< Jeremias 19 >

1 Således sagde HERREN: Gå hen og køb dig et krus hos pottemageren, tag nogle af Folkets og Præsternes Ældste med
Hili ndilo asemalo Bwana: “Nenda ukanunue gudulia la udongo kutoka kwa mfinyanzi. Wachukue baadhi ya wazee wa watu na wa makuhani
2 og gå ud i Hinnoms Søns Dal ved Indgangen til Potteskårporten og udråb der de Ord, jeg taler til dig!
na mtoke mwende mpaka kwenye Bonde la Ben-Hinomu, karibu na ingilio la Lango la Vigae. Huko tangaza maneno ninayokuambia,
3 Du skal sige: Hør HERRENs Ord, Judas Konger og Jerusalems Borgere: Så siger Hærskarers HERRE, Israels Gud: Se, jeg sender over dette Sted en Ulykke, så det skal ringe for Ørene på enhver, der hører derom,
nawe useme, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda na watu wa Yerusalemu. Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Sikilizeni! Nitaleta maafa mahali hapa, ambayo yatafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yawashe.
4 fordi de forlod mig og gjorde dette Sted fremmed og tændte Offerild der for andre Guder, som hverken de eller deres Fædre før kendte til, og Judas Konger fyldte dette Sted med skyldfries Blod,
Kwa kuwa wameniacha na kupafanya mahali hapa kuwa pa miungu ya kigeni. Wameiteketezea sadaka miungu ambayo wao wala baba zao wala wafalme wa Yuda kamwe hawakuijua, nao wamelijaza eneo hili kwa damu isiyo na hatia.
5 og de byggede Baalshøjene for at brænde deres Børn i Ild som Brændofre til Baal, hvad jeg ikke havde påbudt eller talt om, og hvad aldrig var opkommet i min Tanke.
Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama sadaka kwa Baali, kitu ambacho sikukiamuru wala kukitaja, wala hakikuingia akilini mwangu.
6 Se, derfor skal Dage komme, lyder det fra HERREN, da dette Sted ikke mere skal hedde Tofet og Hinnoms Søns Dal, men Morddalen.
Hivyo jihadharini, siku zinakuja, asema Bwana, wakati watu hawatapaita tena mahali hapa Tofethi ama Bonde la Ben-Hinomu, bali Bonde la Machinjo.
7 Jeg gør Juda og Jerusalem rådvilde på dette Sted og lader dem falde for Sværdet for deres Fjenders Øjne og for deres Hånd, som står dem efter Livet, og jeg giver Himmelens Fugle og Jordens Dyr deres Lig til Føde.
“‘Nitaiharibu mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa. Nitawafanya waanguke kwa upanga mbele ya adui zao, katika mikono ya wale watafutao uhai wao, nami nitaitoa mizoga yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.
8 Jeg gør denne By til Gru og Spot; alle, der komnmer forbi, skal grue og spotte over alle dens Sår.
Nitauharibu mji huu na kuufanya kitu cha kudharauliwa. Wote wapitao karibu watashangaa na kuudhihaki kwa sababu ya majeraha yake yote.
9 Jeg lader dem æde deres Sønners og Døtres Kød, den ene skal æde den andens Kød under Belejringen og den Trængsel, deres Fjender og de, der står dem efter Livet, volder dem.
Nitawafanya wao kula nyama ya wana wao na binti zao; kila mmoja atakula nyama ya mwenzake wakati wa dhiki ya kuzungukwa na jeshi lililowekwa juu yao na adui wanaotafuta uhai wao.’
10 Knus så Kruset i de Mænds Påsyn, der følger med dig,
“Kisha livunje lile gudulia wale walio pamoja nawe wakiwa wanaangalia,
11 og sig til dem: Så siger Hærskarers HERRE: Jeg vil knuse dette Folk og denne By, som man knuser et Lerkar, så det ikke kan heles igen. De døde skal jordes i Tofet, fordi Pladsen til at jorde på ikke slår til.
uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: Nitalivunja taifa hili na mji huu kama gudulia hili la mfinyanzi lilivyovunjwa, nalo haliwezi kutengenezeka tena. Watawazika waliokufa huko Tofethi hata isiwepo nafasi zaidi.
12 Således vil jeg gøre med dette Sted og dets indbyggere, lyder det fra HERREN, idet jeg gør denne By til et Tofet:
Hivi ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na kwa wale waishio ndani yake, asema Bwana. Nitaufanya mji huu kama Tofethi.
13 Jerusalems og Judas Kongers Huse skal blive urene som Tofets Sted, alle de Huse, på hvis Tage de tændte Offerild for al Himmelens Hær og udgød Drikofre for andre Guder.
Nyumba zilizoko Yerusalemu na zile za wafalme wa Yuda zitatiwa unajisi kama mahali hapa, Tofethi: yaani nyumba zote ambazo walifukiza uvumba juu ya mapaa yake kwa jeshi lote la angani, na kumimina dhabihu za vinywaji kwa miungu mingine.’”
14 Derpå gik Jerenmias fra Tofet, hvorhen HERREN havde sendt ham for at profetere, og stod frenm i Forgården til HERRENs Hus og sagde til alt Folket:
Kisha Yeremia akarudi kutoka Tofethi, mahali ambapo Bwana alikuwa amemtuma kutoa unabii, akasimama katika ua wa Hekalu la Bwana na kuwaambia watu wote,
15 Så siger Hærskarers HERRE, Israels Gud: Se, over denne By og alle Byerne, der hører til den, sender jeg al den Ulykke, jeg har truet den med, fordi de gjorde Nakken stiv og ikke hørte mine Ord.
“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya mji huu pamoja na vijiji vinavyouzunguka kila maafa niliyosema dhidi yake, kwa sababu wamekuwa na shingo ngumu, na hawakuyasikiliza maneno yangu.’”

< Jeremias 19 >