< 路加福音 15 >

1 很多税吏和其他“罪人”经常来到耶稣那里,听他讲道。
Siku moja, watoza ushuru na wahalifu wengi walikwenda kumsikiliza Yesu.
2 于是法利赛人和宗教老师抱怨到:“这个人欢迎罪人,还和他们一起吃饭。”
Mafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunung'unika: “Mtazameni mtu huyu! Anawakaribisha wenye dhambi, na tena anakula nao.”
3 耶稣就对他们讲了一个故事,说:
Yesu akawajibu kwa mfano:
4 “如果你有一百只羊,失去一只,是不是会把剩下的九十九只留在开阔牧场,然后去寻找那丢失的羊,直到找到为止?
“Hivi, mtu akiwa na kondoo mia, akigundua kwamba mmoja wao amepotea, atafanya nini? Atawaacha wale tisini na tisa mbugani, na kwenda kumtafuta yule aliyepotea mpaka ampate.
5 如果你找着了,就会高兴地把羊扛在肩上,
Akimpata, atambeba mabegani kwa furaha.
6 回到家后招呼朋友和邻居来,对他们说:‘来和我一同庆祝吧,因为我找到了丢失的羊!’
Anapofika nyumbani, atawaita rafiki zake akiwaambia, Furahini pamoja nami, kwa sababu nimempata yule kondoo wangu aliyepotea.
7 告诉你们,一个罪人若能悔改,天堂就会获得更多欢乐,甚至超过九十九个不用悔改的良善之人。
Kadhalika nawaambieni, ndivyo kutakavyokuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya kutubu kwa mwenye dhambi mmoja, kuliko kwa ajili ya watu tisini na tisa wanaojiona kuwa wema, wasiohitaji kutubu.
8 假设一个女人有十枚银币,如果丢了一枚,是不是要点上灯,在整个屋子里细细寻找,直到找到?
“Au mwaonaje? Tuseme mwanamke fulani ana sarafu kumi za fedha, akipoteza moja, atafanya nini? Atawasha taa, aifagie nyumba na kuitafuta kwa uangalifu mpaka aipate.
9 当她找到那枚银币,就会叫来亲朋好友,对他们说:‘来和我一同庆祝吧,因为我找到了丢失的银币!’
Akiipata, atawaita rafiki na jirani zake akisema, Furahini pamoja nami, kwa sababu nimeipata ile sarafu yangu iliyopotea.
10 我告诉你们,一个罪人若能悔改,上帝的天使也会感到欢乐。”
Kadhalika nawaambieni, ndivyo watakavyofurahi malaika wa Mungu kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja anayetubu.”
11 耶稣解释道:“从前有个人有两个儿子。
Yesu akaendelea kusema, “Kulikuwa na mtu mmoja mwenye wana wawili.
12 小儿子对父亲说:‘爸爸,请把我应得的家产分给我。’于是父亲就把财产分给兄弟二人。
Yule mdogo, alimwambia baba yake: Baba, nipe urithi wangu. Naye akawagawia mali yake.
13 几天后,小儿子带上所有的家当去了远方,在那里过着放荡的生活,奢侈浪费。
Baada ya siku chache, yule mdogo aliuza urithi wake, akasafiri na fedha aliyopata, akaenda nchi ya mbali ambako aliitumia ovyo.
14 他花光了所有钱财,又恰逢当地遇上严重饥荒,他穷得肚子都吃不饱。
Alipomaliza kutumia kila kitu, kukatokea njaa kali katika nchi ile, naye akaanza kuhangaika.
15 于是他在当地一个农户那里找差事做。那人打发他到田里去放猪,
Akaomba kazi kwa mwananchi mtu mmoja wa huko naye akampeleka shambani mwake kulisha nguruwe.
16 他太饿了,甚至愿意吃猪食,但即使这样也没有人愿意给他食物。
Alitamani kula maganda waliyokula wale nguruwe, ila hakuna mtu aliyempa kitu.
