< Salme 106 >

1 Halleluja! Lov Herren, thi han er god, thi hans miskundhed varer evindelig!
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Hvo kan opregne Herrens vældige gerninger, finde ord til at kundgøre al hans pris?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Salige de, der holder på ret, som altid øver retfærdighed!
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Husk os, Herre, når dit folk finder nåde, lad os få godt af din frelse,
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 at vi må se dine udvalgtes lykke, glæde os ved dit folks glæde og med din arvelod prise vor lykke!
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Vi syndede som vore Fædre, handlede ilde og gudløst.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Vore Fædre i Ægypten ænsede ej dine Undere, kom ikke din store Miskundhed i Hu, stod den Højeste imod ved det røde Hav.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 Dog frelste han dem for sit Navns Skyld, for at gøre sin Vælde kendt;
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 han trued det røde Hav, og det tørrede ud, han førte dem gennem Dybet som gennem en Ørk;
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 han fried dem af deres Avindsmænds Hånd og udløste dem fra Fjendens Hånd;
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 Vandet skjulte dem, som trængte dem, ikke een blev tilbage af dem;
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 da troede de på hans Ord og kvad en Sang til hans Pris.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Men de glemte snart hans Gerninger, biede ej på hans Råd;
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 de grebes af Attrå i Ørkenen, i Ødemarken fristed de Gud;
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 så gav han dem det, de kræved og sendte dem Lede i Sjælen.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 De bar Avind mod Moses i Lejren, mod Aron, HERRENs hellige;
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 Jorden åbned sig, slugte Datan, lukked sig over Abirams Flok;
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Ilden rasede i deres Flok, Luen brændte de gudløse op.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 De lavede en Kalv ved Horeb og tilbad det støbte Billed;
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 de byttede deres Herlighed bort for et Billed af en Okse, hvis Føde er Græs;
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 de glemte Gud, deres Frelser, som øvede store Ting i Ægypten,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Undere i Kamiternes Land, frygtelige Ting ved det røde Hav.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Da tænkte han på at udrydde dem, men Moses, hans udvalgte Mand, stilled sig i Gabet for hans Åsyn for at hindre, at hans Vrede lagde øde.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 De vraged det yndige Land og troede ikke hans Ord,
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 men knurrede i deres Telte og hørte ikke på HERREN;
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 da løfted han Hånden og svor at lade dem falde i Ørkenen,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 splitte deres Sæd blandt Folkene, sprede dem rundt i Landene.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 De holdt til med Ba'al-Peor og åd af de dødes Ofre;
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 de krænked ham med deres Gerninger, og Plage brød løs iblandt dem.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Da stod Pinehas frem og holdt Dom, og Plagen blev bragt til at standse,
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 og det regnedes ham til Retfærdighed fra Slægt til Slægt, evindelig.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 De vakte hans Vrede ved Meribas Vand, og for deres Skyld gik det Moses ilde;
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 thi de stod hans Ånd imod, og han talte uoverlagte Ord.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 De udryddede ikke de Folk, som HERREN havde sagt, de skulde,
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 med Hedninger blandede de sig og gjorde deres Gerninger efter;
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 deres Gudebilleder dyrkede de, og disse blev dem en Snare;
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 til Dæmonerne ofrede de, og det både Sønner og Døtre;
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 de udgød uskyldigt Blod, deres Sønners og Døtres Blod, som de ofred til Kana'ans Guder, og Landet blev smittet ved Blod;
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 de blev urene ved deres Gerninger, bolede ved deres idrætter.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Da blev HERREN vred på sit Folk og væmmedes ved sin Arv;
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 han gav dem i Folkenes Hånd, deres Avindsmænd blev deres Herrer;
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 deres Fjendervoldte dem Trængsel, de kuedes under deres Hånd.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Han frelste dem Gang på Gang, men de stod egensindigt imod og sygnede hen i Brøden;
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 dog så han til dem i Trængslen, så snart han hørte dem klage;
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 han kom sin Pagt i Hu og ynkedes efter sin store Miskundhed;
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 han lod dem finde Barmhjertighed hos alle, der tog dem til Fange.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Frels os, HERRE vor Gud, du samle os sammen fra Folkene, at vi må love dit hellige Navn, med Stolthed synge din Pris.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Lovet være HERREN, Israels Gud, fra Evighed og til Evighed! Og alt Folket svare Amen!
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Salme 106 >