< Mudre Izreke 19 >

1 Bolji je siromah koji živi u nedužnosti nego čovjek opakih usana i k tomu bezuman.
Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
2 Revnost bez razboritosti nije dobra, i tko brzo hoda, spotiče se.
Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
3 Ludost čovjeku kvari život, a srce mu se ljuti na Jahvu!
Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
4 Bogatstvo pribavlja mnoge prijatelje, a siromaha i njegov prijatelj ostavlja.
Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
5 Lažljiv svjekok ne ostaje bez kazne, i tko širi laži, neće uteći.
Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
6 Mnogi laskaju licu odličnikovu i svatko je prijatelj čovjeku darežljivu.
Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
7 Na siromaha mrze sva braća njegova, još više se udaljuju od njega prijatelji njegovi: on hlepi za dobrim riječima, ali ih ne nalazi!
Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
8 Tko stječe razboritost, ljubi sebe, a tko čuva razum, nalazi sreću.
Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
9 Lažljiv svjedok ne ostaje bez kazne, i tko širi laži, propada.
Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
10 Ne dolikuje bezumnomu živjeti raskošno, a još manje sluzi vlast nad knezovima.
Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
11 Um čovjeka usteže od srdžbe, a čast mu je oprostiti krivicu.
Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
12 Kraljev je gnjev kao rika lavlja, a njegova milost kao rosa bilju.
Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
13 Nesreća je ocu svojemu bezuman sin, i neprestano prokišnjavanje svađe su ženine.
Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
14 Kuća se i bogatstvo baštine od otaca, a od Jahve je žena razumna.
Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
15 Lijenost navlači čovjeku dubok san i nemarna duša gladuje.
Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
16 Tko se drži zapovijedi, čuva život svoj, a tko ne pazi putove svoje, umire.
Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
17 Jahvi pozaima tko je siromahu milostiv, i on će mu platiti dobročinstvo.
Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
18 Kažnjavaj sina svoga dok ima nade, ali ne idi za tim da ga ubiješ.
Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
19 Tko je jarostan, plaća globu, i kad ga štediš, samo uvećavaš njegov gnjev.
Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
20 Slušaj savjet i primaj pouku, kako bi naposljetku postao mudar.
Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
21 Mnogo je namisli u srcu čovječjem, ali što Jahve naumi, to i bude.
Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
22 Dražest je čovjekova u dobroti njegovoj, i bolji je siromah od lažljivca.
Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
23 Strah Gospodnji daje život, i tko se njime ispuni, zlo ga ne pohodi.
Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
24 Lijenčina umače ruku u zdjelu, ali je ustima svojim ne prinosi.
Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
25 Udari podsmjehivača, i lud se opameti; ukori razumnog, i shvatit će znanje.
Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
26 Sin je sramotan i pokvaren tko zlostavlja oca i odgoni majku.
Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
27 Prestani, sine moj, slušati naputke koji odvode od riječi spoznaje!
Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
28 Nevaljao se svjedok podruguje pravdi i usta opakih gutaju nepravdu.
Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
29 Pripravljene su kazne podsmjevačima i udarci za leđa bezumnika.
Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.

< Mudre Izreke 19 >