17 他这时才幡然醒悟,于是对自己说:‘我父亲所有的工人都有丰盛的食物可以享用,为什么我却要在这里饿死?
Alipoanza kupata akili akafikiri: Mbona kuna wafanyakazi wengi wa baba yangu wanaokula na kusaza, nami ninakufa njaa?
18 我要回家,到我父亲那里去!对他说:父亲,我的罪违背了天堂,也违背了你,
Nitarudi kwa baba yangu na kumwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia.
19 我不配再做你的儿子,请向对待雇工那样对待我吧。’
Sistahili hata kuitwa mwanao. Nifanye kama mmoja wa wafanyakazi wako.
20 于是他动身回家去找他的父亲。 当他父亲看到他的身影,尽管还在远处,便动了恻隐之心,跑过去拥抱他,亲吻他。
Basi, akaanza safari ya kurudi kwa baba yake. Alipokuwa bado yu mbali, baba yake alimwona, na kwa moyo wa huruma alimkimbilia, akamkumbatia na kumbusu.
21 儿子说:‘父亲,我违背了天堂也违背了你,不配再做你的儿子。’
“Mwanawe akamwambia: Baba, nimemkosea Mungu, na nimekukosea wewe pia. Sistahili hata kuitwa mwanao.
22 但父亲却吩咐仆人说:‘快把那最好的长袍拿来给他穿,给他戴上戒指,穿上鞋。
Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: Haraka! Leteni nguo nzuri mkamvike! Mvisheni pete na viatu!
23 把我们养肥的牛犊宰了,我们要大吃一顿,
Mchinjeni ndama mnono; tule kusherehekea!
24 因为这可是我死而复活、失而复得的儿子。’于是他们开始庆祝起来。
Kwa sababu huyu mwanangu alikuwa amekufa, kumbe yu mzima alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana. Wakaanza kufanya sherehe.
25 这时候大儿子正在田里干活。他朝着家的方向走去,听见音乐和跳舞的声音,
“Wakati huo kaka yake alikuwa bado shambani. Alipokuwa akirudi na kukaribia nyumbani akasikia vifijo na ngoma.
26 于是就找来一个仆人,询问发生了什么。
Akamwita mmoja wa watumishi, akamwuliza: Kuna nini?
27 仆人说:‘你弟弟回来了,你父亲因为他平安归来,就宰了那头肥牛犊。’
Huyo mtumishi akamwambia: Ndugu yako amerudi nyumbani, na baba yako amemchinjia ndama mnono kwa kuwa amempata akiwa salama salimini.
28 大儿子很生气,不肯走进屋子里,于是父亲出来劝他。
Huyo kijana mkubwa akawaka hasira hata akakataa kuingia nyumbani. Baba yake akatoka nje na kumsihi aingie.
29 他对父亲说:‘你看,我照顾你这么多年,从来没有违背过你的命令,但你从未给我任何羊羔,让我可以和朋友们聚会。
Lakini yeye akamjibu: Kumbuka! Miaka yote nimekutumikia, sijavunja amri yako hata mara moja. Umenipa nini? Hujanipa hata mwana mbuzi mmoja nikafanye sherehe pamoja na rafiki zangu!
30 但你这个儿子,把你的钱都浪费在妓女身上,他一回来,你反倒为他宰杀肥牛犊!’
Lakini mtoto wako huyu aliyekula mali yako pamoja na makahaba, mara tu alipokuja umemchinjia yule ndama mnono.
31 父亲对他说:‘孩子,你总是跟我在一起,我的一切都是你的。
Baba yake akamjibu: Mwanangu, wewe uko pamoja nami siku zote, na kila nilicho nacho ni chako.
32 但你这个弟弟是死而复活、失而复得,所以我们应该高兴,应该庆祝!’”
Ilitubidi kufanya sherehe na kufurahi, kwa sababu huyu ndugu yako alikuwa amekufa, kumbe yu mzima; alikuwa amepotea, lakini sasa amepatikana.”

< 路加福音 15 >