< Luke 5 >

1 Now it came to pass, while the multitude pressed upon him to hear the word of God, and having stood still, he was beside the lake of Gennesaret.
Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
2 And he saw two boats standing by the lake, but the fishermen having gone out of them, were washing their nets.
Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
3 And having entered into one of the boats, which was Simon's, he asked him to put out a little from the land. And having sat down, he taught the crowds from the boat.
Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
4 And when he stopped speaking, he said to Simon, Put out into the depth, and let down your nets for a catch.
kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
5 And having answered, Simon said to him, Master, having toiled through the whole night, we took nothing, but at thy saying, I will let down the net.
Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
6 And having done this, they enclosed a great multitude of fishes, and their net was tearing.
Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
7 And they beckoned to their partners in the other boat, after coming, to assist them. And they came and filled both the boats, so as for them to be sunk down.
Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
8 But Simon Peter having seen, he fell down at Jesus' knees, saying, Depart from me, because I am a sinful man, Lord.
Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
9 For astonishment surrounded him, and all those with him, at the catch of the fishes that they caught,
Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
10 and likewise also James and John, sons of Zebedee, who were partners with Simon. And Jesus said to Simon, Fear not, from henceforth thou will be catching men.
Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
11 And when they brought their boats to land, after forsaking all, they followed him.
Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
12 And it came to pass while he was in one of the cities, behold, a man full of leprosy. And having seen Jesus, having fallen on his face, he besought him, saying, Lord, if thou will, thou can make me clean.
Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
13 And having stretched forth his hand, he touched him, having said, I will, be thou clean. And straightaway the leprosy departed from him.
Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
14 And he commanded him to tell no man, but, After going, show thyself to the priest, and bring concerning thy cleansing, just as Moses commanded for a testimony to them.
“Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
15 But the report about him went through more, and many multitudes came together to hear, and to be healed by him from their infirmities.
Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
16 But he himself was withdrawing into the desolate regions, and praying.
Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
17 And it came to pass during one of those days, he was also teaching. And there were seated Pharisees and law teachers, who were men having come out of every town of Galilee and Judea and Jerusalem. And the power of the Lord was to heal them.
Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
18 And behold, men bringing a man on a bed who was paralyzed. And they sought to bring him in, and to lay him before him.
watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
19 And not having found how they might bring him in because of the multitude, after going up upon the housetop, they let him down through the tiles with the small bed into the midst in front of Jesus.
Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
20 And having seen their faith, he said to him, Man, thy sins are forgiven thee.
Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
21 And the scholars and the Pharisees began to deliberate, saying, Who is this who speaks blasphemies? Who can forgive sins, except God alone?
Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
22 But when Jesus perceived their thoughts, having responded, he said to them, Why do ye deliberate in your hearts?
Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
23 Which is easier, to say, Thy sins are forgiven thee, or to say, Arise and walk?
Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
24 But that ye may know that the Son of man has authority upon earth to forgive sins (he said to the paralyzed man), I say to thee, Arise, and after taking up thy small bed, go to thy house.
Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
25 And immediately having risen up before them, after taking up that on which he lay, he departed to his house glorifying God.
Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
26 And amazement gripped all, and they glorified God. And they were filled with fear, saying, We have seen strange things today.
Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
27 And after these things he went forth and saw a tax collector, named Levi, sitting at the tax office. And he said to him, Follow me.
Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
28 And after leaving behind all, having risen up, he followed him.
Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
29 And Levi made a great feast for him in his house, and there was a large crowd of tax collectors and others who were relaxing with them.
Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
30 And their scholars and Pharisees murmured against his disciples, saying, Why do ye eat and drink with the tax collectors and sinners?
Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
31 And having answered, Jesus said to them, Those who are well have no need of a physician, but those faring badly.
Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
32 I have not come to call the righteous but sinners to repentance.
Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
33 And they said to him, Why do the disciples of John fast often, and make supplications, and likewise those of the Pharisees, but thine eat and drink.
Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
34 And he said to them, Ye cannot make the sons of the wedding hall fast while the bridegroom is with them.
Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
35 But the days will also come when the bridegroom will be taken away from them, then they will fast in those days.
Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
36 And he also spoke a parable to them. No man puts a patch of a new garment on an old garment, otherwise both the new tears, and that from the new will not blend with the old.
Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
37 And no man puts new wine into old wineskins, otherwise the new wine will burst the wineskins, and will itself be spilled, and the wineskins will be ruined.
pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
38 But new wine must be put into fresh wineskins, and both are preserved together.
Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 And no man having drunk old straightaway desires new, for he says, The old is better.
Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'

< Luke 5 >