< Luk 1 >

1 Ka talue poung e Theophilus, maimouh dawk kamnuek tangcoung e a konglamnaw hah,
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 apuengcue hoi kahmawt ni teh kapanuekkhainaw hoi lawk dawk thaw katawknaw ni maimouh koe a dei tangcoung e patetlah tami moikapap ni ca lahoi thut hanelah a panki awh.
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 Kai ni hai apuengcue hoi ka kamtu e a konglamnaw pueng teh atang katang tie na panue thai nahanelah,
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 hote konglamnaw teh nang koe pou hruek hane kawi lah ao telah ka pouk.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 Judah ram ka uk e Herod Siangpahrang kut rahim vah Abijah tie vaihma miphun dawk hoi e vaihma Zekhariah teh ao. Ahnie a yu teh Aron e catoun, a min teh Elizabeth,
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 ahnimouh roi teh kâpoelawknaw pueng a tarawi roi, tounhoehe lah ao teh, Cathut hmalah tamikalan lah ao roi.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 Elizabeth teh carôe dawkvah ahnimouh roi teh ca tawn roi hoeh. A kum haiyah a cue poung roi toe.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Hatnavah, Zekhariah teh amae a huinaw hoi cungtalah atueng a pha toung dawkvah, Cathut hmalah vaihma thaw a tawk lahun nah,
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 vaihmanaw e singyoe patetlah cungpam a khoe. Cathut e bawkim thung a kâen teh hmuitui hmai sawinae a sak.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 Hottelah Cathut koe a sak lahun navah taminaw pueng teh alawilah a ratoum awh.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 Hatnavah Cathut e kalvantami teh Zekhariah hmalah a kamnue teh hmuitui hmaisawi thuengnae aranglah a kangdue.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 Zekhariah ni a hmu navah a kalue teh a taki.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 Kalvantami ni Zekhariah taket hanh, nange ratoumnae teh Cathut ni a thai toe. Na yu Elizabeth teh ca tongpa a khe han, a min teh Jawhan telah na phung han.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 Nang teh na konawm vaiteh na lunghawi han, hote ca tongpa na khe kecu dawk taminaw pueng hai a konawm awh han.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 Bangkongtetpawiteh, ahni teh Cathut hmalah ka talue e tami lah ao han. Misurtui hoi parui kawinaw pueng net mahoeh. A manu e von thung ao nahoi Kathoung Muitha hoi akawi han.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 Ahni ni Isarel catounnaw moikapap Cathut koe lah a kamlang sak han.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 Ahni teh Cathut ni a tha e laicei lah ao vaiteh Profet Elijah patetlah muitha hnotithainae hoi kakawi e tami lah ao han. A napanaw hoi a capanaw kâpo sak vaiteh lawk ka ngai hoeh e taminaw hah tami kalannaw e lungangnae lam koe lah bout a hrawi han. Cathut e taminaw teh Bawipa hanelah coungkacoe lah ao thai nahan kârakueng awh telah a dei.
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 Zekhariah ni kalvantami koevah hote hno a coung thai han doeh telah bangtelah hoi maw ka panue thai han. Bangkongtetpawiteh, kai teh, ka matawng toe, ka yu hai a matawng toe telah atipouh.
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 Kalvantami ni kai teh Gabriel doeh, hete lunghawinae kamthang nang koe dei hanelah, na ka patoun e Cathut hmalah ka kangdout e doeh.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 Nang teh kaie lawk na tang hoeh dawkvah hete hno a kuep hoehnahlan totouh lawk dei thai laipalah, na lawk a a han. Kaie ka lawk teh atueng a pha toteh a kuep han telah a dei pouh.
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 Taminaw ni Zekhariah teh ngaihawi laihoi a ring awh teh bangkongmaw bawkim thung atu sittouh a o vaw titeh a kângairukhai awh.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 Ahni teh bawkim thung hoi a tâco navah lawk a dei thai hoeh dawkvah, kamnuenae a hmu telah a panue awh. Zekhariah teh a lawk a a dawkvah a kut khok hoi ahnimanaw koe a yavai pouh
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 Vaihma thaw a tawk e atueng abaw hnukkhu Zekhariah teh im lah a ban.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 Hathnukkhu hoi a yu Elizabeth teh camo a neng dawkvah thapa yung panga touh imthungkhu a kamung.
