< 路加福音 4 >

1 耶穌充滿聖神,由約旦河回來,就被聖神引到荒野裏去了,
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 四十天的工夫受魔鬼試探;祂在那時期內什麼也沒有吃,過了那期就餓了。
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 魔鬼對祂說:「你若是天主子,命這塊石頭變成餅吧! 」
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 耶穌回答說:「經上記載:『人生活不只靠餅。』
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 魔鬼引祂到高處,頃時間把普世萬國指給祂看,
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 並對祂說:這一切權勢及其榮華,我都要給你,因為全交給我了;我願意把它給誰,就給誰。
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 所以你若是朝拜我,這一切都是的。」
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 耶穌回答說:「經上記載:『你要朝拜上主,你的天主;惟獨事奉祂。』」
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 魔鬼又引祂到耶路撒冷,把祂放在聖殿頂上,向祂說:「你若是天主子,從這裡跳下去吧!
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 因為經上記載:『祂為你吩咐自己的天使保護你,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 他們要用手托著你,色免得你的腳碰在石頭上。』」
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 耶穌回答說:「經上說:『不可試探上主,你的天主。』」
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 魔鬼用盡了各種試探後,就離開了祂,再等待機會。
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 耶穌因聖神的德能,回到加利肋亞。祂的名聲音傳遍了臨近各地。
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 祂在他們的會堂施教,受到眾人的稱揚。
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 祂來到了納匝肋,自己曾受教養的地方;按他們的慣例,就在安息日那天進了會堂,並站起來要誦讀。
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 有人把依撒意亞先知書遞給祂;祂遂展開書卷,找到了一處,上邊寫說:
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 『上主的神臨於我身上,因為祂給我傅了油,派遣我向貧窮人傳報善訊,向俘虜宣告釋放,向盲者宣告復明,使受壓迫者獲得自由,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 宣佈上主恩慈之年。』
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 祂把書卷捲起來,交給侍役,就坐下了。會堂內眾人的眼睛都注視著祂。
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 祂便開始對他們說:「你們剛才聽過的這段聖經,今天應驗了。」
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 眾人都驚奇他口中所說的動聽的話;並且說:「這不是若瑟的兒子嗎﹖」
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 他回答他們說:「你們必定要對我說這句俗語:醫生,醫治你自己! 我們聽說你在葛法翁所行的一切,也在你的家鄉這裡行吧! 」
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 祂又說:「我實在告訴你們:沒有一個先知在本鄉受到悅納的。
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 我據實告訴你們:在厄里亞時代,天閉塞了三年零六個月,遍地起了大飢荒,在以色列原有許多寡婦,
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 厄里亞並沒有被派遺到她們中的一個那裡去,而只到了漆冬匝爾法特的一個寡婦那裡。
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 在厄里叟先知時代,在以色列有許多癩病人,他們中沒有一個得潔淨的,只有敘利亞的納阿曼。」
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 在會堂中聽見這話的人,都忿怒填胸,
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 起來把祂出趕出城外,領祂到了山崖上,─他們的成是建在山上的─要把祂推下去。
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 祂卻由他們中間過去走了。
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 耶穌下到加利肋亞的葛法翁城,就在安息日教訓人。
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 人都十分驚奇祂的教訓,因為祂的話具有一種權威。
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 在會堂裡有一個附著邪魔惡鬼的人,他聲喊叫說:
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 「啊! 納匝肋人耶穌,我們與你有什麼相干? 你來毀滅我們嗎? 我們知道你是誰:是天主的聖者。」
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 耶穌吒斥他說:「不要作聲,從這人身上出去!」魔鬼把那人摔倒在人中間,便從他身上出去了,絲豪沒有傷害他。
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 遂有一種驚駭籠罩了眾人彼此談論說:「這是什麼事? 祂權柄和能力命令邪魔,而他們竟出去了!」
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 祂的名聲便傳遍了附近各地。
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 祂從會堂裡出來,進了西滿的家,西滿的岳母正發高熱,他們為她祈求耶穌。
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 耶穌就走到她身邊,叱退熱症,熱症就離開了她;她立刻起來服事他們。
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 日落後,眾人把所有患各種病症的,都領到祂跟前,祂就把手覆在每一個人身上,治好了他們。
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 又有些從許多人身上出來的魔鬼吶喊說:「你是天主子。」祂便叱責他們,不許他們說話,因為他們知道祂是默西亞。
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 天一亮,耶穌就出去到了荒野地方;群眾就尋找祂,一直來到祂那裡,挽留祂不要離開他們。
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 祂卻向他們說:「我也必須向別的城傳報天主國的喜訊,因為我被派遺,正是為了這事。」
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 祂就常在猶太的各會堂中宣講。
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< 路加福音 4 >