< Luke 4 >

1 And Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led by the Spirit into the wilderness,
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 being tempted forty days by the devil. And he ate nothing in those days, and when they were ended, afterward he was hungry.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 And the devil said to him, If thou are the Son of God, speak to this stone that it may become bread.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 And Jesus answered, saying to him, It is written, Man will not live on bread alone, but on every saying of God.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 And having brought him onto a high mountain, the devil showed him all the kingdoms of the world in a moment of time.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 And the devil said to him, I will give to thee all this authority, and the glory of them, because it has been delivered to me, and to whomever I want I give it.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 If therefore thou will worship before me, it will all be thine.
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 And having answered, Jesus said to him, Go thee behind me, Satan. It is written, Thou shall worship the Lord thy God, and him only shall thou serve.
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 And he brought him to Jerusalem, and set him on the pinnacle of the temple, and he said to him, If thou are the Son of God, cast thyself down from here,
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 for it is written, He will give his agents orders about thee, to protect thee,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 and, They will take thee up on their hands, lest thou dash thy foot against a stone.
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 And having answered, Jesus said to him, It is said, Thou shall not challenge the Lord thy God.
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 And when the devil ended every temptation, he withdrew from him until a time.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 And Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee. And a report went out about him through the entire region around.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 And he taught in their synagogues, being glorified by all.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 And he came to Nazareth, where he was brought up. And according to that which was customary to him, he entered into the synagogue on the sabbath day, and stood up to read.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 And the book of the prophet Isaiah was given to him. And having opened the book, he found the place where it was written,
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 The Spirit of the Lord is upon me, because he anointed me to preach good news to the poor. He has sent me to heal the broken hearted, to proclaim deliverance to the captives, and recovering of sight to the blind, to sent forth in deliverance those who have been broken,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 to proclaim the acceptable year of the Lord.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 And having closed the book, having given it back to the attendant, he sat down. And the eyes of all in the synagogue were focused on him.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 And he began to say to them, Today this scripture has been fulfilled in your ears.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 And all witnessed to him, and wondered at the words of grace that proceeded out of his mouth. And they said, Is this not the son of Joseph?
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 And he said to them, Ye will doubtless say to me this proverb: Physician, heal thyself. How many things we heard that happened at Capernaum, do also here in thy fatherland.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 And he said, Truly I say to you, that not one prophet is acceptable in his fatherland.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 But in truth I say to you, many widows were in Israel in the days of Elijah, when the sky was shut up for three years and six months, when a great famine occurred on all the land.
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 And Elijah was sent to none of them, except to Zarephath, to a widow woman of Sidon.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 And many lepers were in Israel near Elisha the prophet, and none of them was cleansed, except Naaman the Syrian.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 And all in the synagogue were filled with rage, having heard these things.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 And having risen up, they thrust him outside of the city, and brought him as far as the brow of the hill on which their city had been built, in order to throw him down headlong.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 But he, having passed through the midst of them, departed.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 And he came down to Capernaum, a city of Galilee. And he was teaching them on the sabbath day,
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 and they were astonished at his teaching, for his word was with authority.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 And in the synagogue there was a man who had a spirit of an unclean deity. And it cried out in a great voice, saying,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 Oh no! What is with us and with thee, Jesus of Nazareth? Did thou come to destroy us? I know thee who thou are, the Holy man of God.
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 And Jesus rebuked it, saying, Be thou muzzled, and come out of him. And the demon having thrown him down in the midst, it came out of him, not having harm him.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 And amazement developed in all, and they spoke among each other, saying, What is this word? Because with authority and power he commands the unclean spirits, and they come out.
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 And a report about him went forth into every place of the region around.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 And having arisen from the synagogue, he entered into the house of Simon. And Simon's mother-in-law was gripped by a great fever, and they besought him about her.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 And having stood over her, he rebuked the fever. And it left her, and immediately after rising up, she served them.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 And when the sun was setting, all, as many as had those who were incapacitated with various diseases, brought them to him. And having laid his hands on each one of them, he healed them.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 And also demons came out from many, crying out, and saying, Thou are the Christ, the Son of God. And rebuking them, he did not allow them to speak, because they knew him to be the Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 And when it became day, having departed, he went to a desolate place. And the multitudes sought him, and they came to him, and were restraining him not depart from them.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 But he said to them, I must preach the good news of the kingdom of God to the other cities also, because I was sent for this.
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 And he was preaching in the synagogues of Galilee.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luke 4 >