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
24 The sons of Uzziel: Micah; of the sons of Micah, Shamir.
Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
25 The brother of Micah: Isshiah; of the sons of Isshiah, Zechariah.
Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
26 The sons of Merari: Mahli and Mushi. The son of Jaaziah: Beno.
Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
27 The sons of Merari by Jaaziah: Beno, Shoham, Zaccur, and Ibri.
Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
28 Of Mahli: Eleazar, who had no sons.
Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
29 Of Kish, the son of Kish: Jerahmeel.
Wana wa Kishi: Yerameli
30 The sons of Mushi: Mahli, Eder, and Jerimoth. These were the sons of the Levites after their fathers’ houses.
wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
31 These likewise cast lots even as their brothers the sons of Aaron in the presence of David the king, Zadok, Ahimelech, and the heads of the fathers’ households of the priests and of the Levites, the fathers’ households of the chief even as those of his younger brother.
Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.

< 1 Chronicles 24 >