< 1 Samuel 1 >

1 Masang laiyin Elkanah kiti mikhat Ramah kho thinglhang gam molsang Ramathiam Zophim mun’ah anacheng in ahi. Ama chu Jeroham chapa, Elihu chapa, Tohu chapa, Zuph chapa, Ephriam mi ahi.
Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.
2 Elkanah in ji ni aneiyin, Hannah le Peninnah ahi. Peninnah in cha aneiyin, ahin Hannah vang'in aneipoi.
Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.
3 Elkanah hi kumseh leh Shiloh a Pakai van gam sepaite henga gan kilhaina maicham semdin acheyin ahi. Hiche lai chun Eli Pakai thempupan chapa ni aneiyin ahi, amani min chu Hopni le Phinehe ahilhone.
Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana.
4 Elkanah hin gan kilhaina abolni tengle achan dingdol sachan chu Peninnah le achate apeyin ahi.
Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.
5 Chule Hannah angailut jeh chun, Pakaiyin anaobu akhapeh jeh chun, sachan chan khat bou apeyin ahi.
Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
6 Chumale Pakaiyin Hannah chu anaobu akhapeh jeh chun, Peninnah in jong Hannah chu noise tah in alunghan han nadin totnopnan abolyin ahi.
Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi.
7 Kumlhun seh leh abang bang ahiyingin-Hannah Pakai hou dinga Houin'a achetengle Peninnah kitinu hin phin lunghang jin, hijeh chun amanu akapin anjong aneji tapon ahi.
Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.
8 “Ipi jeh’a naka ham, Hannah?” Elkanah in adongin, “Ibola an nelouva umah nahim? Chule ibola lungkhama um nahim? Kei neinei hime-chapa somkhat neiho sanga kaphatchom joh louham? ati.
Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”
9 Amahon Shiloh’a gan kilhaina anneh, twidon achaiphat’un, Hannah akipatdoh in taoding in achetai. Eli thempu chu Pakai houin khombul khatna touna chunga touva ahi.
Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana.
10 Hannah vang chu lhase beh seh jengin, Pakai henga ataovin, lhasetah in akapjah in ahi.
Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana.
11 Chule amanun kitepna khat aneiyin, “O Van gam Sepaite Pakai, gentheiya ka kana neihin velhin lang kataona neihin ngailhah peh inlang ‘chapa khat neipetan,’” ati.
Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”
12 Amanu Pakai henga ataopet’in Eli thempun ane phunchu ana mulhin ahi.
Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake.
13 Anephu achaloh chu amun, ahinlah ataogin aw chu ajapoi, ageldan in amanu hin ju adonkham hinte ati ahi.
Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa
14 Aman Hannah jah’a “Hilai munna hi jukham puma nahung ham? Najukham chu paidoh loijin,” ati.
naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”
15 “Kahipoi, kapu!” tin adonbut’e, “Keiman ju kadonpoi, chule khamnathei ho jong kadonpoi, ahinlah kei hi numei genthei chungnung kahi, Pakai agsunga hi kahinna pumpia thuseijoh kahibouve,” ati.
Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana.
16 “Keima numei phalouvin neigel hihbeh in! Ahinlah lung genthei puma taojing jengjoh kahibouve,” ati.
Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”
17 Hiche chung thu ahin Elin hitin ana seipeh in ahi, “Lungmongin chetan, Israel Pathen in nathilthum jouse chu nasan peh intin phatthei naboh hen.”
Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”
18 Hannah in jong, “Oh hepu kakipah e!” atin, akinunglen an anepantai, alungkham tapon ahi.
Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.
19 Ajingkah khovah matah’in ainsung pumpi athouvun, Pakai houkit dingin ache tauve. Chujou’in ain’u Ramah ah ahung kile kit tauvin ahi.
Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka.
20 Chule Hannah chun aphat chan, naosen pasal khat aneitai. Amanun jong amin Samuel asahtai, ajeh chu “Ama ding’a hi Pakai koma kathum ahi,” ati.
Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”
21 Akum kit’in Elkanah le ainsung mite jouse kum kichaiya gan kilhaina-a Pakai hou ding in akitol kit tauve.
Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake,
22 Ahinlah Hannah chu anache tapon ahi. Ainneipu komah hitin aseiyin, “Naosen aletdom kahsen ngah hitin kumkit tengle keiman hinpui ingting, imatih chana dingin Pakai toh umden tante,” ati.
Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”
23 Nasei chu aphaselle tin Elkanah in pha asatai. “Tutadin hichea hin uminlang, Pakaiyin nakitepna bang in napanpi hen.” Hijeh chun amanu inah aumin, naosen aletdom kahsen aumpin ahi.
Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.
24 Chuin naosen ahunglet domphat in, Hannah in Shiloh a pon-in ah ahinpuiyin ahi. Amahon bongchal kumthum lhingsa khat toh ahinpui thauvin, changbong neldisel Ephah dimkhat toh apon lengpitwi peng thei khat dimset toh akidop’in naosen chapang chu Shiloh khoa Pakai houna in ah ahin puilut tai, naosen chu chapang chabou ahi nalaiye.
Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo.
25 Bongchal atha jou phat’un amahon naosen chu Eli thempu kom ahin puilut tauve.
Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,
26 “Kapuu, neigeldoh em?” tin Hannah in adong in ahi. “Keima kum tampi hilai muna Pakai henga anatao jing numei nu chu kahi,” ati.
naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana.
27 “Pakai koma hiche chapa hi eipeh dia ana taojing kahin, Pakaiyin kataona eidonbut pen tan ahi,” ati.
Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba.
28 “Tun keiman amahi Pakai henga kahin pehdoh ahitai. Ahinkho lhumkeiya dinga kapehdoh ahitai. Hichun amahon hikoma chun Pakai chibai aboh tauve.
Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.

< 1 Samuel 1 >