< 诗篇 146 >

1 你们要赞美耶和华! 我的心哪,你要赞美耶和华!
Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
2 我一生要赞美耶和华! 我还活的时候要歌颂我的 神!
Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
3 你们不要倚靠君王,不要倚靠世人; 他一点不能帮助。
Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
4 他的气一断,就归回尘土; 他所打算的,当日就消灭了。
Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
5 以雅各的 神为帮助、 仰望耶和华—他 神的,这人便为有福!
Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
6 耶和华造天、地、海,和其中的万物; 他守诚实,直到永远。
Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
7 他为受屈的伸冤, 赐食物与饥饿的。 耶和华释放被囚的;
Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
8 耶和华开了瞎子的眼睛; 耶和华扶起被压下的人。 耶和华喜爱义人。
Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
9 耶和华保护寄居的, 扶持孤儿和寡妇, 却使恶人的道路弯曲。
Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
10 耶和华要作王,直到永远! 锡安哪,你的 神要作王,直到万代! 你们要赞美耶和华!
Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.

< 诗篇 146 >