< 4 Mosebog 1 >

1 HERREN talede således til Moses i Sinaj Ørken i Åbenbaringsteltet på den første Dag i den anden Måned af det andet år efter deres Udvandring fra Ægypten:
Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
2 Optag det samlede Tal på hele Israelitternes Menighed efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved at tælle Navnene på alle af Mandkøn, Hoved for Hoved;
'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
3 fra Tyveårsalderen og opefter skal du og Aron mønstre alle våbenføre Mænd i Israel, Hærafdeling for Hærafdeling;
kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
4 en Mand af hver Stamme skal hjælpe eder dermed, Overhovedet for Stammens Fædrenehuse.
Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
5 Navnene på de Mænd, der skal stå eder bi, er følgende: Af Ruben Elizur, Sjedeurs Søn;
Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
6 af Simeon Sjelumiel, Zurisjaddajs Søn;
kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
7 af Juda Nahasjon, Amminadabs Søn;
Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 af Issakar Netanel, Zuars Søn;
Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
9 af Zebulon Eliab, Helons Søn;
kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
10 af Josefs Sønner: Af Efraim Elisjama, Ammihuds Søn, af Manasse Gamliel, Pedazurs Søn;
kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
11 af Benjamin Abidan, Gidonis Søn;
kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
12 af Dan Ahiezer, Ammisjaddajs Søn;
Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
13 af Aser Pagiel, Okrans Søn;
kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
14 af Gad Eljasaf, Deuels Søn,
kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
15 og af Naftali Ahira, Enans Søn.
na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
16 Det var de Mænd, der udtoges af Menigheden, Øversterne for deres Fædrenestammer, Overhovederne for Israels Stammer.
Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
17 Da tog Moses, og Aron disse Mænd, hvis Navne var nævnet,
Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
18 og de kaldte hele Menigheden sammen på den første Dag i den anden Måned. Så lod de sig indføre i Familielisterne efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, Hoved for Hoved,
na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
19 som HERREN havde pålagt Moses. Således mønstrede han dem i Sinaj Ørken.
Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
20 Rubens, Israels førstefødtes, Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene Hoved for Hoved, alle af Mandkøn fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
21 de, som mønstredes af Rubens Stamme, udgjorde 46500.
Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
22 Simeons Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, så mange af dem, som mønstredes ved Optælling af Navnene Hoved for Hoved, alle af Mandkøn, fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
23 de, som mønstredes af Simeons Stamme, udgjorde 59 300.
Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
24 Gads Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
25 de, som mønstredes af Gads Stamme, udgjorde 45650.
Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
26 Judas Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
27 de, som mønstredes af Judas Stamme, udgjorde 74600.
walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
28 Issakars Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
29 de, som mønstredes af Issakars Stamme, udgjorde 54 400.
Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
30 Zebulons Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
31 de, som mønstredes af Zebulons Stamme, udgjorde 57 400.
Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
32 Josefs Sønner: Efraims Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
33 de, som mønstredes af Efraims Stamme, udgjorde 40500;
Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
34 Manasses Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
35 de, som mønstredes af Manasses Stamme, udgjorde 32200.
Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
36 Benjamins Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd.
Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
37 de, som mønstredes at Benjamins Stamme, udgjorde 35400.
Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
38 Dans Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
39 de, som mønstredes af Dans Stamme, udgjorde 62 700.
Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
40 Asers Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
41 de, som mønstredes af Asers Stamme, udgjorde 41 500.
Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
42 Naftalis Sønner, deres Efterkommere efter deres Slægter, efter deres Fædrenehuse, ved Optælling af Navnene fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd,
Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
43 de, som mønstredes af Naftalis Stamme, udgjorde 53 400.
Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
44 Det var dem, som mønstredes, dem, Moses og Aron og Israels tolv Øverster, en for hvert Fædrenehus, mønstrede.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
45 Og alle, som mønstredes af Israeliterne efter deres Fædrenehuse fra Tyveårsalderen og opefter, alle våbenføre Mænd i Israel,
Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
46 alle, som mønstredes, udgjorde 603 550.
Walihesabu wanaume 603, 550.
47 Men Leviterne efter deres Fædrenestamme mønstredes ikke sammen med dem.
Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
48 HERREN talede til Moses og sagde:
Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
49 Kun Levis Stamme må du ikke mønstre, og dens samlede Tal må du ikke optage sammen med de andre Israeliters.
“usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
50 Du skal overdrage Leviterne Tilsynet med Vidnesbyrdets Bolig, alle dens Redskaber og alt dens Tilbehør; de skal bære Boligen og alle dens Redskaber, de skal betjene den, og rundt om Boligen skal de have deres Lejr.
Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
51 Når Boligen skal bryde op, skal Leviterne tage den ned, og når Boligen skal gå i Lejr, skal Leviterne rejse den. Enhver Lægmand, der kommer den nær, skal lide Døden.
Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
52 Israeliterne skal lejre sig hver i sin Lejrafdeling og under sit Felttegn, Hærafdeling for Hærafdeling,
Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
53 men Leviterne skal lejre sig rundt om Vidnesbyrdets Bolig, for at der ikke skal komme Vrede over Israelitternes Menighed; og Leviterne skal tage Vare på, hvad der er at varetage ved Vidnesbyrdets Bolig.
Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
54 Og Israeliterne gjorde ganske, hvad HERREN havde pålagt Moses.
Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.

< 4 Mosebog 1 >