< 路加福音 5 >

1 有一天,耶稣站在革尼撒勒湖边,众人簇拥着他,希望聆听上帝之道。
Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.
2 耶稣看见两只船停在湖边,渔夫离开船去洗网了。
Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.
3 他走上西门的那只船,请他撑船到离岸不远的水面,然后坐下,在船上教导众人。
Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.
4 教导结束后,他对西门说:“把船划到水更深的地方,下网打鱼吧!”
Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, “Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki.”
5 西门说:“老师,我们整夜劳苦工作却一无所获,不过我愿听从你,我会撒网。”
Simoni akamjibu, “Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu.”
6 西门撒网后捞上很多鱼,几乎将网撑裂。
Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.
7 于是他叫来另外那只船上的同伴来帮忙,他们捞上来的鱼把两只船装满了,甚至压得船开始下沉。
Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama.
8 西门(彼得)看见这番情景,就跪在耶稣面前说:“主啊,你不能靠近我,因为我是个罪人。”
Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, “Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!”
9 因为他和身边其他人一样,完全被刚才捕捞上来的鱼数量惊住了。
Simoni pamoja na wenzake wote walishangaa kwa kupata samaki wengi vile.
10 西庇太的儿子雅各和约翰是西门的打鱼同伴,他们也有同样的感觉。耶稣对西门说:“不要怕!从现在起,你就要成为收获人的渔夫了。”
Hali kadhalika Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, waliokuwa wavuvi wenzake Simoni. Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope; tangu sasa utakuwa ukivua watu.”
11 这几名渔夫把两只船靠上岸后,便放下一切跟随耶稣。
Basi, baada ya kuzileta zile mashua ukingoni mwa ziwa, wakaacha yote, wakamfuata.
12 有一次,耶稣来到一个城中,一名严重的麻风病人看到他,就伏倒将脸贴在地上,求他说:“主啊!如果你愿意,就治愈我。”
Ikawa, Yesu alipokuwa katika mmojawapo wa miji ya huko, mtu mmoja mwenye ukoma mwili mzima akamwona. Basi, mtu huyo akaanguka kifudifudi akamwomba Yesu: “Mheshimiwa, ukitaka, waweza kunitakasa.”
13 耶稣伸手触碰他,说:“我愿意,治愈吧!”于是这个人的麻风病立刻好了。
Yesu akaunyosha mkono wake, akamgusa na kusema, “Nataka, takasika!” Mara ule ukoma ukamwacha.
14 耶稣嘱咐他:“不要告诉其他人,去给祭司看看,然后照着摩西所说的,为你的治愈进行献祭,向大家作证。”
Yesu akamwamuru: “Usimwambie mtu yeyote; bali nenda ukajionyeshe kwa kuhani, ukatoe sadaka kwa ajili ya kutakasika kwako kama inavyotakiwa na Sheria ya Mose, iwe uthibitisho kwao kwamba umepona.”
15 但关于耶稣的消息却传得越来越远,大量的民众来到这里聆听耶稣教导,希望他能治愈他们的疾病。
Lakini habari za Yesu zilizidi kuenea kila mahali. Watu makundi mengi wakakusanyika ili kumsikiliza na kuponywa magonjwa yao.
16 但耶稣却经常躲到安静的地方祷告。
Lakini yeye alikwenda zake mahali pasipo na watu, akawa anasali huko.
17 有一天,耶稣正在教导众人之时,人群中有法利赛人和宗教老师,他们来自加利利和犹太的乡村以及耶路撒冷。因为主的力量与耶稣同在,所以他可以治愈病患。
Siku moja Yesu alikuwa akifundisha. Mafarisayo na walimu wa Sheria kutoka katika kila kijiji cha Galilaya, Yudea na Yerusalemu, walikuwa wameketi hapo. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kwa ajili ya kuponyea wagonjwa.
18 几个人用床抬着一个瘫痪之人,想送他到耶稣跟前。
Mara watu wakaja wamemchukua mtu mmoja aliyepooza maungo, amelala kitandani; wakajaribu kumwingiza ndani wamweke mbele ya Yesu.
19 但因为这里的人实在太多,无法挤进房间,于是他们爬上房顶,在屋瓦中挖了一个洞,将患者和垫子通过洞放了下来,正好落在人群中耶稣的面前。
Lakini kwa sababu ya wingi wa watu, hawakuweza kuingia ndani. Basi, wakapanda juu ya dari, wakaondoa vigae, wakamshusha huyo aliyepooza pamoja na kitanda chake, wakamweka mbele ya Yesu.
20 耶稣看出了他们对他的信任,于是说:“你们的罪被宽恕了。”
Yesu alipoona jinsi walivyokuwa na imani kubwa, akamwambia huyo mtu, “Rafiki, umesamehewa dhambi zako.”
