< 耶利米书 48 >

1 论摩押。万军之耶和华—以色列的 神如此说: 尼波有祸了!因变为荒场。 基列亭蒙羞被攻取; 米斯迦蒙羞被毁坏;
Juu ya Moabu, Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, “Ole kwa Nebo, kwani umekuwa ukiwa. Kiriathaimu umetekwa na kuaibishwa. Ngome zake zimeangushwa na kuaibishwa.
2 摩押不再被称赞。 有人在希实本设计谋害她,说: 来吧!我们将她剪除,不再成国。 玛得缅哪,你也必默默无声; 刀剑必追赶你。
Heshima ya Moabu haipo tena. Adui zake katika Heshboni walipanga njama za kumwangamiza. Walisema, 'Njoni tumwangamize kama taifa. Madmena pia itaangamizwa - upanga utakutangulia.'
3 从何罗念有喊荒凉大毁灭的哀声:
Sikilizeni! Sauti ya mvumo inakuja kutoka Horonaimu.
4 摩押毁灭了! 她的孩童发哀声,使人听见。
Moabu ameangamizwa. Vilio vya watoto wake vinasikika.
5 人上鲁希坡随走随哭, 因为在何罗念的下坡听见毁灭的哀声。
Wanapanda kilima cha Luhithi wakilia, njia yote kuelekea Horonaimu, vilio vinasikika kutokana na maangamizi.
6 你们要奔逃,自救性命, 独自居住,好像旷野的杜松。
Kimbieni! okeeni maisha yenu kama kichaka cha mreteni katika nyika.
7 你因倚靠自己所做的和自己的财宝必被攻取。 基抹和属他的祭司、首领也要一同被掳去。
Maana kwa sababu ya tumaini lenu katika matendo na utajiri wenu, ninyi pia mtatekwa. Kisha Kemoshi atachukuliwa matekani, pamoja na makuhani na viongozi wake.
8 行毁灭的必来到各城, 并无一城得免。 山谷必致败落, 平原必被毁坏; 正如耶和华所说的。
Maana mwaribu atafika kila mji; hakuna mji utakaookoka. Hivyo bonde litaangamia na tambarare itateketezwa, kama alivyosema Yahwe.
9 要将翅膀给摩押, 使她可以飞去。 她的城邑必致荒凉, 无人居住。 (
Mpeni Moabu mabawa, maana ni lazima aruke mbali bila shaka. Miji yake itakuwa magofu, pasipo na mtu wa kuishi humo.
10 懒惰为耶和华行事的,必受咒诅;禁止刀剑不经血的,必受咒诅。)
Na alaaniwe kila aliye mvivu katika kufanya kazi ya Yahwe! Na alaaniwe kila auzuiaye upanga wake usimwage damu!
11 摩押自幼年以来常享安逸, 如酒在渣滓上澄清, 没有从这器皿倒在那器皿里, 也未曾被掳去。 因此,它的原味尚存, 香气未变。
Moabu amekuwa akijisikia salama tangu alipokuwa kijana. Yeye ni kama mvinyo wake ambao haujamiminwa kutoka mtungi kwenda mtungi mwingine. Hajaenda matekani. Hivyo radha yake ni njema kama mwanzo; radha yake haibadiliki.
12 耶和华说:“日子将到,我必打发倒酒的往她那里去,将她倒出来,倒空她的器皿,打碎她的坛子。
Hivyo tazama, siku zinakuja - asema Yahwe - nitakapompelekea watakao mchovya na kumwaga mitungi yake yote na kupasua mitungi yake.
13 摩押必因基抹羞愧,像以色列家从前倚靠伯特利的神羞愧一样。
Kisha Moabu atamwaibikia Kemoshi kama ambavyo nyumba ya Israeli ilivyoiabikia Betheli, tumaini lao.
14 你们怎么说: 我们是勇士,是有勇力打仗的呢?
Utawezaje kusema, 'Tu askari, wapiganaji wenye nguvu'?
15 摩押变为荒场, 敌人上去进了她的城邑。 她所特选的少年人下去遭了杀戮; 这是君王—名为万军之耶和华说的。
Moabu itaangamizwa na miji yake kushambuliwa. Kwa maana vijana wake wazuri wameshuka katika eneo la machinjo. Hili ni tamko la mfalme! Yahwe wa majeshi ndilo jina lake.
16 摩押的灾殃临近; 她的苦难速速来到。
Maangazizo ya Moabu yanakaribia; maafa yanaharakisha.
17 凡在她四围的和认识她名的, 你们都要为她悲伤,说: 那结实的杖和那美好的棍, 何竟折断了呢?
