< Anden Krønikebog 1 >

1 Salomo, Davids Søn, fik sikret sig Magten, og HERREN hans Gud var med ham og gjorde ham overmåde mægtig.
Selemani mwana wa Daudi, aliimariswa katika utawala wake, na Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye na alimpa nguvu nyingi sana.
2 Da tilsagde Salomo hele Israel, Tusind- og Hundredførerne, Dommerne og alle Israels Øverster, Fædrenehusenes Overhoveder,
Sulemani akasema kwa Israleli wote, na maakida wa maelfu na wa mamia, na kwa waamuzi, na kwa kila mfalme kiongozi katika Israeli yote, wakuu wa kaya.
3 og ledsaget af hele Forsamlingen drog han til Offerhøjen i Gibeon. Der stod Guds Åbenbaringstelt, som HERRENs Tjener Moses havde rejst i Ørkenen,
Hivyo Sulemani na kusanyiko lote wakaenda pamoja naye sehemu ya juu iliyokuwa Gibeoni, maana ndipo palikuwepo hema ya kukutania ya Mungu, ambayo Musa mtumishi wa Yahwe, alikuwa ameitengeneza jangwani.
4 men Guds Ark havde David bragt op fra Kijat-Jearim til det Sted, han havde beredt den, idet han havde ladet rejse et Telt til den i Jerusalem.
Lakini Daudi alikuwa ameleta pale sanduku la Mungu kutoka Kiriath yeriam hadi sehemu ambayo alikuwa ametayarisha, maana alikuwa ameliandalia hema huko katika Yerusalemu.
5 Men Kobberalteret, som Bezal'el, en Søn af Hurs Søn Uri, havde lavet, stod der foran HERRENs Bolig, og der søgte Salomo og Forsamlingen ham.
Zaidi ya hayo, madhabahu ya shaba iliyotengenezwa na Bezaleli mwana wa uri mwana wa Huri ilikuwepo huko kabla ya mbele ya madhabahu ya Yahwe; Sulemani na kusanyiko wakaenda ilikokuwa. (Maandiko ya zamani yanasema
6 Og Salomo ofrede der på Åbenbaringsteltets Kobberalter, som stod foran HERRENs Åsyn, han ofrede 1000 Brændofre derpå.
Selemani akaenda huko kwenye kwenye madhabahu ya shaba mbele za Yahwe, ambayo ilikuwepo mahali pa hema ya kukutamia, na akatoa sadaka elfu za kuteketezwa juu yake.
7 Samme Nat lod Gud sig til Syne for Salomo og sagde til ham: "Sig, hvad du ønsker, jeg skal give dig!"
Mungu akamtokea Selemani usiku huo na akasema kwake, “Omba! Nikupe nini?”
8 Da sagde Salomo til Gud: "Du viste stor Miskundhed mod min Fader David, og du har gjort mig til Konge i hans Sted.
Selemani akasema kwa Mungu, “Umeonesha agano la uaminifu mkuu kwa Daudi baba yangu, na umenifanya mfalme katika nafasi yaye.
9 Så lad da, Gud HERRE, din Forjæftelse til min Fader David gå i Opfyldelse, thi du har gjort mig til Konge over et Folk, der er talrigt som Jordens Støv.
Sasa, Yahwe Mungu, ahadi yako kwa Daudi baba yangu itimie, maana umenifanya mfalme juu ya watu wengi kama mavumbi ya dunia.
10 Giv mig derfor Visdom og Indsigt, så jeg kan færdes ret over for dette Folk, thi hvem kan dømme dette dit store Folk?"
Sasa nipe hekima na maarifa, ili niweze kuwaongoza watu hawa, maana ni nani anayeweza kuwaamua watu wako, ambao ni wengi sana kwa idadi?”
11 Da sagde Gud til Salomo: "Fordi din Hu står til dette, og du ikke bad om Rigdom, Gods og Ære eller om dine Avindsmænds Liv, ej heller om et langt Liv, men om Visdom og Indsigt til at dømme mit Folk, som jeg gjorde dig til Konge over,
Mungu akasema kwa Selemani, “Kwa kuwa hili lilikuwa kwenye moyo wako, na kwa kuwa hujaomba mali, utajiri, au heshima, wala maisha ya wale wanaokuchukia, wala maish marefu kwa jili yako binafsi, lakini umeomba hekima na maarifa kwa ajili yako, ili uwatawale watu wangu, ambao juu yao nimekufanya mfame, na hivi ndivyo nitafanya.
12 så skal du få Visdom og Indsigt; men jeg giver dig også Rigdom, Gods og Ære, så at ingen Konge før dig har haft Mage dertil. og ingen efter dig skal have det."
Sasa nitakupa hekima na maarifa, pia nitakupa mali na utajiri, na heshima, kuliko wafalme wote waliokuwepo kabla yako walivyokuwa, na baada yako hakuna yeyote atakayekuwa navyo.”
13 Derpå begav Salomo sig fra Offerhøjen i Gibeon, fra Pladsen foran Åbenbaringsteltet, til Jerusalem; og han herskede som Konge over Israel.
Kwa hiyo Selemani akaenda Yerusalemu kutoka sehemu ya juu iliyokuwepo Gibeoni, kutoka mbele ya hema ya kukutania; akatawala juu ya Israeli.
14 Salomo anskaffede sig Stridsvogne og Ryttere, og han havde 1400 Vogne og 12000 Ryttere; dem lagde han dels i Vognbyerne, dels hos sig i Jerusalem.
Selemani akakusanya magari na wanaume waendesha farasi, naye alikuwa na magari 1, 400 na waendesha farasi kumi na mbili elfu ambao aliwaweka katika miji ya magari, pamoja naye, mfalme katika Yerusalemu.
15 Kongen bragte det dertil, af Sølv og Guld i Jerusalem var lige så almindeligt som Sten, og Cedertræ lige så almindeligt som Morbærfigentræ i Lavlandet.
Mfalme akatengeneza fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe katika Yerusalemu, na mbao za mierezi kuwa kama miti ya mikuyu iliyomo katika nyanda za chini.
16 Hestene, Salomo indførte, kom fra Mizrajim og Kove; Kongens Handelsfolk købte dem i Kove.
Selemani katika uagizaji wa farasi kutoka Misiri, wafanya biashara wake walinunua farasi kutoka Misiri kwa bei stahiki.
17 De udførte en Vogn fra Mizrajim for 600 Sekel Sølv, en Hest for150 Ligeledes udførtes de ved Handelsfolkenes Hjælp til alle Hetiternes og Arams Konger.
Waliagiza gari kutoka Misiri kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi mmoja kwa shekeli 150. Pia walinunua kutoka kwa wafalme wa Wahiti na wafalme wa Washamu.

< Anden Krønikebog 1 >