21 于是宗教老师和法利赛人开始议论:“这人是谁?竟然会说如此亵渎上帝之语?除了上帝,谁能宽恕罪过?”
Walimu wa Sheria na Mafarisayo wakaanza kujiuliza: “Nani huyu anayemkufuru Mungu kwa maneno yake? Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi ila Mungu peke yake!”
22 耶稣知道他们正在讨论这个问题,于是对他们说:“你们为什么会想到这样的问题?
Yesu alitambua mawazo yao, akawauliza, “Mnawaza nini mioyoni mwenu?
23 说‘你的罪已被宽恕’容易,还是说‘站起来走吧’容易?
Ni lipi lililo rahisi zaidi: kusema, Umesamehewa dhambi, au kusema, Simama utembee?
24 我想要向你们证明的是,人子在人间也有宽恕罪过的权力。”然后他对瘫痪之人说:“我现在对你说,站起来,拿着你的垫子回家去吧。”
Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anao uwezo wa kusamehe dhambi duniani.” Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Simama, chukua kitanda chako uende zako nyumbani.”
25 那人立刻在众人面前站起来,拿起刚才躺着的垫子,赞美着上帝离开了。
Mara, huyo mtu aliyepooza akasimama mbele yao wote, akachukua kitanda chake akaenda zake nyumbani huku akimtukuza Mungu.
26 众人对眼前的一切感到震惊,在倍感敬畏之余也纷纷开始赞美上帝。他们说:“我们今天见证了令人惊讶的事情。”
Wote wakashangaa na kushikwa na hofu; wakamtukuza Mungu wakisema: “Tumeona maajabu leo.”
27 稍后,耶稣离开了这个城镇,看见一位名叫利未的税吏坐在交税亭处,于是对他说:“跟随我吧!”
Baada ya hayo, Yesu akatoka nje, akamwona mtoza ushuru mmoja aitwaye Lawi, ameketi ofisini. Yesu akamwambia, “Nifuate!”
28 于是利末站起来放下一切,决定跟随耶稣。
Lawi akaacha yote, akamfuata.
29 利未在自己家中大摆宴席,客人中除了很多税吏,还有其他一些人。但法利赛人和宗教老师开始抱怨耶稣的门徒,说:
Kisha Lawi akamwandalia Yesu karamu kubwa nyumbani mwake; na kundi kubwa la watoza ushuru na watu wengine walikuwa wameketi pamoja nao.
30 “你们为什么要跟税吏和那些罪人一起吃喝呢?”
Mafarisayo na walimu wa Sheria wakawanung'unikia wafuasi wake wakisema: “Mbona mnakula na kunywa pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?”
31 耶稣回答:“健康之人不需要医生,病患才需要。
Yesu akawajibu, “Wenye afya hawahitaji daktari, lakini wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa.
32 我来这里并非感召正道之人,而是要召唤罪人。”
Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu.”
33 他们对耶稣说:“约翰的门徒经常禁食和祈祷,法利赛人的门徒也是,但你的门徒却大吃大喝。”
Watu wengine wakamwambia Yesu, “Wafuasi wa Yohane mbatizaji hufunga mara nyingi na kusali; hata wafuasi wa Mafarisayo hufanya vivyo hivyo. Lakini wafuasi wako hula na kunywa.”
34 耶稣又问:“男傧相和新郎在一起时,怎么可以让男傧相禁食呢?
Yesu akawajibu, “Je, mnaweza kuwataka wale walioalikwa arusini wafunge hali bwana arusi yuko pamoja nao?
35 时间一到,新郎要离开大家了,那一刻他们就要禁食了。”
Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kati yao, na wakati huo ndipo watakapofunga.”
36 耶稣又讲了一个比喻:“没有人会从新衣服上撕下一块布,补在旧衣服上。如果这样,不但新衣服撕破了,新撕下来的布与旧衣服也不协调。
Yesu akawaambia mfano huu: “Hakuna mtu akataye kiraka cha nguo mpya na kukitia katika vazi kuukuu; kama akifanya hivyo, atakuwa amelikata hilo vazi jipya, na hicho kiraka hakitachukuana na hilo vazi kuukuu.
37 没有人会把新酒装在旧皮袋中,否则新酒就会把皮袋胀破,不但酒漏掉了,皮袋也损坏了。
Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; kwani hiyo divai mpya itavipasua hivyo viriba, divai itamwagika, na viriba vitaharibika.
38 人们总是把新酒放在新皮袋里。
Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!
39 人们喝了陈酿的酒,就不想喝新酒了,他们会说:‘陈酿的口味就是好。’”
Wala hakuna mtu ambaye hutamani kunywa divai mpya baada ya kunywa ya zamani, kwani husema: Ile ya zamani ni nzuri zaidi.”

< 路加福音 5 >