< Luhka 4 >

1 Jesuh Ngmüimkhya Ngcim am beki, Jordan tuinu üngka naw a nghlat law be üng Ngmüimkhya naw khawkhyawng khawa cehpüi se,
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 mhmüp kphyükip khawyai naw a hlawhlep. Acunüng ipi am ei se, anghnua a ei cawi lawki.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 Khawyai naw, “Nang Mhnama capa na kyak üng, hina lung muka ngthawn law khaia ngthu pea,” a ti.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 Acunsepi Jesuh naw msang lü, “Khyang cun ei däng üng am xüng, tia cangcim üng ng’yuki,” a ti.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 Acunüng khawyai naw Jesuh khawmcung a hlüngnaka kaipüiki naw khawmdeka khana khawe avan mik mkhyüp üng jah mhmuh lü,
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 “Hin he avan ka veia peta kyaki, upi ka ngaih üng ka peki, hina ana avan la a kyäpsawknak avan ka ning pe khai,
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 acunakyase na sawhkhah lü, avan na kaa kya khai,” a ti.
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 Jesuh naw a veia, “Cangcim üng, ‘Na Bawipa Pamhnam sawhkhah lü, ani däng na khüih vai,’ tia ng’yuki,’” a ti.
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 Acunüng khawyai naw Jerusalema cehpüiki naw, Temple khan, amsumnaka ta lü, “Mhnama capa na kyak üng hin üngka naw mcea namät kcoa,
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 ‘Ani naw khankhawngsä he ning na k’äih u lü, ning na mcei khai hea jah mcawn khai,
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 na khaw am lung am na su khaia, ami kut am ning na mcei khai he’ tia, ng’yüki,” a ti.
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 Cunsepi Jesuh naw, “Na Bawipa, Pamhnam ä na mhnütei vai,’ tia kyaki ni,” ti lü a msang.
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 Acunüng khawyai naw a hlawhlepnak vai avan am a hlawhlep käna asäng a ceh tak ma.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 Acunüng Jesuh, Ngmüimkhya Ngcima khyaihnak am Kalilea nghlat be se, a mawng cun acuna khaw pei avan üng ngthang hüki.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 Acunüng sinakoka jah mthei hü se, khyang avan naw ngak u lü, ami mhlünmtai.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 Acunüng angvainak Nazareta a law be üng a thum khawia kba Sabbath mhmüp üng, Sinakoka k'uma lut lü ngthungcim khe khaia ngdüiki.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 Acunüng sahma Hesajah cauk ami pet. Acunüng cauk ktawm a kphyan üng hinkba angyuknak a kheh,
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 “Bawipa Ngmüimkhya ka khana awmki, ani naw thangkdaw m'yyenkse hea veia ka sang khaia a na xü. Ami mlung naki he ka jah mhlät be khai, khuikhaki hea veia lätnaka thangkdaw ka sang khai, amikmü he ka jah mdaw be khai, ami jah man he ka jah mhlät khaia la,
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 Bawipa naw a khyang he a jah küikyanak vaia kcün pha lawki ti, ka sang khaia ana tüih law ni,” tia kyaki.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 Jesuh naw cauk ktawmki naw jah pe be lü ngawki. Acunüng Sinakoka k'uma ngawki he avan naw kcävä u lü ami teng.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 Acunüng Jesuh naw, “Tuhngawi hina thungcim nami sim kümkawi law ve,” a ti.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 Acunüng ami van naw, a ngthu pyen cun aktäa ngai hlü u lü, aktäa kyühkhyai u lü, “Hin hin Josepa capa am kyakia kya aih se,” ami ti.
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 Jesuh naw, “Hina msuimcäpnak, ‘Sibawi, namät la namät m’yai bea! Ipi Kapenawm khawa pawh hina khaw üng pi pawh lü mdang lawa’ nami ti khai,” a ti.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 Acunüng Jesuh naw, “Akcanga ka ning jah mthehki, sahma cun amäta khawa am dokhamei khawi u.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 “Cunsepi ka ning jah mthehki, Elijaha kcün üng, khawkum kthum la khya khyuk khaw am a se, khaw avan üng khaw a set law üng, hmeinu khawjah Isarel khawa awmki he,
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 cunsepi ua veia pi Elijah tüiha am kya naw, Sidon khaw da Sarepta khawa hmeinu mata veia ni tüiha akya ve.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 “Acunüng sahma Elishaa kcün üng pi Isarel khawa mnehkse mnehki khawjah awmki he; cunsepi Naman, Siria khawa ka dänga thea upi ngcimsak bea am kya naw,” a ti.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 Acunüng Sinakoka k'uma awmki he ami van acun ami ngjak üng, aktäa ami mlung soki.
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 Acunüng tho law u lü, mlüh üngka naw ktämki he naw ami mlüha awmnak mcunga khana ami buhtawn vaia ami cehpüi.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 Cunsepi Jesuh ami ksunga ngjui lü akcea citeiki.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 Acunüng Jesuh naw Kalile mlüh, Kapenawma cit lü Sabbath mhmüp üng a jah mthei.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 A ngthu pyen ana a awma phäha aktäa cäicah lawki he.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 Acunüng Sinakoka k'uma khyang mat ngmüimkhya ksea awmnak awmki cun,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 “Nazaret Jesuh, i mi nglak awm se ni? Jah mkhyüh khaia na lawki aw? Nang ka ning ksingki, nang Mhnama ngsä ngcima na kyaki ni,” ti lü ngpyangki.
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 Jesuh naw, “Ä khikheh lü a k'um üngka naw lut law,” ti lü jüi se, acunüng khawyai naw khyang hea maa mkhyu lü, ia pi am pawh lü a ceh tak.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 Acunüng awmki he ami van naw cäi u lü, “Hin hin ia ngthu ni? Ana la khyaihnak am khawyai kse he jah jüi se lut lawki he hin,” tia ngthäh kyuki he.
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 Acunüng acuna pipei, khaw avan üng a mawng ngthang hüki.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 Jesuh Sinakok üngka naw ktawih lü Sihmona ima citki. Acuia Sihmona pi aktäa mhnatei se ami mtheh.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 Jesuh naw a peia ngdüi lü a mhnat jüi se mhnat naw a khyah. Acunüng angxita tho law lü a jah khüih.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 Acunüng khaw kya se, natnak akce kcea jah hui, am phetki he avan a veia ami jah lawpüi; acunüng ami vana khana a kut mtaih lü a jah m’yai be.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Khawyai he naw, “Pamhnama Capa na kyaki ni,” tia, ngpyang u lü, khyang khawjaha k'um üngka naw lut lawki he. Acunüng Jesuh naw jah jüi se, Mesijaha kyaki ti ami ksinga phäha am a jah ngthuhei sak.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 Khawa thaih law la, Jesuh mlüh ktawi ta lü angkhyinaka cit se, khyang he naw sui u lü a veia law siki he naw, am a jah ceh tak vaia ami khyawh.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 Cunsepi Jesuh naw, “Pung kcea pi Pamhnama khawa mawng thangkdaw ka pyen khaia kyaki, acun vaia tüih lawa ka kyaki ni,” a ti.
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 Acunakyase acuna khawaa awmkia Sinakok hea k'uma ngthu sang hüki.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luhka 4 >