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 Cathut ni taminaw e hmalah kaie yeiraiponae pueng na la pouh toe a ti.
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 Thapa yung taruk navah Cathut ni kalvantami Gabriel koe, Galilee ram Nazareth kho dawk kaawm e tangla koe a patoun.
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 Hote tangla teh Devit miphun a min Joseph ka kâphung e tami hoi kâhâ tangcoung e lah ao. A min teh Meri doeh.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 Kalvantami ni Meri koe a tho teh na konawm haw, yawhawinae ka coe e napui nang teh Cathut ni na okhai telah atipouh.
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 Meri ni hote lawk a thai navah a lungtâsue teh hote lawk teh bangpatet e lawk maw ati teh a kâpouk.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 Kalvantami ni hai Meri na lungpuen hanh. Nang teh Cathut koe minhmai kahawi na hmu toe.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 Nang teh camo na neng vaiteh ca tongpa na khe han, a min teh Jisuh telah na phung han.
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 Hote capa teh ka lentoe poung e tami lah ao vaiteh Lathueng Poung e Capa telah kaw lah ao han. Cathut ni ahni teh a na pa Devit e bawitungkhung a poe han.
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 Ahni ni Jakop catounnaw hah pout laipalah a uk han. Ahnie uknaeram teh poutnae awm mahoeh telah atipouh. (aiōn g165)
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
34 Meri ni kai teh tongpa hoi kâ panuenae awmhoeh rah, hete hno heh kai koe bangtelamaw a coung thai han telah kalvantami hah a pacei.
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 Kalvantami ni Kathoung Muitha nang dawk a pha toteh Lathueng Poung e bahu nang dawk ao han. Hatdawkvah khe lah kaawm e kathounge camo hah Cathut capa telah kaw lah ao han.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 Hothloilah cakaroe telah kaw e nange na hui Elizabeth teh camo a nengnae thapa yung taruk touh a pha toe.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 Cathut hanelah ka coung thai hoeh e hno buet touh hai awm hoeh telah bout a dei pouh.
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 Meri ni kai teh Cathut e a sannu doeh, Bawipa e lawk patetlah kai dawk kuep lawiseh telah a dei pouh hnukkhu kalvantami ni a ceitakhai.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Hathnukkhu Meri ni, Judah ram mon dawk kaawm e kho buet touh dawk karanglah a cei hnukkhu,
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 Zekhariah im dawk a kâen teh Elizabeth a pato.
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 Meri ni a patonae lawk Elizabeth ni a thai navah a von thung e camo teh a kâroe. Elizabeth teh Kathoung Muitha hoi akawi teh,
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 nang teh napuinaw pueng hlak yawkahawipoung e lah na o. Nange na von thung kaawm e camo hai a yawkahawi e tami doeh.
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 Ka Bawipa e a manu ni kai koe a pha navah yawhawinae bangkongmaw kai ni ka coe.
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 Nange na lawk kai ni ka thai navah kaie ka von thung e camo teh a lunghawi teh a coukdouk.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 Bawipa ni a dei e lawk a kuep mingming han doeh telah ka yuem e napui teh a yawkahawi e doeh telah a hram laihoi a dei.
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 Meri nihai, ka lungthin ni Cathut a pholen teh,
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 ka muitha ni ka rungngangkung Cathut dawk a lunghawi.
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 Bangkongtetpawiteh, amamae a sannu a kârahnoumnae na hmu pouh toe. Atu hoi hmalah ka tho hane a tami pueng ni a yawkahawi e tami telah na dei awh han.
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 Athaonae hoi kakawi e Cathut ni hno kalen kai hanlah na sak pouh toe. A min teh thoung raw naseh.