Ninyi nyote mlio karibu na Moabu, ombolezeni. Nanyi mjuao fahari yake, pigeni kelele hivi, 'Ole, fimbo yenye nguvu, fimbo yenye heshima, imevunjwa.'
18 住在底本的民哪, 要从你荣耀的位上下来, 坐受干渴; 因毁灭摩押的上来攻击你, 毁坏了你的保障。
Shukeni kutoka mahali penu pa heshima na kuketi katika nchi kavu, ewe binti uishie Diboni. Maana aiangamizaye Moabu anakushambulia, atakayeziharibu ngome zako.
19 住亚罗珥的啊, 要站在道旁观望, 问逃避的男人和逃脱的女人说: 是什么事呢?
Simameni njiani na kuangalia, enyi mwishio katika Aroeri. Waulizeni wanaokimbia na kutoroka. Sema, 'Nini kimetokea?'
20 摩押因毁坏蒙羞; 你们要哀号呼喊, 要在亚嫩旁报告说: 摩押变为荒场!
Moabu ameaibika, maana amevujwa. Lieni kwa sauti na uchungu; pigeni yowe kuomba msaada. Wambieni watu waliokando ya Mto Arinoni kwamba Moabu ameangamizwa.
21 “刑罚临到平原之地的何伦、雅杂、米法押、
Basi maangamizi yamefika katika nchi ya kilima, huko Holoni, Yakza, na Mefathi,
22 底本、尼波、伯·低比拉太音、
huko Diboni, Nebo, na Bethi Diblathaimu,
23 基列亭、伯·迦末、伯·米恩、
huko Kiriatahaimu, Beth Gamul, na Bethi Meoni,
24 加略、波斯拉,和摩押地远近所有的城邑。
huko Keriothi na Bozra, na katika miji yote iliyomo katika nchi ya Moabu - miji iliyoko mbali na karibu.
25 摩押的角砍断了,摩押的膀臂折断了。这是耶和华说的。”
Nguvu za Moabu zimekwisha; mkono wake umevunjwa - asema Yahwe.
26 “你们要使摩押沉醉,因她向耶和华夸大。她要在自己所吐之中打滚,又要被人嗤笑。
Mnywesheni, maana alitenda kwa kiburi kinyume changu, Yahwe. Basi Moabu anapiga makofi kwa machukizo kwa matapiko yake mwenyewe, hivyo amekuwa pia kitu cha kuchekesha.
27 摩押啊,你不曾嗤笑以色列吗?她岂是在贼中查出来的呢?你每逢提到她便摇头。
Maana Israeli hakuwa kitu cha kuchekesha kwako? Alionekana miongoni mwa wezi, kwamba ulitikisa kichwa chako kwake mara ulipoongea juu yake?
28 摩押的居民哪, 要离开城邑,住在山崖里, 像鸽子在深渊口上搭窝。
Jitengeni na miji na kuweka kambi katika minuko, enyi watu wa Moabu. Kuwa kama njiwa anayeatamia juu ya mlango wa tundu katika miamba.
29 我们听说摩押人骄傲, 是极其骄傲; 听说他自高自傲, 并且狂妄,居心自大。
Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu - majivuno yake, maringo, kiburi, utukufu binafsi na kujiinua moyoni.
30 耶和华说: 我知道他的忿怒是虚空的; 他夸大的话一无所成。
Hili ni tamko la Yahwe - mimi mwenyewe najua maneno yake ya ukaidi, yasiyosaidia chochote, kama matendo yake.
31 因此,我要为摩押哀号, 为摩押全地呼喊; 人必为吉珥·哈列设人叹息。
Hivyo nitavumisha maombolezo kwa ajili ya Moabu, na nitapiga kelele katika uzuni kwa ajili ya Moabu. Nitaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir Hereshi.
32 西比玛的葡萄树啊,我为你哀哭, 甚于雅谢人哀哭。 你的枝子蔓延过海, 直长到雅谢海。 那行毁灭的已经临到你夏天的果子 和你所摘的葡萄。
Nitalia zaidi kwa ajili yenu kuliko nilivyofanya kwa Yazeri, mzabibu wa Sibma! Matawi yako yalipita katika Bahari ya Chumvi na kufika hata Yazeri. Mwaribu ameshambulia matunda yenu ya kiangazi na mzabibu wenu.
