< Job 38 >

1 Nato Jahve odgovori Jobu iz oluje i reče:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 “Tko je taj koji riječima bezumnim zamračuje božanski promisao?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Bokove svoje opaši k'o junak: ja ću te pitat', a ti me pouči.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Gdje si bio kad zemlju utemeljih? Kazuj, ako ti je znanje sigurno.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 Znaš li tko joj je mjere odredio i nad njom uže mjerničko napeo?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 Na čemu joj počivaju temelji? Tko joj postavi kamen ugaoni
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 dok su klicale zvijezde jutarnje i Božji uzvikivali dvorjani?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 Tko li zatvori more vratnicama kad je navrlo iz krila majčina;
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 kad ga oblakom k'o haljom odjenuh i k'o pelenam' ovih maglom gustom;
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 kad sam njegovu odredio među, vrata stavio sa prijevornicama?
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 Dotle, ne dalje, rekao sam njemu, tu nek' se lomi ponos tvog valovlja!
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 Zar si ikad zapovjedio jutru, zar si kazao zori mjesto njeno,
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 da poduhvati zemlju za rubove i da iz nje sve bezbožnike strese;
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 da je pretvori u glinu pečatnu i oboji je k'o kakvu haljinu.
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 Ona uzima svjetlost zlikovcima i pesnicu im lomi uzdignutu.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Zar si ti prodro do izvora morskih, po dnu bezdana zar si kad hodio?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 Zar su ti vrata smrti pokazali; vidje li dveri kraja mrtvih sjena?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 Zar si prostranstvo zemlje uočio? Govori, ako ti je znano sve to.
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 Koji putovi u dom svjetla vode, na kojem mjestu prebivaju tmine,
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 da ih odvedeš u njine krajeve, da im put k stanu njihovu pokažeš?
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Ti znadeš to, tÓa davno ti se rodi, tvojih dana broj veoma je velik!
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 Zar si stigao do riznica snijega i zar si tuče spremišta vidio
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 što ih pričuvah za dane nevolje, za vrijeme boja krvava i rata?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 Kojim li se putem dijeli munja kada iskre po svoj zemlji prosipa?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Tko li je jaz iskopao povodnju, tko prokrčio pute grmljavini
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 da bi daždjelo na kraj nenastanjen, na pustinju gdje žive duše nema,
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 da bi neplodnu napojio pustoš, da bi u stepi trava izniknula?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Ima li kiša svoga roditelja? Tko je taj koji kapi rose rađa?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 Iz čijeg li mraz izlazi krila, tko slanu stvara što s nebesa pada?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 Kako čvrsnu vode poput kamena i led se hvata površja bezdana?
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 Možeš li lancem vezati Vlašiće i razdriješiti spone Orionu,
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 u pravo vrijeme izvesti Danicu, vodit' Medvjeda s njegovim mladima?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 Zar poznaješ ti zakone nebeske pa da njima moć na zemlji dodijeliš?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 Zar doviknuti možeš oblacima pa da pljuskovi tebe poslušaju?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 Zar na zapovijed tvoju munje lijeću i tebi zar se odazivlju: 'Evo nas'?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 Tko je mudrost darovao ibisu, tko li je pamet ulio u pijetla?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 Tko to mudro prebrojava oblake i tko nebeske izlijeva mjehove
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 dok se zemlja u tijesto ne zgusne i dok se grude njezine ne slijepe?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 Zar ćeš ti plijen uloviti lavici ili ćeš glad utažit' lavićima
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 na leglu svojem dok gladni čekaju i vrebaju na žrtvu iz zaklona?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Tko hranu gavranovima pribavlja kad Bogu ptići njegovi cijuču i naokolo oblijeću bez hrane?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< Job 38 >