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 Cathut ka taket e taminaw teh Bawipa e pahrennae ahnimouh dawk pou a kangning.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 A kut hoi a hnotithainae teh a kamnue sak toe. Kâoupkâpawi e taminaw teh koung kathek kayak awh toe.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 Bawitungkhungnaw dawk hoi khobawinaw a pabo teh, ka kârahnoum e taminaw a tawmdawm toe.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 A von kahlamnaw ka boum ca lah a paca vaiteh, katangrengnaw a kuthrawng lah a ban sak toe.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 Maimae mintoenaw ni a dei e patetlah,
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 Abraham koehoi a catounnaw koe pahrennae pou a sak hanelah a pouk teh, amae san Isarelnaw a tawmdawm toe telah atipouh. (aiōn g165)
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
56 Meri teh Elizabeth koe thapa yung thum touh ao hnukkhu a ma im bout a ban.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 Elizabeth teh a khenae hnin thapa a kuep navah ca tongpa teh a khe.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 Cathut ni ka taluepoung e pahrennae Elizabeth koe a kamnue sak e hah imteng e a huikonaw ni a thai navah, ahni hoi cungtalah a konawm awh.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 Ataroe hnin vah, camo e vuensoma hanelah, a tho awh teh, a na pa e a min Zekhariah patetlah phung hane a kâdei awh.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 A manu ni telah na phung mahoeh, Jawhan telah na phung han atipouh.
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 Ahnimouh ni hai, nangmae miphun dawk telah min phung e tami buet touh hai awmhoeh rah atipouh awh.
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 Hathnukkhu, a na pa ni bangtelamaw phung han a ngai telah a pacei awh.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 A na pa ni hai calung a hei teh Jawhan telah a min a thut navah, taminaw pueng ni kângai a ru awh.
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 Telah a thut tahma vah Zekhariah teh lawk bout a dei thai teh Cathut a pholen.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 Imteng kaawmnaw pueng ni a taki awh teh, hete a konglamnaw pueng teh Judah ram pueng koe koung a kamthang.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 Ka thai e naw pueng ni a lung thung a pâkuem awh teh, hete camo teh bangpatet e tami lah maw ao han titeh a kâpankhai awh. Bangkongtetpawiteh Bawipa e hnotithainae teh camo hoi cungtalah ao.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 Camo e a na pa Zekhariah teh, Kathoung Muitha hoi akawi teh profet lawk a dei,
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 Isarelnaw e kahring Cathut teh yawhawinae awmseh. Bangkongtetpawiteh Bawipa ni amae a taminaw na kountouk teh ratangnae na sak pouh toe.
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 Talaivan pek kamtawng hoi amae profet kathoungnaw ni a dei e patetlah,
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 maimouh hanelah rungngangnae ki teh a sanpa Devit e catoun dawk hoi a tho sak toe. (aiōn g165)
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
71 Hete hloutnae teh maimouh na ka taran e naw hoi ka maithoe e naw pueng, kut dawk hoi hloutnae doeh.
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 Maimae mintoenaw koe lung na patawnae kamnue sak hane hoi,
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 maimanaw taran kut dawk hoi na rungngang vaiteh,
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 hringyung lam lungpuennae tawn laipalah thoungnae, lannae lahoi Cathut bawk thai nahan,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 maimae na pa Abraham koe thoungnae lawk a kam e hah pahnim hoeh nahanelah doeh.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 Camo nang, nang hai Lathueng Poung e profet telah na kaw awh han.
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 Bangkongtetpawiteh, maimae Cathut ni yonnae a ngaithoum teh rungngangnae dawk pha thainae a kong hah, amae taminaw koe pâpho vaiteh, Cathut e lamthung rakueng hanelah, nang teh hmalah na cei han.
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 Hote pahrennae lahoi kalvan hoi kanî raeng maimouh dawk a pha teh,
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 hmonae hoi duenae tâhlip dawk kaawm e naw koe a ang vaiteh, maimouh koe roumnae lamthung na patue awh han telah a dei.
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 Hote camo teh, a roung takhang teh muitha thaonae hoi akawi. Isarel miphunnaw koe a kamnue hoehroukrak thingyeiyawn vah ao.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.

< Luk 1 >