< 2 Timoteus 3 >

1 Men vid dette, at i de sidste Dage skulle vanskelige Tider indtræde.
Lakini fahamu hili: katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati ngumu.
2 Thi Menneskene skulle være egenkærlige, pengegridske, praleriske, hovmodige, spottelystne, ulydige imod Forældre, utaknemmelige, ryggesløse,
kwa sababu watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye majivuno, wenye dhihaka, wasiotii wazazi wao, wasiokuwa na shukurani na waovu.
3 ukærlige, uforligelige, bagtaleriske, uafholdne, rå, uden Kærlighed til det gode,
Wasio na upendo wa asili, wasiotaka kuishi kwa amani na yeyote, wachonganishi, wasingiziaji, wasioweza kujizuia, wenye vurugu, wasiopenda mema.
4 forræderske, fremfusende, opblæste, Mennesker, som mere elske Vellyst, end de elske Gud,
Watakuwa wasaliti, wakaidi, wenye kujipenda wenyewe na wapenda anasa kuliko kumpenda Mungu.
5 som have Gudfrygtigheds Skin, men have fornægtet dens Kraft. Og fra disse skal du vende dig bort!
Kwa nje watakuwa na sura ya ucha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe na watu hao.
6 Thi til dem høre de, som snige sig ind i Husene og fange Kvindfolk, der ere belæssede med Synder og drives af mange Hånde Begæringer
Kwa kuwa baadhi yao ni wanaume wanaoingia kwenye familia za watu na kushawishi wanawake wajinga. Hawa ni wanawake waliojawa dhambi na wenye kuongozwa na tamaa za kila aina.
7 og altid lære og aldrig kunne komme til Sandheds Erkendelse.
Wanawake hawa hujifunza siku zote, lakini kamwe hawawezi kuufikia ufahamu wa ile kweli.
8 Men ligesom Jannes og Jambres stode Moses imod, således modstå også disse Sandheden: Mennesker, fordærvede i Sindet, forkastelige i Troen.
Kama vile ambavyo Yane na Yambre walisimama kinyume na Musa. Kwa njia hii walimu hawa wa uongo husimama kinyume na kweli. Ni watu walioharibiwa katika fikira zao, wasiokubalika kuhusiana na imani.
9 Dog, de skulle ikke få Fremgang ydermere; thi deres Afsind skal blive åbenbart for alle, ligesom også hines blev.
Lakini hawataendelea mbali. Kwa kuwa upumbavu wao utawekwa wazi kwa watu wote, kama ulivyokuwa wa wale watu.
10 Du derimod har efterfulgt mig i Lære, i Vandel, i Forsæt, Tro, Langmodighed, Kærlighed, Udholdenhed,
Lakini wewe umeyafuata mafundisho yangu, mwenendo wangu, makusudi yangu, imani yangu, uvumilivu wangu, upendo wangu na ustahimilivu wangu,
11 i Forfølgelser, i Lidelser, sådanne, som ere komne over mig i Antiokia, i Ikonium, i Lystra, sådanne Forfølgelser, som jeg har udstået, og Herren har friet mig ud af dem alle.
mateso, maumivu na yaliyonipata kule Antiokia, Ikonio na Listra. Niliyavumilia mateso. Bwana aliniokoa katika yote hayo.
12 Ja, også alle de, som ville leve gudfrygtigt i Kristus Jesus, skulle forfølges.
Wote wanaotaka kuishi katika maisha ya kumcha Mungu katika Kristo Yesu watateswa.
13 Men onde Mennesker og Bedragere ville gå frem til det værre; de forføre og forføres.
Watu waovu na wadanganyifu watazidi kuwa waovu zaidi. Watawapotosha wengine. Wao wenyewe wamepotoshwa.
14 Du derimod, bliv i det, som du har lært, og som du er bleven forvisset om, efterdi du ved, af hvem du har lært det,
Lakini wewe, dumu katika mambo uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti. Kwa kuwa unajua umejifunza kwa nani.
15 og efterdi du fra Barn af kender de hellige Skrifter, som kunne gøre dig viis til Frelse ved Troen på Kristus Jesus.
Unatambua ya kuwa tangu utotoni mwako uliyajua maandiko matakatifu. Haya yanaweza kukuhekimisha kwa ajili ya wokovu kwa njia ya imani katika kristo Yesu.
16 Hvert Skrift er indåndet af Gud og nyttig til Belæring, til Irettesættelse, til Forbedring, til Optugtelse i Retfærdighed,
Kila andiko limetiwa pumzi na Mungu. Linafaa kwa mafundisho yenye faida, kwa kushawishi, kwa kurekebisha makosa, na kwa kufundishia katika haki.
17 for at Guds-Mennesket må vorde fuldkomment, dygtiggjort til al god Gerning.
Hii ni kwamba mtu wa Mungu awe kamili, akiwa amepewa nyenzo zote kwa ajili ya kutenda kila kazi njema.

< 2 Timoteus 3 >