< Ephesians 3 >

1 For this reason I Paul, the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles,
Kwa sababu ya hii mimi, Paulo, ni mfungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu Mataifa.
2 since indeed ye heard of the administration of the grace of God, which was given to me for you,
Na amini ya kwamba mmesikia juu ya kazi ya neema ya Mungu aliyo nipa kwa ajili yenu.
3 that according to revelation he made known to me the mystery, as I wrote before in brief.
Nawaandikieni kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu. Huu ni ukweli uliyofichika ambao niliandika kwa kifupi kwenye barua nyingine.
4 With which reading ye can recognize my understanding in the mystery of the Christ,
Usomapo kuhusu haya, utaweza kutambua busara yangu katika ukweli huu uliofichika kuhusu Kristo.
5 which in other generations was not made known to the sons of men, as it has now been revealed by Spirit to his holy apostles and prophets.
Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa wana wa watu. Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho kwa Mitume waliotengwa na Manabii.
6 For Gentiles to be fellow-heirs, and of the same body, and fellow partakers of his promise in the Christ through the good news.
Ukweli huu uliofichika ni kwamba watu wa Mataifa ni washiriki wenzetu na wajumbe wenzetu wa mwili. Niwashiriki pamoja na ahadi ya Kristo Yesu kupitia injili.
7 Of which I became a helper according to the gift of that grace of God, which was given to me according to the working of his power.
Na kwa hili nimefanyika mtumishi kwa zawadi ya neema ya Mungu iliyotolewa kwangu kupitia utendaji wa nguvu yake.
8 To me, a man less than the least of all the sanctified, this grace was given to preach good news among the Gentiles, the unsearchable wealth of Christ,
Mungu alitoa zawadi hii kwangu, japo kuwa mimi ni mtu mdogo wa wote katika wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu. Zawadi hii ni kwamba inanipasa kuwatangazia mataifa injili yenye utajiri usiochunguzika wa Kristo.
9 and to make all men see what is the administration of the mystery hidden from the ages in God who created all things through Jesus Christ. (aiōn g165)
inanipasa kuwaangazia watu wote juu ya nini ni mpango wa Mungu wa siri. Huu ni mpango ambao ulikuwa umefichwa kwa miaka mingi iliyopita, na Mungu ambaye aliviumba vitu vyote. (aiōn g165)
10 So that now the manifold wisdom of God might be made known to the principal offices and the positions of authority in the heavenly things, through the church,
Hii ilikuwa kwamba, kupitia Kanisa, watawala na mamlaka katika sehemu za mbingu wapate kujua pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu.
11 according to the purpose of the ages, which he made in Christ Jesus our Lord, (aiōn g165)
Haya yangetokea kupitia mpango wa milele ambao aliukamilisha ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
12 in whom we have boldness and access in confidence through his faith.
Kwa kuwa katika Kristo tuna ujasiri na uwezo wa kuingia kwa ujasiri kwa sababu ya imani yetu kwake.
13 Therefore I ask that ye not become discouraged at my tribulations on your behalf, which is your glory.
Kwa hiyo nawaomba msikate tamaa kwasababu ya mateso yangu kwa ajili yenu. Haya ni utukufu wenu.
14 For this reason I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
Kwa sababu hii napiga magoti kwa Baba.
15 from whom every patriarchy in heavens and on earth is named.
ambaye kwa yeye kila familia mbinguni na juu ya nchi imeitwa jina.
16 So that he would grant you, according to the wealth of his glory, to be strengthened with power through his Spirit for the inner man,
Ninaomba kwamba apate kuwanemesha, kutokana na utajiri wa utukufu wake, awafanye imara kwa nguvu kupitia Roho wake, ambaye yu ndani yenu.
17 for the Christ to dwell in your hearts through faith,
Ninaomba kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani.
18 having been rooted and grounded in love, so that ye may be able to grasp with all the sanctified what is the breadth and length and depth and height,
Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Muwe katika pendo lake ili muweze kuelewa, pamoja na wote waaminio, jinsi upana, na urefu na kimo na kina cha upendo wa Kristo.
19 and to become aware of the love of the Christ, which transcends knowledge, so that ye may be filled in all the fullness of God.
Ninaomba Kwamba mjue ukuu wa upendo wa Kristo, ambao unazidi ufahamu. Mfanye haya ili mjazwe na ukamilifu wote wa Mungu.
20 Now to him who is able to do above extraordinary-above all things that we ask or think-according to the power that works in us,
Na sasa kwake yeye awezaye kufanya kila jambo, zaidi ya yote tuyaombayo au tuyawazayo, kupitia nguvu yake itendayo kazi ndani yetu,
21 to him is the glory in the church in Christ Jesus for all generations of the age of the ages. Truly. (aiōn g165)
kwake yeye kuwe utukufu ndani ya kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina. (aiōn g165)

< Ephesians 3 >