< Postanak 14 >

1 Kad Amrafel bijaše kralj Šineara, Ariok kralj Elasara, Kedor-Laomer kralj Elama, Tidal kralj Gojima,
Ikiwa katika siku za Amrafeli, mfalme wa shinari, Arioko, mfalme wa Elasari, Kedorlaoma, mfalme wa Elam na Tidali, mfalme wa Goimu,
2 povedoše oni rat protiv Bere, kralja Sodome, Birše, kralja Gomore, Šinaba, kralja Adme, Šemebera, kralja Sebojima, i protiv kralja u Beli, to jest Soaru.
walifanya vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha, mfalme wa Gomora, Shinabu, mfalme wa Adma, Shemeberi, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela(pia ikiitwa Soari).
3 I vojske se sliju u dolinu Sidim, gdje je danas Slano more.
Hawa wafalme watano wa mwisho waliungana pamoja katika bonde la Sidim (pia likiitwa bahari ya chumvi).
4 Dvanaest su godina služili Kedor-Laomera, ali trinaeste godine dignu se na ustanak.
Kwa miaka kumi na mbili walimtumikia Kedorlaoma, lakini katika mwaka wa kumi na tatu waliasi.
5 U četrnaestoj godini digne se Kedor-Laomer i kraljevi koji su bili s njim te potuku Refaimce u Ašterot Karnajimu, Zuzijce u Hamu, Emijce na ravnici Kirjatajimu,
Kisha katika mwaka wa kumi na nne, Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae walikuja na kuwashambulia Warefai katika Ashteroth Karnaimu, na Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe Kiriathaimu,
6 Horijce u brdskom kraju Seiru, blizu El Parana, koji je uz pustinju.
na Wahori katika mlima wao wa Seiri, mpaka El Parani iliyo karibu na jangwa.
7 Onda se povuku natrag i stignu u En Mišpat, to jest Kadeš, i pokore sve krajeve Amalečana i Amorejaca, koji su nastavali Haseson Tamar.
Kisha wakarudi wakaja En Misifati (Pia ikiitwa Kadeshi), na kuishinda nchi yote ya Waamaleki, na pia Waamori ambao waliishi Hasasoni Tamari.
8 Zatim istupi kralj Sodome, kralj Gomore, kralj Adme, kralj Sebojima i kralj Bele, odnosno Soara, te zapodjenu borbu protiv onih u dolini Sidimu:
Kisha mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboim, na mfalme wa Bela (pia ikiitwa Soari) walikwenda na kuandaa vita
9 Kedor-Laomera, kralja Elama, Tidala, kralja Gojima, Amrafela, kralja Šineara, Arioka, kralja Elasara - četiri kralja protiv pet.
dhidi ya Kadorlaoma, mfalme wa Elam, Tidali mfalme wa Goim, Amrafeli, mfalme wa Shinari, Arioki, mfalme wa Elasari; wafme wanne dhidi ya wale watano.
10 Dolina Sidim bila je puna provalija s paklinom, pa kraljevi Sodome i Gomore, na bijegu, u njih poskaču, a ostali izmaknu u planine.
Na sasa bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, na wafalme wa Sodoma na Gomora walipokimbia, wakaanguka pale. Wale waliosalia wakakimbilia milimani.
11 Pobjednici pokupe sve blago po Sodomi i Gomori i svu hranu pa odu.
Kwa hiyo adui akachukua mali zote za Sodoma na Gomora na vyakula vyao vyote, na wakaenda zao,
12 Pograbe i Lota, Abramova bratića - i on je živio u Sodomi - i njegovo blago pa otiđu.
walipoondoka, wakamchukua pia Lutu, mtoto wa ndugu yake na Abram ambaye aliishi Sodoma, pamoja na mali zake zote.
13 A bjegunac neki - rođak Eškola i Anera, Abramovih saveznika - donese vijest Abramu Hebrejcu dok je boravio kod hrasta Amorejske Mamre.
Mmoja ambaye alitoroka alikuja na kumwambia Abram mwebrania. Alikuwa anaishi katika mialoni ya Mamre, mwamori ambaye alikuwa ni ndugu wa Eshkoli na Aneri ambao walikuwa washirika wa Abram.
14 Kad je Abram čuo da mu je bratić zarobljen, skupi svoju momčad - rođenu u njegovu domu - njih trista osamnaest, pa pođe u potjeru do Dana.
Abram aliposikia kuwa maadui wamemteka ndugu yake, akawaongoza wanaume waliofunzwa na kuzaliwa nyumbani mwake 318 na akawaongoza hadi Dani.
15 Podijeli svoje momke u dvije čete, napadne noću te one potuče. Progonio ih je do Hobe, sjeverno od Damaska.
Akawagawanya watu wake dhidi yao usiku na kuwavamia, na kuwafukuza mpaka Hoba, ambayo iko kaskazini mwa Dameski.
16 Povrati sve blago, svoga bratića Lota i njegovo blago, žene i ostali svijet.
Kisha akarudisha mali zote, pia akamrudisha ndugu yake Lutu na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
17 Pošto se vratio, porazivši Kedor-Laomera i kraljeve koji su bili s njim, u susret mu, u dolinu Šave, to jest u Kraljev dol, iziđe kralj Sodome.
Baada ya Abram kurudi kutoka kumpiga Kadorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja nae, mfalme wa Sodoma akatoka kuonana nae katika bonde la Shawe (pia iliitwa bonde la mfalme).
18 A Melkisedek, kralj Šalema, iznese kruha i vina. On je bio svećenik Boga Svevišnjega.
Melkizedeki, mfalme wa Salem, akaleta mkate na divai. Alikuwa ni kuhani wa Mungu aliye juu sana.
19 Blagoslovi ga govoreći: “Od Boga Svevišnjega, Stvoritelja neba i zemlje, neka je Abramu blagoslov!
Alimbariki akisema, “Abarikiwea Abram na Mungu aliye juu sana, muumba wa mbingu na nchi.
20 I Svevišnji Bog, što ti u ruke preda neprijatelje, hvaljen bio!” Abram mu dade desetinu od svega.
Abarikiwe Mungu aliye juu sana, ambaye amekupatia adui zako katika mikono yako.” Kisha Abram akampatia sehemu ya kumi ya kila kitu.
21 Tada kralj Sodome reče Abramu: “Meni daj ljude, a dobra uzmi sebi!”
Mfalme wa Sodama akamwambia Abram, “Nipatie watu, na ujichukulie wewe mwenyewe mali.”
22 Abram odgovori kralju Sodome: “Ruku uzdižem pred Jahvom, Svevišnjim Stvoriteljem neba i zemlje,
Abram akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua juu mkono wangu kwa Yahwe, Mungu aliye juu sana, muumbaji wa mbingu na nchi,
23 da neću uzeti ni končića, ni remena od obuće, niti išta što je tvoje da ne kažeš: na meni se Abram obogatio.
kwamba sitachukua uzi wala gidamu ya kiatu, au kitu chochote ambacho ni chako, 'ili kwamba usiseme, nimemfanya Abram kuwa tajiri.'
24 Ne, meni ništa, osim što su moji momci upotrijebili; i dio za momčad što je sa mnom išla: Aner, Eškol i Mamre, oni neka uzmu svoj dio.”
Sitachukua chochote isipokuwa kile ambacho vijana wamekula na sehemu za watu waliokwenda nami. Aneri, Eskoli, na Mamre na wachukue sehemu zao.”

< Postanak 14 >