< Psalmen 135 >

1 Halleluja! Looft Jahweh’s Naam, Looft Hem, dienaars van Jahweh:
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Gij, die in het huis van Jahweh staat, In de voorhoven van het huis van onzen God!
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Looft Jahweh: want Jahweh is goed, Verheerlijkt zijn Naam: want die is zo lieflijk;
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Want Jahweh heeft Zich Jakob verkoren, En Israël tot zijn bezit!
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Ja, ik weet het: Jahweh is groot, Onze Heer boven alle goden verheven;
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Jahweh doet wat Hij wil In hemel en aarde, in zeeën en diepten.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 Hij laat de wolken verrijzen Aan de kimmen der aarde; Smeedt de bliksem tot regen, Haalt de wind uit zijn schuren.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 Hij was het, die Egypte’s eerstgeborenen sloeg, Van mensen en vee;
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Die tekenen en wonderen deed in uw midden, Egypte, Tegen Farao en al die hem dienden;
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 Die talrijke volken versloeg, En machtige koningen doodde:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 Sichon, den vorst der Amorieten, En Og, den koning van Basjan. Hij was het, die alle vorsten vernielde En alle koninkrijken van Kanaän;
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 En die hun land ten erfdeel gaf, Tot bezit aan Israël, zijn volk.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Uw Naam duurt eeuwig, o Jahweh, Uw roem, o Jahweh, van geslacht tot geslacht;
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Want Jahweh schaft recht aan zijn volk, En ontfermt Zich over zijn dienaars.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Maar de goden der volken zijn zilver en goud, Door mensenhanden gemaakt:
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Ze hebben een mond, maar kunnen niet spreken; Ogen, maar kunnen niet zien;
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Oren, maar kunnen niet horen; Ze hebben geen adem in hun mond.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Aan hen worden gelijk, die ze maken, En allen, die er op hopen!
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Huis van Israël, zegent dan Jahweh; Huis van Aäron, zegent dan Jahweh;
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Huis van Levi, zegent dan Jahweh; Die Jahweh vrezen, zegent dan Jahweh;
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Gezegend zij Jahweh uit Sion, Hij, die in Jerusalem woont!
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Psalmen 135 >