< 3 Mosebog 18 >

1 HERREN talede fremdeles til Moses og sagde:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 Tal til Israeliterne og sig til dem: Jeg er HERREN eders Gud!
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
3 Som de handler i Ægypten, hvor I opholdt eder, må I ikke handle, og som de handler i Kana'ans Land, hvor jeg fører eder hen, må I ikke handle; I må ikke vandre efter deres Anordninger.
Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
4 Efter mine Lovbud skal I handle. og mine Anordninger skal I holde, så I vandrer efter dem; jeg er HERREN eders Gud!
Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 I skal holde mine Anordninger og Lovbud; det Menneske, der handler efter dem, skal leve ved dem. Jeg er HERREN!
Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 Ingen af eder må komme sine kødelige Slægtninge nær, så han blotter deres Blusel. Jeg er HERREN!
Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 Din Faders og din Moders Blusel må du ikke blotte; hun er din Moder, du må ikke blotte hendes Blusel!
Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 Din Faders Hustrus Blusel må du ikke blotte, det er din Faders Blusel.
Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 Din Søsters Blusel, hvad enten hun er din Faders eller din Moders Datter, hvad enten hun er født i eller uden for Hjemmet, hendes Blusel må du ikke blotte.
Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 Din Sønnedatters eller Datterdatters Blusel må du ikke blotte, det er din egen Blusel.
Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 En Datter, din Faders Hustru har med din Fader hun er din Søster hendes Blusel må du ikke blotte.
Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 Din Fasters Blusel må du ikke blotte, hun er din Faders kødelige Slægtning.
Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 Din Mosters Blusel må du ikke blotte, hun er din Moders kødelige Slægtning.
Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 Din Farbroders Blusel må du ikke blotte, du må ikke komme hans Hustru nær, hun er din Faster.
Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 Din Sønnekones Blusel må du ikke blotte, hun er din Søns Hustru, du må ikke blotte hendes Blusel.
Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 Din Broders Hustrus Blusel må du ikke blotte, det er din Broders Blusel.
Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 En Kvindes og hendes Datters Blusel må du ikke blotte, heller ikke må du ægte hendes Sønnedatter eller Datterdatter, så at du blotter hendes Blusel; de er hendes kødelige Slægtninge; det er grov Utugt.
Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 Søster må du ikke tage til Søsters Medhustru, så længe Søsteren lever, så du blotter både den enes og den andens Blusel.
Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 Du må ikke komme en Kvinde nær under hendes månedlige Urenhed, så du blotter hendes Blusel.
Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
20 Med din Næstes Hustru må du ikke have Samleje, så du bliver uren ved hende.
Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
21 Dit Afkom må du ikke give hen til at ofres til Molok; du må ikke vanhellige din Guds Navn. Jeg er HERREN!
Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
22 Hos en Mand må du ikke ligge, som man ligger hos en Kvinde; det er en Vederstyggelighed.
Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
23 Med intet som helst Dyr må du have Omgang, så du bliver uren derved; en Kvinde må ikke stille sig hen for et dyr til kønslig Omgang; det er en Skændsel.
Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
24 Gør eder ikke urene med noget sådant, thi med alt sådant har de Folkeslag, jeg driver bort foran eder, gjort sig urene.
Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
25 Derved blev Landet urent, og jeg straffede det for dets Brøde, og Landet udspyede sine Indbyggere.
Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
26 Hold derfor mine Anordninger og Lovbud og øv ikke nogen af disse Vederstyggeligheder, det gælder både den indfødte og den fremmede, der bor iblandt eder
Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
27 thi alle disse Vederstyggeligheder øvede Indbyggerne, som var der før eder, og Landet blev urent
Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
28 for at ikke Landet skal udspy eder, når I gør det urent, ligesom det udspyede det Folk, som var der før eder.
Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
29 Thi enhver, som øver nogen af alle disse Vederstyggeligheder, de, der øver dem, skal udryddes af deres Folk.
Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
30 Så hold mine Forskrifter, så I ikke øver nogen af de vederstyggelige Skikke, som øvedes før eders Tid, at I ikke skal gøre eder urene ved dem. Jeg er HERREN eders Gud!
Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.

< 3 Mosebog 18 >