< 诗篇 143 >

1 大卫的诗。 耶和华啊,求你听我的祷告, 留心听我的恳求, 凭你的信实和公义应允我。
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie.
2 求你不要审问仆人; 因为在你面前,凡活着的人没有一个是义的。
Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako.
3 原来仇敌逼迫我, 将我打倒在地, 使我住在幽暗之处, 像死了许久的人一样。
Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani.
4 所以,我的灵在我里面发昏; 我的心在我里面凄惨。
Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.
5 我追想古时之日, 思想你的一切作为, 默念你手的工作。
Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya.
6 我向你举手; 我的心渴想你, 如干旱之地盼雨一样。 (细拉)
Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame.
7 耶和华啊,求你速速应允我! 我心神耗尽! 不要向我掩面, 免得我像那些下坑的人一样。
Ee Bwana, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni.
8 求你使我清晨得听你慈爱之言, 因我倚靠你; 求你使我知道当行的路, 因我的心仰望你。
Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.
9 耶和华啊,求你救我脱离我的仇敌! 我往你那里藏身。
Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako.
10 求你指教我遵行你的旨意, 因你是我的 神。 你的灵本为善; 求你引我到平坦之地。
Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare.
11 耶和华啊,求你为你的名将我救活, 凭你的公义,将我从患难中领出来,
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu.
12 凭你的慈爱剪除我的仇敌, 灭绝一切苦待我的人, 因我是你的仆人。
Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

< 诗篇 143 >