33 肥田和摩押地的欢喜快乐都被夺去; 我使酒榨的酒绝流, 无人踹酒欢呼; 那欢呼却变为仇敌的呐喊。
Hivyo sherehe na furaha vimeondolewa kutoka miti ya matunda na nchi ya Moabu. Nimekomesha mvinyo kutoka mashinikizo yao. Hawatakanyaga kwa kelele za furaha. Kelele yoyote haitakuwa kelele ya furaha.
34 “希实本人发的哀声达到以利亚利,直达到雅杂;从琐珥达到何罗念,直到伊基拉·施利施亚,因为宁林的水必然干涸。”
Kutoka kelele huko Heshiboni hata kufika Eleale, sauti yao inasikika hata Yahazi, kutoka Soari hata Horonaimu na Eglathi Shelishiya, hata maji ya Nimrimu yamekauka.
35 耶和华说:“我必在摩押地使那在邱坛献祭的,和那向他的神烧香的都断绝了。
Maana nitamkomesha kila mtu katika Moabu atoaye sadaka mahali pa juu na kuteketeza uvumba kwa miungu yake - asema Yahwe.
36 我心腹为摩押哀鸣如箫,我心肠为吉珥·哈列设人也是如此,因摩押人所得的财物都灭没了。
Hivyo moyo wangu unamwombolezea Moabu kama zomari. Moyo wangu unaomboleza kama zomari kwa ajili ya watu wa Kir Heresi. Utajiri walioupata umekwisha.
37 “各人头上光秃,胡须剪短,手有划伤,腰束麻布。
Maana kila kichwa kina upaa na kila kidevu kimenyolewa. Chale zipo katika kila mkono, na nguo za magunia katika viuno vyao.
38 在摩押的各房顶上和街市上处处有人哀哭;因我打碎摩押,好像打碎无人喜悦的器皿。这是耶和华说的。
Maombolezo yapo kila mahali, juu ya kila paa la nyumba ya Moabu na katika masoko ya Moabu. Kwa maana nimeivunja Moabu kama chungu kisichotakiwa tena - asema Yahwe.
39 摩押何等毁坏!何等哀号!何等羞愧转背!这样,摩押必令四围的人嗤笑惊骇。”
Jinsi gani imeharibiwa! Jinsi wanavyopiga kelele katika maombolezo yao! Moabu ameigeuza kwa aibu! Hivyo Moabu atakuwa kitu cha kuchekwa na kitisho kwa wote wanaomzunguka.”
40 耶和华如此说: 仇敌必如大鹰飞起, 展开翅膀,攻击摩押。
Maana Yahwe asema hivi, “Tazama, adui atakuja akiruka kama tai, akieneza mabawa yake juu ya Moabu.
41 加略被攻取,保障也被占据。 到那日,摩押的勇士心中疼痛如临产的妇人。
Keriothi umetekwa, na ngome zake zimekamatwa. Maana siku hiyo myoyo ya askari wa Moabu itakuwa kama mioyo ya wanawake katika uchungu wa kujifungua.
42 摩押必被毁灭,不再成国, 因她向耶和华夸大。
Hivyo Moabu utaharibiwa kama watu, kwa kuwa walijivuna kinyume changu, Yahwe.
43 耶和华说:摩押的居民哪, 恐惧、陷坑、网罗都临近你。
Hofu na shimo, na mtego vinakujia, watu wa Moabu - asema Yahwe.
44 躲避恐惧的必坠入陷坑; 从陷坑上来的必被网罗缠住; 因我必使追讨之年临到摩押。 这是耶和华说的。
Kila akimbiaye kwa sababu ya hofu ataanguka shimoni, na kila atokaye shimoni atanaswa na mtego, maana nitayaleta haya juu yao katika mwaka wa kisasi changu dhidi yao - asema Yahwe.
45 躲避的人无力站在希实本的影下; 因为有火从希实本发出, 有火焰出于西宏的城, 烧尽摩押的角和哄嚷人的头顶。
Wakimbiao watasimama katika kivuli cha Heshboni bila nguvu, maana moto utatoka Heshboni, miale kutoka katikati ya Sihoni. Utateketeza paji la uso wa Moabu na juu ya vichwa vya watu wenye majivuno.
46 摩押啊,你有祸了! 属基抹的民灭亡了! 因你的众子都被掳去, 你的众女也被掳去。
Ole wako, Moabu! watu wa Kemoshi wameangamizwa, Kwa maana wana wako wamechukuliwa kama mateka na binti zako matekani.
47 耶和华说: 到末后,我还要使被掳的摩押人归回。 摩押受审判的话到此为止。
Lakini nitazirejesha siku njema za Moabu katika siku zijazo - asema Yahwe.” Hukumu ya Moabu inaishia hapa.

< 耶利米书 48 >