< Salme 81 >

1 (Til Sangmesteren. Al-haggittit. Af Asaf.) Jubler for Gud, vor Styrke, råb af fryd for Jakobs Gud,
Mwimbieni Mungu aliye nguvu yetu kwa sauti; pigeni kelele za furaha kwa Mungu wa Yakobo.
2 istem Lovsang, lad Pauken lyde, den liflige Citer og Harpen;
Imbeni wimbo na pigeni matari, kinubi chenye sauti nzuri pamoja na kinanda.
3 stød i Hornet på Nymånedagen, ved Fuldmåneskin på vor Højtidsdag!
Pigeni panda mwandamo wa mwezi, katika siku ya mbalamwezi, mwanzoni mwa sikukuu.
4 Thi det er Lov i Israel, et Bud fra Jakobs Gud;
Kwa kuwa ni agizo kwa Israeli, amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo.
5 han gjorde det til en Vedtægt i Josef, da han drog ud fra Ægypten, hvor han hørte et Sprog, han ikke kendte.
Aliitoa kama maelekezo kwa Yusufu alipoenda katika nchi ya Misri, ambako nilisikia sauti ambayo sikuweza kuitambua:
6 "Jeg fried hans Skulder for Byrden, hans Hænder slap fri for Kurven.
“Niliutua mzigo kutoka mabegani mwake; mikono yake ilipumzishwa kubeba kikapu.
7 I Nøden råbte du, og jeg frelste dig, jeg svarede dig i Tordenens Skjul, jeg prøvede dig ved Meribas Vande. (Sela)
Katika dhiki yako uliniita, nami nikakusaidia; nilikujibu kutoka katika wingu jeusi la radi. Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba. (Selah)
8 Hør, mit Folk, jeg vil vidne for dig, Israel, ak, om du hørte mig!
Sikilizeni, watu wangu, nami nitawaonya, Israeli, kama tu ugalinisikiliza!
9 En fremmed Gud må ej findes hos dig, tilbed ikke andres Gud!
Lazima kati yenu kusiwepo na mungu wa kigeni; haupaswi kumwabudu mungu wa kigeni.
10 Jeg, HERREN, jeg er din Gud! som førte dig op fra Ægypten; luk din Mund vidt op, og jeg vil fylde den!
Mimi ni Yahwe niliyekutoa katika nchi ya Misri, fungua sana kinywa chako, nami nitakijaza.
11 Men mit Folk vilde ikke høre min Røst, Israel lød mig ikke.
Lakini watu wangu hawakusikiliza maneno yangu; Israeli hawakunitii.
12 Da lod jeg dem fare i deres Stivsind, de vandrede efter deres egne Råd.
Nikawaacha waende katika katika njia yao wenyewe ya ukaidi ili kwamba waweze kufanya kinachoonekana sahihi kwao.
13 Ak, vilde mit Folk dog høre mig, Israel gå mine Veje!
Oh, laiti watu wangu wangenisikiliza mimi; oh, watu wangu wangelitembea katika njia yangu.
14 Da kued jeg snart deres Fjender, vendte min Hånd mod deres Uvenner!
Kisha ningewatiisha adui zao haraka na kugeuzia mkono wangu dhidi ya watesi wao.
15 Deres Avindsmænd skulde falde og gå til Grunde for evigt;
Wale wanaomchukia Yahwe katika hofu na waanguke chini mbele zake! Wawe wanyonge milele.
16 jeg nærede dig med Hvedens Fedme, mættede dig med Honning fra Klippen!"
Ningewalisha Israeli kwa ngano bora; Ningewatosheleza kwa asali itokayo mwambani.”

< Salme 81 >